EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, February 9, 2013

MwanaHALISI lashinda kesi

KESI ya kukashifu, iliyokuwa ikilikabili gazeti la MwanaHALISI, imetupiliwa mbali na mdai ametakiwa kulipa gharama zote za kesi.

Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam, Warialwande Lema, katika hukumu yake Jumatano, alisema ili maneno yawe, au yaonekane kuwa ya kashfa, sharti yawe ama si ya kweli au yawe ya uongo.
Alisema kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa mahakama haikuona chochote kile kilichothibitisha madai ya kashfa.

Juma Jaffari Nyaigesha, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Msewe, jijini Dar es Salaam ndiye alilishtaki gazeti akidai kuwa kwa habari na makala zilizochapishwa katika matoleo yake matano, alikashifiwa na kuvunjiwa heshima mbele ya jamii.
Mdai alimshtaki mhariri wa gazeti, Jabir Idrisa, mshauri wa gazeti, Ndimara Tegambwage, Stella Kajuna – mkazi wa Msewe, mhariri mkuu, kampuni inayochapisha gazeti, Hali Halisi Publishers Limited, kampuni ya uchapaji ya Printech na kampuni nyingine ya uchapaji, Tanzania Standard Printers Limited.
Nyaigesha alidai kuwa matoleo matano ya MwanaHALISI yalikuwa na taarifa zilizomkashifu na kumwondolea hadhi mbele ya jamii.

Aliyataja matoleo hayo kuwa yale ya 10, 12, 24, 31 Oktoba 2007 na 14 Oktoba 2008.
Katika matoleo hayo kulikuwa na habari na makala juu ya madai ya kuwepo vitendo vya uhalifu Msewe, ukosefu wa amani na matumizi mabaya ya madaraka ambavyo Nyaigesha alidai vilikuwa vinaelekezwa kwake.

Katika hukumu yake, hakimu Lema alisema kwanza mdai hakuleta hata shahidi mmoja kuthibitisha madai yake na kwamba yeye mwenyewe hakuweza kuthibitisha kuwa amekashifiwa.
Hata takwimu za kura za uchaguzi alizopeleka mahakamani, zilionyesha kuwa hata baada ya kuandika yaliyokuwa yakitokea Msewe, katika uchaguzi uliofuata alipata kura nyingi, jambo ambalo lilikinzana na madai ya kukashfiwa.

Hakimu alisema Jaffari ni kiongozi na kile walichofanya waandishi kilikuwa ni mjalizo halali na wa haki juu ya kiongozi na uongozi wa umma na siyo kashfa.
Alisema ameridhika na ushahidi uliotolewa na walalamikiwa, ushahidi wa maandishi kutoka kwenye kata na hata kauli ya mdai kuwa mmoja wa walalamikiwa alipigwa na kwamba yote hayo yalidhihirisha umuhimu wa kilichoandikwa.
MwanaHALISI ilikuwa ikitetewa na wakili maarufu, Mabere Marando, wakati Tanzania Standard Printers Ltd, iliwakilishwa na wakili Audax Kahendaguza Vedasto wote wa Dar es Salaam.

Kuhusu wachapaji wa gazeti, hakimu alisema hawakuwa na hatia kwa kuwa hawakutenda kashfa yoyote, kwa vile hakuna kashfa iliyothibitishwa.
Aidha hakimu alikubaliana na hoja kwamba mchapaji anayefanya kazi aliyopewa na kuirejesha kwa mhusika, hawezi kuwa ametenda kashfa.
Alipoulizwa Mkurugenzi Mtendaji wa HaliHalisi Publishers, Saeed Kubenea, juu ya hatua anayojiandaa kuchukua, alisema hajakaa na wakili wake kupanga hatua inayofuata.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate