EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, November 22, 2012

Jela maisha kwa kubaka, kuambukiza ukimwi.

MAHAKAMA ya Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, imewahukumu kifungo cha maisha vijana wawili kwa makosa mawili ya ubakaji na kumuambukiza ugonjwa wa ukimwi mtoto wa miaka minne.

Akitoa hukumu hizo kwa nyakati tofauti, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Ushindi Swalo, alisema mahakama imeridhishwa na ushahidi uliotolewa huku mmoja wa watuhumiwa hao akikiri kutenda kosa hilo la kumbaka mtoto wa miaka minne.
Katika tukio la kwanza, Mwendesha Mashtaka wa mahakama hiyo, Zephania Mnisi, alisema kuwa Desemba 21 mwaka jana, mshitakiwa Revocatus Mihayo (25) alimbaka mtoto wa miaka minne katika Kijiji cha Msonga wilayani Bukombe.

Mnisi aliiambia mahakama hiyo kuwa katika tukio hilo, Mihayo alikamatwa akiwa amempakata mtoto huyo mapajani, huku akimbaka na uchunguzi wa awali wa daktari ulionesha alikuwa ameharibika sehemu zake za siri.
Alisema wakati kesi hiyo ikiendelea na miezi kadhaa ikipita, mtoto huyo alifanyiwa uchunguzi wa daktari kwa mara ya pili na kubainika tayari ameambukizwa virusi vya ukimwi, shitaka ambalo liliongezwa kwenye kesi yake ya msingi ya ubakaji.

Katika shtaka la pili, Shija Marko (18) mkazi wa Lulembera anadaiwa kumbaka mtoto wa miaka minne baada ya kukutana naye shambani wakati mtuhumiwa akiwa na shughuli za kilimo.
Mwendesha mashtaka huyo aliiambia mahakama hiyo kuwa, katika tukio hilo mtoto huyo alipita shambani kwa Marko akiwa uchi wa mnyama jambo ambalo kijijini ni kawaida, lakini mshitakiwa alimshika na kumlaza kwenye matuta na kuanza kumbaka.

Hata hivyo mshitakiwa Marko alikiri papo hapo kutenda kosa lake na kumfanya hakimu Swalo, amhukumu kifungo cha maisha kwa kosa hilo.
Akitoa adhabu hizo kwa nyakati tofauti kwa washtakiwa hao wawili, Mihayo na Marko, hakimu Swalo alisema kwa kuwa washitakiwa wametenda makosa ya kubaka watoto chini ya umri wa miaka kumi, kifungo cha miaka 30 na viboko 12 kimejifuta na sasa watatumikia kifungo cha maisha ili liwe funzo kwa vijana wengine.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate