EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, March 6, 2013

TFF wamkataa Waziri Makalla.. Wasema ameonyesha wazi kuwa na upande

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limewasilisha rasmi ombi la kukutana na serikali kuhusu msigano uliopo baina ya pande hizo mbili, lakini wakitoa sharti kuwa hawako tayari kuketi na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla.

Akizungumza kwa kujiamini, Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo, Angetile Osiah, alisema jana kwamba hawataki kujadili suala hilo na Makalla kwa sababu ameonekana wazi kuwa na upande kupitia kauli zake mbalimbali.
 
Alisema kabla na baada ya serikali kutangaza kuifuta katiba mpya ya TFF ya mwaka 2012 na kuitambua ya mwaka 2006, Makalla amekuwa akitoa kauli zinazoashiria wazi kuwa upande mmoja wa wagombea walioenguliwa na Kamati ya Rufaa.
Osiah alisema kwa mazingira hayo, wao TFF hawataketi na Makalla kujadili jambo hilo kwa maslahi ya soka nchini kwa sababu kupitia vyombo vya habari hasa radio, amekuwa akilishutumu shirikisho hilo tangu Kamati ya Rufaa iwaengue baadhi ya wagombea.

“Hata kama waziri asipokuwepo, hatuko tayari kufanya mazungumzo yoyote na naibu wake, tunasema hivyo kwa sababu tayari Makalla (Amos), ameonyesha yeye ni mdau wa upande fulani, hatuna imani naye,” alisema Osiah na kuongeza:

“Kwanza alianza kuongelea ishu hii mara baada ya Kamati ya Rufaa kuwaengua baadhi ya wagombea, yeye akiwa nyumbani kwake akatoa tamko, halafu pili akiwa Morogoro mjini, aliitisha mkutano na waandishi wa habari juu ya msimamo wake kuhusu mchakato wa uchaguzi na mabadiliko ya katiba,” alisisitiza Osiah.
Osiah alisema Makalla kama kiongozi mwenye dhamana ya michezo, hakupaswa kuonyesha kuwa upande gani kabla ya kutoa nafasi na kusikiliza pande zote mbili kwa maana ya walalamikaji na walalamikiwa.
Aliongeza kuwa njia pekee ya kutatua mgogoro uliopo ni wao TFF kuonana na Mukangara na sio Makalla ambaye anaonekana wazi ni sehemu ya tatizo akiwa upande wa mdau aliyeenguliwa.

Hata baada ya Rais wa TFF, Leodegar Chilla Tenga, kutoa msimamo kuwa uamuzi wa serikali wa kuibatilisha katiba ya 2012 na kuitambua ya mwaka 2006, hautekelezeki, hivyo wanataka kukutana na waziri, Makalla alisema milango iko wazi, lakini TFF ijue uamuzi wa awali wa serikali hautabadilika.

Kuhusu ombi la kutaka kuonana na serikali, Osiah alisema waliliwasilisha wizarani tangu Machi 4, ikipendekeza kikao hicho kifanyike Machi 7 au 13 kwani viongozi wa juu wa shirikisho hilo watakuwa kwenye mkutano nchini Morocco.
Uamuzi wa TFF kukutana na serikali ulifikiwa na Kamati ya Utendaji ya Shirikisho hilo iliyoketi Machi 2, kujadili tamko ya Waziri Mukangara kutengua matumizi ya katiba hiyo mpya kwa hoja kwamba ilipitishwa kinyume cha sheria ya michezo ya mwaka 1967 na marekebisho yake 1971.

Tanzania Daima ilipomtafuta Makalla jana jioni kwa njia ya simu kuhusu sharti la TFF, alisema TFF hawana ujanja kwa hilo kwani yeye ndiye watakutana naye kutokana na kitengo cha michezo kuwa chini yake.
Makalla alisema kwa siku zilizopendekezwa, Mukangara atakuwa safarini nje ya nchi kwa siku 10 na kusema anashindwa kuelewa msimamo wa shirikisho hilo kwani awali walitaka kukutana na waziri, sasa wanatoa sharti juu ya nani wakutane naye.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate