EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, November 16, 2012

Kawemba afagilia uozo marefa Ligi Kuu.

Na Salum Mkandemba wa Tanzania Daima.
WAKATI malalamiko kwa waamuzi wa Ligi Kuu Tanzania Bara kuhusu kuboronga yakishika kasi, Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Saad Kawemba, amewakingia kifua na kudai uamuzi wa haki zaidi ya walioutoa haupatikani duniani.

Akizungumza na kipindi cha Tuongee Asubuhi – Michezo, kinachorushwa na kituo cha Star TV cha jijini Mwanza kila siku za Alhamisi, Kawemba alisema kuwa kamati yake imeridhishwa na kiwango cha uchezeshaji cha waamuzi hao, licha ya kukiri kuwapo kwa kasoro kadhaa, akidai ni za kibinadamu.

Kawemba alisema kuwa waamuzi kama walivyo binadamu wengine, hawawezi kufanya uamuzi wa kumfurahisha kila mmoja, huku akidai, kutovunjika mechi yoyote kutokana na uamuzi wao, ni uthibitisho mwingine kwamba walikuwa makini katika mechi hizo.
“Niseme ukweli kiwango cha uchezeshaji wao kilikuwa kizuri na kimetuvutia. Najua wapo ambao hawakupendezwa nayo, lakini ndivyo binadamu tulivyo. Haki ya kiwango hicho hupatikana mbinguni, sio duniani,” alisema Kawemba aliyekuwa akizungumzia usajili wa dirisha dogo Januari mwakani.

Kawemba alisema kuwa hatua kali kwa waamuzi wabovu na wazembe zilizochukuliwa mapema mwanzoni mwa msimu huu wa 2012/13, zilisaidia kuongeza umakini miongoni mwao, kiasi cha kuimarisha utendaji wao dimbani hadi kumalizika kwa mzunguko wa kwanza.
Akaenda mbali zaidi na kukosoa kauli za makocha wa klabu za Ligi Kuu, juu malalamiko yao kuwa viwanja vibovu mikoani ndiyo chanzo cha matokeo mabovu ya timu zao na kuwataka kufanya tathmini za matokeo chanya pindi zinaposhinda na sio kutathmini matokeo hasi tu.

“Sisi kama TFF tunaishukuru sana serikali kwa kukubali kutupa Uwanja wa Taifa kwa matumizi ya Ligi Kuu. Haiwezekani viwanja vyote vikawa kama ule, fursa tuliyopata ya kuutumia, isiwalemaze baadhi ya makocha kiasi cha kutarajia viwanja vyote nchini kuwa kama Taifa,” alisaema.
Katika mzunguko wa kwanza uliofikia tamati hivi karibuni, kilio kikubwa kilikuwa ni kuvurunda kwa waamuzi wa Ligi Kuu, kulikotokana na ama kushindwa kutafsiri sheria au upindishaji wa kawaida, utokanao na mapenzi au rushwa, kitu kilichothibitishwa na kuondolewa au kufungiwa kwa baadhi yao.

Baadhi ya waamuzi waliokumbana na adhabu za kufungiwa, kuondolewa au kuonywa katika Ligi Kuu kutokana na kuvurunda ni pamoja na Mathew Akrama na Paul Soleji wa Mwanza, Ephraim Ndissa, Mwarabu Mumbi, Ronald Swai na Kamishna Pius Mashera.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate