EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, March 28, 2013

Kikwete asimulia alivyoiba wali JKT


Rais Jakaya Kikwete
RAIS Jakaya Kikwete amesimulia maisha yake ya jeshini, huku akikumbuka namna alivyokamatwa na mkuu wa jiko (afande ubwabwa) akiiba wali. Rais Kikwete alitoa ushuhuda huo wakati akifunga mafunzo maalumu ya uongozi kwa wabunge na kuzindua mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria.

Hafla hiyo ilifanyika juzi katika Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kikosi cha 832 KJ, kilichopo Ruvu, Kibaha mkoani Pwani, ambapo viongozi mbalimbali walihudhuria.

Rais Kikwete aliwakumbusha vijana hao kwamba yeye ni miongoni mwa watu waliochukua mafunzo ya JKT kambini hapo akiwa katika Operesheni Tumaini mwaka 1972.

Rais Kikwete alisema katika mafunzo hayo alijengwa vizuri, ingawa hadi leo bado anakumbuka matukio mawili ya kufurahisha na kusikitisha akiwa kambini hapo.

Alisema tukio la kwanza ambalo hawezi kusahau ni pale alipokamatwa akiiba wali na tukio jingine ni kuhusu kifo cha askari mwenzao aliyefariki dunia baada ya kukanyagwa na trekta.

“Nawashukuru kwa kunialika katika shughuli hii, nimetembelea na kujionea miradi mbalimbali inayoendelea kufanywa hapa kambini.

“Wakati tukiwa kule nilikuwa naangalia kwa makini, hasa nilikuwa naangalia lile bweni letu, sisi tuliokuwa Kombania A mwaka ule, nimepakumbuka ingawa sasa pamekarabatiwa vizuri.

“Yapo matukio mawili ninayoyakumbuka siwezi kuyasahu hadi leo wakati nikiwa hapa kambini…(kicheko) jeshi si mchezo, nawaeleza haya mjue maisha ya jeshi hayana mzaha.

“Nakumbuka namna nilivyokamatwa na bwana ubwabwa nikiiba wali kule katika bwalo la chakula,” alisema Rais Kikwete huku wananchi na askari wanafunzi (kuruta) waliokuwapo wakiangua kicheko.

Rais Kikwete aliendelea kusema. “Katika kombania yetu tulikuwa na mchezo siku zikipikwa nyama na wali tunaiba tunakwenda kuficha kisha baadaye tunakuja kula baada ya kazi.

“Sasa siku hiyo ilikuwa zamu yangu kuiba wali, kama kawaida nikachukua mestini zangu mbili nikachukua wali ili nikafiche, natoka tu nje, hamad! afande ubwabwa huyu hapa mlangoni (kicheko).

“Akaniambia piga magoti, huku nimeshikilia mestini zangu za wali. Akaniambia hivi! Brother maana alikuwa anapenda sana kuita brother, wewe ni form six (kidato cha sita) umekuja kuchukua mafunzo.

“Huko juu kuna makamu wa rais anaitwa Rashid Mfaume Kawawa, akisikia kwamba kuna kijana wa form six ameiba wali kambini atafurahi?

“Nikamwambia hapana, akasema kama hivyo ndivyo acha tabia hiyo, akanikanya nisiendelee na tabia ile. Nilikamatwa lakini nilifanikiwa kuondoka kwa huruma.

“Tukio la pili ninalokumbuka ilikuwa ni masuala ya kufundisha, tulikuwa tunakwenda Misugusugu kulikuwa na umwagiliaji katika skimu ya mpunga.

“Sasa tukiwa tunajiandaa zilifika habari kambini kwamba kuna askari mwenzetu amekanyagwa na trekta amefariki dunia, tukiwa bwenini nikapaza sauti ‘Stanley kuna habari gani, nasikia askari amekanyagwa na trekta’.

“Wakati napiga kelele, sikujua kumbe huyo ninayemwita ndiye aliyepatwa na janga hilo, tulienda kule barabarani kujua mazingira ya kifo yalikuwaje.

“Tulipofika pale tuliambiwa kwamba mwenzetu alikuwa amepanda trekta na alikaa kwenye madi gadi huku akila muwa, kwa bahati mbaya aliteleza akaanguka na kukanyagwa na tairi kubwa,” alisema Rais Kikwete huku watu wakisikitika.

Rais Kikwete pia alitumia fursa hiyo kuwaeleza vijana hao chimbuko la kuanzishwa kwa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), ambapo vijana wanaomaliza kidato cha sita watajiunga na jeshi hilo kwa mujibu wa sheria kabla ya kujiunga na vyuo.

Rais Kikwete alisema JKT ilianzishwa mwaka 1963 na kwamba msingi wake mkuu ni kutoa fursa kwa vijana kujifunza na kujenga umoja wa taifa.

Akielezea historia ya jeshi hilo, Rais Kikwete alipinga madai ya baadhi ya watu ambao wamekuwa wakidai kuwa wananchi walisomeshwa bure chini ya utawala wa awamu ya kwanza.

“Wazo la kuanzisha JKT lilianzia TANU Youth League, 10/07/1963 wazo lilitolewa na aliyekuwa katibu wake, Joseph Nyerere wakati huo, ndiye aliyependekeza JKT ianzishwe.

“Aprili 19, 1963 Baraza la Mawaziri liliridhia uanzishwaji wake. Sheria namba 64 ya mwaka 1966 ilitungwa na hapo JKT ilianza kupokea vijana wasomi wa elimu ya juu.

“Enzi zetu mafunzo ya JKT yalikuwa miezi 5 kambini, halafu miezi 18 kazini, baadaye unarudi kumalizia mwezi mmoja.

“Ilikuwa huwezi kuanza kazi bila kupitia JKT. Katika miezi yako 18 ya kazi, hapakuwa na ruhusa ya kuchukua mshahara wote.

“Unachukua asilimia 40 ya mshahara wako, asilimia 60 inayobaki Serikali inachukua kufidia gharama zake za mafunzo ya JKT, suala la kwamba watu walisoma bure katika nchi hii mimi silioni.

“Tumedhamiria kuboresha na kuongeza uwezo wa JKT ili iweze kutimiza wajibu wake. Jeshi hili lina wajibu mkubwa katika kuwajenga vijana na suala zima la uzalishaji mali,” alisema.

Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na Kaimu Mkuu wa Kambi hiyo, Luteni Kanali Menas Mbele na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza.

Katika hatua nyingine, wabunge 25 wameshindwa kujiunga na mafunzo ya JKT yaliyofanyika katika kambi mbalimbali nchini, licha ya kujiandikisha.

Kwa mujibu wa Rais Kikwete, wabunge 47 walijiandikisha, lakini wabunge walioripoti kambini ni 24 na waliohitimu mafunzo hayo ya wiki tatu ni 22 tu.

Wabunge waliohitimu mafunzo maalumu ya uongozi katika Kambi ya 832 KJ, Ruvu ni pamoja na Mbunge wa Mchinga, Said Mtanda, Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, Murtaza Mangungu na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate