EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, December 30, 2012

Simba yakiona kwa Tusker..Yacharazwa bakora tatu Uwanja wa Taifa.

MABINGWA wa soka wa Kenya, Tusker FC, jana walizidi kudhihirisha ubabe wao kwa miamba ya soka ya Tanzania, baada ya kuwabonyeza Simba kwa mabao 3-0 kwenye mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Kwa ushindi huo, Tusker ambao ni mabingwa mara 10 wa Ligi Kuu ya Kenya tangu kuanzishwa kwao mwaka 1970, wameweka rekodi ya kuvifunga vigogo vya soka nchini baada ya kuifunga pia Yanga bao 1-0 katika mechi ya kwanza katikati ya wiki.
Shujaa wa mechi ya jana alikuwa Ismail Dunga aliyeifungia timu yake mabao mawili katika kipindi cha kwanza, akifunga la kwanza dakika ya 39, baada ya kuwazidi mbinu mabeki wa Simba kabla ya kumpiga chenga kipa William Mweta na kuujaza mpira katika vyavu.

Bao hilo liliwaamsha wachezaji wa Simba ambao walizidi kulisakama lango la Tusker, lakini safu ya ulinzi ya Wakenya hao ikiongozwa na Joseph Shikokoti aliyewahi kuichezea Yanga, ilikuwa makini kuokoa hatari nyingi kumfikia kipa wao Samwel Odhiambo.
Dakika ya 45, Dunga alirejea katika lango la Simba na kumtungua Mweta kwa mara nyingine baada ya kupokea pasi murua kutoka kwa Maurice Odipo, hivyo wakali hao kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao hayo mawili.


Kipindi cha pili kilianza kwa kila timu kufanya mabadiliko hasa Simba ambayo jana ilichezesha wageni na chipukizi, lakini Tusker walizidi kung’ara baada ya kufunga bao la tatu dakika ya 53, likifungwa kwa kichwa na Frederick Onyango akiitendea haki kona murua iliyokuwa imepigwa na Robert Omunuk.
Katika mechi hiyo, Simba ilifanya mabadiliko ya wachezaji mara saba saba, huku Tusker ikiwabadili sita.
Licha ya kufungwa, Simba walionesha soka maridadi huku ikiwapa picha halisi makocha wa timu hiyo nini wafanye katika kipindi hiki cha maandalizi ya raundi ya pili ya Ligi Kuu Tanzania bara na Ligi ya Mabingwa Afrika.

Mbali ya Simba na Tusker kukabiliwa na michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, pia zitakuwa visiwani Zanzibar kushiriki Kombe la Mapinduzi litakalofikia tamati Januari 12, siku ya kilele cha maadhimisho ya mapinduzi ya mwaka 1964.
Simba: William Mweta, Haruna Shamte, Paul Ngalewa, Hassan Hatibu, Koman bil Keita, Mussa Mudde, Haroun Athuman, Abdallah Seseme, Abdallah Juma, Ramadhan Chombo na Kigi Makasy.
Tusker FC: Samwel Odhiambo, Luke Ochieng, Jeremiah Bright, Mark Odhiambo, Joseph Shikokoti, Khalid Aucho, Edwin Ombasa, Fredrick Onyango, Ismail Dunga, Jesse Were na Robert Omunuk.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate