EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, February 16, 2013

Bunge lasalimu amri taarifa kuhusu tafsiri ya kusitisha matangazo ya shughuli za bungeni

WAKATI Jukwaa la Wahariri Tanzania likiazimia kususia kuripoti mikutano yote ya Bunge kutokana na kukerwa na uamuzi wa kupiga marufuku kurushwa moja kwa moja kwa vikao, Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah ameibuka na kukana kutoa kauli hiyo.

Katika hatua isiyokuwa ya kawaida, jana Jukwaa la Wahariri lilisema kuwa limepokea kwa mshangao mkubwa kauli ya Kashililah ya Jumatano wiki hii, ya kutaka kuzuia kurushwa kwa mikutano ya Bunge, badala yake itaruhusu kurekodi vipindi hivyo na kuvirusha baadaye vikiwa vimehaririwa, na kwamba ofisi yake inawasiliana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kupata njia ya kurusha matangazo hayo.
Mwenyekiti wa jukwaa hilo, Absalom Kibanda aliwaambia waandishi wa habari kuwa: 

“Tunashangaa Bunge la Tanzania limejifunza wapi siasa hizi za kufunika mambo yanayowahusu wananchi, huku likijua kwamba wanaofuatilia vikao hivyo ndio walipa kodi na wapiga kura wa wabunge ambao uongozi wa Bunge unataka kuwalinda.”
Alisema kuwa tamko la Katibu wa Bunge linaenda kinyume na la Haki za Binadamu, Desemba 10, 1948 ambapo Kifungu cha 19 cha tamko hili (kifungu cha 19) kinatoa uhuru wa mtu kutoa na kupokea mawazo bila kujali mipaka ya nchi na haki hii ya kutoa mawazo haipaswi kuingiliwa.

Kibanda alisisitiza kuwa kutokana na kuridhia tamko hilo la kimataifa Bunge lilifanya mabadiliko ya tano ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1984 ambayo kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hii, yaliliingiza tamko hili la Haki za Binadamu hivyo kuwezesha Ibara ya 18 ya katiba hiyo ya 1977 kuakisi kifungu cha 19 cha tamko hiko kwa kutoa uhuru wa mawasiliano na haki ya kupewa taarifa.


Alisema jitihada zozote za kuwafungia wabunge ndani na kuhariri kazi wanazofanya na matamko wanayotoa, ni ishara kwamba Bunge linataka kuficha maovu au udhaifu wa mhimili huo au mihimili mingine inayowajibishwa na wabunge, na kwamba hatua hiyo itakuwa inawachimbia kaburi la kisiasa wabunge kwani ndio wanaomulikwa kwa majibu ya maswali wanayoulizwa na hatua wanazochukua.

“Jukwaa la Wahariri limesisitiza kwamba utaratibu huu unaoandaliwa sasa na Dk. Kashililah ni wa kidikteta na ni mbaya kuliko udikteta wowote uliowahi kutokea hapa nchini kwa miaka yote ya uhuru wa Tanzania. Na kusema kuwa harakati hizi za uongozi wa sasa wa Bunge zinaonekana kama hatua za kufuta yaliyofanywa na uongozi wa Bunge la tisa.

“Jukwaa limetahadharisha kuwa katika mazingira haya, linaamini kwamba iwapo hili litatokea, jitihada ndogo za uwazi zilizokuwa zimefanywa na Serikali ya Rais Jakaya Kikwete, zitafutika na kumfanya aonekane mbele ya jumuiya ya kimataifa kuwa kiongozi dhalimu na dikteta asiyevumilia kukosolewa, na itaifanya serikali na Bunge visiaminike kwa umma na itasababisha zogo na vurugu zisizomithilika kwani waliojifungia ndani watatoka na kusema hadharani kwa jinsi watakavyoona inafaa hivyo kuharibu kabisa mfumo wa taarifa za chombo hicho,” alisema Kibanda.

Bunge lakana
Wakati Jukwaa la Wahariri likitoa mashambulizi hayo mazito, Dk. Kashililah amekana kutoa matamshi hayo akidai kunukuliwa vibaya na vyombo vya habari.
Katika taarifa yake ya jana kwa vyombo vya habari, ofisi ya Bunge imesema imepokea kwa masikitiko taarifa kuhusu tafsiri ya kusitisha matangazo ya shughuli za bungeni na kamati, kinyume na jinsi ilivyoakisiwa katika mazungumzo ya pamoja kati ya wanahabari na katibu wa ofisi hiyo Dk. Kashililah.

Katika taarifa hiyo jana, Dk. Kashililah pamoja na kuomba radhi kwa wananchi kwa taarifa hizo, alisema Bunge halina mpango wa kusitisha matangazo yake wala kamati zake, ambazo kwa mahitaji ya sasa nazo zinapaswa kurushwa moja kwa moja kama sehemu ya mpango kabambe wa kuwapasha wananchi yanayojiri katika uendeshaji bora wa shughuli zake.

“Dhamira ya Bunge ni kuhakikisha kuwa mpango kabambe uliopo ni kumfikia kila Mtanzania alipo na kwa uwezo alionao aweze kupata na kushiriki katika uendeshaji wa shughuli za Bunge… hivyo mpango mkakati uliopo utakuwa kuboresha mawasiliano ya kawaida kupitia teknolojia ya mawasiliano,” ilisema taarifa ya Bunge.
Aidha, taarifa hiyo ilisema kwamba kwa wale watakaokuwa na uwezo wa kupata huduma za mtandao, wataweza kuona picha za video kupitia tovuti ya Bunge.
Ilisema kwa wale watakaokuwa na uwezo wa kushika mawimbi ya redio, wataweza kufuatilia majadiliano katika redio ya Bunge inayotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni katika masafa yanayopatikana nchi nzima kama redio zingine zinazotoa huduma hiyo hapa nchini.

“Hivyo utaratibu uliopo sasa utaendelea kutumika ambapo vituo vyote vya televisheni vitapewa fursa ya kurusha matangazo kwa utashi wao bila kuwekewa mipaka ya aina yoyote sambamba na matangazo yatakayotolewa na mitandao ya Bunge,” ilisema.

Kwamba utaratibu huo unatokana na uamuzi wa pamoja kati ya Bunge na Tume ya Mawasiliano Nchini (TCRA) kwamba vipindi vyote vya Bunge vitakuwa vinarushwa bila kudhaminiwa na taasisi yoyote zaidi ya hiyo.

“Hivyo basi kwa maelezo hayo ni dhahiri kuwa Bunge halina mpango wa kusitisha matangazo ya TV wala yale ya redio au teknohama bali linatarajia kuboresha upatikanaji wa huduma kwa utaratibu ulio rahisi na unaoweza kusimamiwa na pande zote, yaani Bunge na wananchi,” ilisema taarifa hiyo.
Kashililah alisema televisheni zote zinazorusha matangazo ya Bunge hupata toka katika mitambo yake na pale wanapoona yafaa basi huomba kutumia mitambo yao na hivyo kutumia fursa hiyo kuingiza kamera na wanahabari ndani ya kumbi za Bunge.

“Kuzingatia mabadiliko tajwa, utaratibu huo umepewa ukomo ila sasa hapatakuwa na fursa ya kuingiza kamera ndani ya kumbi za Bunge, bali wote watakaotaka kurusha matangazo ya Bunge kwa utashi wao, watapata clear feed toka katika mitambo yake hivyo kurusha live vipindi vyote vya Bunge bila kuhaririwa kama ilivyonakiliwa katika makala mbalimbali.
“Hata hivyo utaratibu huu wa kutumia camera katika kumbi utaendelea katika kamati za Bunge, hadi hapo mitambo mipya ya mawasiliano itakapofungwa katika kumbi zote za kamati.

“Hivyo basi, ili kwenda sawia na taratibu hizo, Bunge litaendesha zoezi la kuwatathmini waandishi wote wa habari za Bunge na kuwasajili kwa vigezo vitakavyoafikiwa kati ya Baraza la Habari, hivyo basi, wakati zoezi la maboresho hayo likiendelea, wananchi watajulishwa kila hatua na matarajio tajwa,” ilisema taarifa hiyo ya Bunge.
Tangu kutolewa kwa tamko hilo la vikao vya Bunge kutorushwa ‘live’, makundi mbalimbali na wanasiasa walilaani wakisema kuwa limelenga kuisaidia serikali kutoumbuka. Walisema takriban mwaka sasa, serikali imekuwa ikivuliwa nguo hadharani na wabunge hususan wa kambi ya upinzani, na pia kushuhudia jinsi kupitia kiti cha spika jinsi wapinzani walivyokuwa wakidhibitiwa kwa uonevu mkubwa.

CHANZO TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate