EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, November 10, 2012

Juma Kaseja azira Msimbazi kutokana na matusi aliyotukanwa na mashabiki.

NAHODHA wa mabingwa wa soka Tanzania Bara, Simba, Juma Kaseja, amesusia mazoezi ya timu yao tangu kumalizika kwa mchezo wao na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Kutokana na kutofanya mazoezi na wenzake muda wote huo, Kocha Mkuu, Mserbia Milovan Cirkovic, hatompanga katika mchezo wa leo dhidi ya Toto African kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Kaseja amekuwa akidai kuwa hakuwa vizuri kwa ajili ya kufanya mazoezi na wenzake kutokana na matusi aliyotukanwa na mashabiki baada ya kulala kwa mabao 2-0 siku hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema Kaseja alikataa kufanya mazoezi na hatocheza mchezo wa leo, kutokana na kutofanya mazoezi na wenzake akidai hakuwa vizuri kisaikolojia hadi leo.
Kamwaga alisema pia beki Amir Maftah naye ataukosa mchezo wa leo kutokana na kuwa majeruhi mara baada ya juzi kufanyiwa upasuaji mdogo kuondoa uvimbe uliokuwa unamsumbua kwa siku kadhaa kichwani.

“Maftah anatarajiwa kuondolewa nyuzi zake hii leo na wakati wowote anaweza kujiunga na timu ya taifa, kwani maendeleo yake ni mazuri na yanaridhisha, maana sio majeraha makubwa aliyonayo,” alisema Kamwaga.

Mbali na mechi hiyo, kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya, Prisons itaialika JKT Ruvu, huku Kagera Sugar ikiumana na Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Kaitaba wakati JKT Oljoro itamenyana na Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid na Mgambo Shooting itakuwa na kibarua kigumu kwa Azam FC kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Kamwaga alisema timu yao iko vizuri na imefanya mazoezi ya nguvu tangu ilipotoka Morogoro na wachezaji wako vizuri, ukiwatoa wachezaji hao wawili.
Aliwaomba mashabiki na wanachama wao, kujitokeza kwa wingi leo, kwani yaliyopita yameshapita na sasa waelekeze nguvu katika mechi hiyo, kwani sapoti yao itawafanya wachezaji wacheze kwa kujituma zaidi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate