Wakati mashabiki wa Simba wakitaka kuitishwa kwa Mkutano Mkuu wa
klabu hiyo mara moja, Mwenyekiti wao Aden Rage amesema anakwenda kwanza
India kwa ajili ya matibabu hivyo, wanachama wametakiwa kuvuta subira.

Rage aliiambia Mwananchi kuwa, kwa sasa akili yake
ameielekeza kwenye matibabu nje ya nchi, hivyo uongozi hauwezi kuitisha
mkutano kwa sasa mpaka atakaporejea kutoka India.
"Nitawaeleza mwenyewe wanachama wangu na siyo vyombo vya habari. Muhimu kwanza ni afya, mambo mengine yatafuata. Wakati wowote kuanzia sasa nakwenda India, natumaini watanivumilia," alisema Rage.
Rage pia alipinga wachezaji wa timu yao kulaumiwa kutokana na matokeo mabaya wanayopata kwenye mechi za ligi na badala yake amewataka wanachama kuwatia nguvu kwani bado wana mechi za ligi.
No comments:
Post a Comment