EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, March 31, 2013

Mahakama ya Juu ya Kenya imemthibitisha Uhuru Kenyetta kuwa Rais halali Kenya.

Nairobi.
Mahakama ya Juu ya Kenya imemthibitisha Uhuru Kenyetta kuwa Rais halali mteule wa nchi hiyo pamoja na mgombea mwenza wake, William Ruto.
Mahakama hiyo iliwathibitisha Kenyatta na Ruto jana katika uamuzi wa kesi ya kupinga matokeo uliowapa ushindi katika uchaguzi mkuu uliofanyika Machi 4, 2013, iliyofunguliwa na mpinzani wao mkuu katika kinyang’anyiro hicho, Waziri Mkuu, Raila Odinga.

Odinga katika kesi hiyo aliituhumu Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya nchi hiyo kuwa ilihujumu matokeo ya uchaguzi ili kumpa ushindi, Kenyatta.Hata hivyo, katika uamuzi wake jana Mahakama hiyo ilisema kwamba Kenyatta na Ruto walichaguliwa kihalali katika uchaguzi huo mkuu.

Vilevile, Jaji Mkuu wa Mahakama hiyo, Dk Willy Mutunga alisema kwamba uchaguzi ulikuwa wa haki na huru, kwa sababu katiba na sheria zilifuatwa, hivyo Mahakama imempitisha Rais huyo Mteule kuwa Rais wa Kenya.

Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kutolewa hukumu hiyo, Odinga alisema kwamba amekubaliana na uamuzi wa Mahakama kama alivyoahidi.
‘’Naitakia kila la kheri Serikali ya Uhuru Kenyatta, kwani hakuna ushindani usiokuwa na mshindi,’’alisema .

Aliwaasa Wakenya wakae kwa amani na kuheshimu Serikali mpya inayokuja baada ya kumalizika kwa kesi za uchaguzi katika Mahakama ya juu.
 

“Nilisema kwamba nitakubali uamuzi wa Mahakama ya juu kwani ikiwa sikajubaliana na uamuzi huo nitakuwa nimevunja sheria,’’alisema Odinga.Ukiachilia mbali kesi iliyofunguliwa na Odinga kupinga Kenyatta kutangazwa mshindi wa uchaguzi huo wa tano tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini Kenya, kuna kesi nyingine ambayo ilifunguliwa na Muungano wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali, `The African Centre for Open Governance’ (Africog). Katika kesi hiyo, Africog ilihoji uhalali wa uchaguzi huo.

Kesi ya tatu ilifunguliwa na wajumbe wa timu ya kampeni ya Kenyatta, Wanaharakati kutoka katika mitandao ya kijamii, Dennis Itumbi na Moses Kuria wanaopinga uamuzi wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya kujumuisha kura zilizoharibika wakati wa kujumlisha kura za wagombea urais.

Katika uamuzi wake, Mahakama iliamua kwamba kesi zote tatu zitaunganishwa kuwa moja mbali na ile iliyowasilishwa na Odinga .

Ombi la mashirika latupwa
Awali Mahakama ya Juu ilitupilia mbali ombi la muungano wa mashirika yasiyo ya kiserikali lililoitaka Mahakama hiyo iiamuru Tume ya Uchaguzi kufikisha mahakamani hapo nyaraka zote zilizotumika wakati wa uchaguzi huo.
Kadhalika Mahakama hiyo ilitupilia mbali hati ya kiapo yenye kurasa 839 iliyowasilishwa na Cord ikidai kuwa kura katika majimbo 120 zilikuwa haziwiani na idadi ya wapiga kura hivyo kuitaka Mahakama hiyo iitishe uchunguzi wa kina wa daftari la wapigakura ukioanishwa na kura zilizopigwa.

Maandamano
Juzi Jeshi la Polisi nchini Kenya lilifanikiwa kuzuia maandamano yaliyopangwa kufanyika nje ya Mahakama ya Juu mjini Nairobi wakati kesi hiyo ikiendelea.Waandamanaji hao walidaiwa kuwa ni kambi ya Waziri Mkuu, Odinga walikuwa wakipinga mwenendo wa kesi hiyo ulivyokuwa ukiendelea mahakamani hapo.

Hata hivyo Odinga alisema licha ya Mahakama hiyo kuacha kutendea haki baadhi ya vipengele vya kesi hiyo amekubali uamuzi huo.
Kutokana na ushindi huo, Kenyatta kutoka Muungano wa Jubilee sasa anafahamika kuwa ndiye Rais Mteule halali wa Kenya atakayeapishwa Aprili 9 mwaka huu.

Kesi hiyo ilifunguliwa na Raila Odinga wa Muungano wa Cord baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu uliofanyika mapema mwezi huu.
Katika uchaguzi huo matokeo yalionyesha kuwa Uhuru alishinda kwa asilimia 50.07 huku Raila akipata asilimia 43.28 ya kura.

Uchaguzi huo ni wa kwanza tangu kufanyika uchaguzi uliokumbwa na ghasia mwaka 2007 na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 1,000.
Kenyatta na mgombea mwenza wake, Ruto, wanakabiliwa na kesi katika Mahakama ya Kimataifa Makosa ya Jinai wakituhumiwa kwa kuchochea vurugu zilizotokea mwaka 2007.

Kura kuhesabiwa tena
Machi 25, Mahakama ya Juu ya Kenya iliagiza kuchunguzwa kwa fomu 34 za matokeo ya uchaguzi wa rais kutoka katika vituo vyote 34,400, vya kupigia kura vilivyotumika katika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo uliofanyika Machi 4, mwaka huu.

Kadhalika Mahakama hiyo iliagiza kuhesabiwa upya kwa kura za urais katika vituo 22 kati ya 33,000 vilivyolalamikiwa na aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Cord, Odinga.
Odinga alidai kuwa vituo hivyo 22 kura zilizopigwa zinazidi idadi ya wapiga kura walioandikishwa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate