EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, February 16, 2013

Wananchi wateketeza nyumba kwa imani za kishirikina


Tukio la kuteketezwa kwa nyumba hizo lilitokea jana saa 9:00 mchana na kusababisha mali zote zilizokuwa ndani ya nyumba hizo, ikiwamo mifugo kuteketea kwa moto.

FAMILIA nne katika Kijiji cha Ihahi, Wilaya ya Mbarali hazina mahali pa kuishi baada ya nyumba zao kuteketezwa kwa moto na wananchi wenye hasira baada ya kuwatuhumu kufanya mauaji ya kishirikina.
Watu waliochomewa nyumba zao walitambulika kwa majina ya Mohamed Mangea (48) ambapo pamoja na mkewe, Pili Hamisi wanahisiwa na ushirikina huo, Ramadhani Mhongole na wengine waliotambuliwa kwa jina moja moja la Mzee Mwampishi na Sekilulumo.

Baadhi ya wananchi waliozungumza na gazeti hili wamedai kuwa wamefikia hatua ya kuteketeza makazi ya watu hao baada ya Serikali ya wilaya hiyo kupuuza madai yao dhidi ya watu hao walipotoa taarifa za mauaji.

Mwenyekiti wa kijiji hicho, Ramadhan Hassan alisema tuhuma za kuwapo kwa mauaji ya kishirikina yaliyofanywa na watu waliochomewa nyumba zao yamekuwapo kwa muda mrefu sasa, lakini Serikali ngazi ya wilaya haikuzifanyia kazi ipasavyo. Alisema taarifa za awali zilipofika Serikali, mapema mwezi uliopita, Serikali ilimtuma afisa wa upelelezi kutoka kituo cha Polisi Chimala kwa ajili yan kushughulikia suala hilo.

Alisema mpelelezi huyo aliendesha kura za siri kwa ajili ya kuwabaini watu wanaojihusisha na ushirikina kijijini hapo,ambapo wananchi walipiga kura bila matatizo.
Alisema matokeo ya kura hiyo yalionyesha watuhumiwa waliochomewa nyumba kuwa ndio vinara wa ushirikina na Polisi iliwakamata na kuwapeleka kituoni.
Alisema hata hivyo watuhumiwa hao walirejea uraiani baada ya muda mfupi,hali iliyosababisha wananchi waliokuwa na hofu ya maisha yao, kupandwa na ghadhabu na kuamua kuteketeza nyumba zao kama njia ya kuwaondoa katika kijiji chao.

Kwa upande wake,Ramle Ibrahim ambaye ni mtoto wa mmoja wa waathirika wa tukio la kuchomewa nyumba alisema kabla ya kuchoma nyumba ya wazazi wake, kundi la vijana walikwenda nyumbani kwao wakiwa wamebeba mapanga na kuanza kuwapiga wazazi wake na kuwataka waondoke kijijini hapo na wakati wa tukio hilo wazazi wake pamoja na wenzake walilazimika kukimbilia kituo cha polisi kwa ajili ya kunusuru maisha yao.

Hata hivyo, taarifa zilizolifikia gazeti hili jana jioni, Polisi walikwenda kijijini hapo na kukamata watu wawili, tukio ambalo lilisababisha wananchi kuandamana kwenda kituo cha Polisi cha Chimala ili kushinikiza wenzao kuachiwa huru. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya,Diwani Athuman alipoulizwa kuhusiana na tukio hili alidai kuwa yupo Dodoma kwa shughuli za kikazi na kumtaka mwandishi wa habari hii kuwasiliana na Kaimu wake Barakael Msaki.    

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate