EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, April 5, 2013

CHADEMA yafichua ufisadi wa Mwakyembe.

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemtuhumu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe kuwa amefanya yale aliyoyakataa kwenye Kampuni ya Richmond, licha ya wakati huo kujidai anajua kufuata taratibu.

CHADEMA imefichua kuwa Dk. Mwakyembe amekiuka sheria ya manunuzi ya umma katika mradi wa upanuzi wa bandari kavu unaofanyika katika eneo la Sukita, Tabata jijini Dar es Salaam.

Siri hiyo ilifichuliwa na Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Mafunzo wa CHADEMA, Benson Kigaila alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kabla ya kuanza kwa vikao vya Kamati Kuu ya chama hicho.

Kigaila alidai kuwa Dk. Mwakyembe ni mnafiki, kwani yale aliyoyakataa wakati akiwa Mwenyekiti wa Kamati teule ya Richmond ambapo ripoti yake ilisababisha Waziri Mkuu wa wakati huo, Edward Lowassa ajiuzulu, leo ameyafanya.

“Alilaumu kuwa Richmond ilipewa zabuni bila kuwa na vigezo, bila kufanyiwa upembuzi yakinifu, tena bila zabuni husika kutangazwa.
Hili ni eneo la SUKITA linamilikiwa na CCM na lipo maeneo ya barabara ya Kawawa na Mandela,” alisema.

Alisema mradi huu utatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Kampuni ya CCM inayoitwa Jitegemee Trading Company na TPA kwa gharama ya mabilioni ya shilingi.
Kigaila alidai kuwa katika mwaka ujao wa fedha 2013/2014 Mamlaka ya Bandari (TPA) itailipa CCM sh bilioni 10 na kwamba tayari fedha hizo zimetengwa katika bajeti ya serikali.
Kampuni ya SUKITA ilisajiliwa Machi 15, 1978 na Jitegemee Trading Company Limited ilisajiliwa mwaka 1997.
 
Wakurugenzi wa Jitegemee ni Sam Mapande, Peter Machunde na Diwani wa CCM Kata ya Hananasif, wilayani Kinondoni, Abbas Tarimba. Mapande, ndiye mwanasheria aliyehakiki fomu za Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.
“Kwanza mradi huu unaotaka kufanywa na Mwakyembe kwa kutumia kivuli cha TPA haukufanyiwa tathimini, upembuzi yakinifu kiuchumi sawa sawa na ilivyokuwa kwa kampuni ya kitapeli ya Richmond,” alisema Kigaila.

Aliongeza kuwa mradi huu haukufanyiwa uchanganuzi wa kiuchumi ili kubaini pamoja na kulipa sh bilioni 10 ya plot kabla ya kujengwa kwa mradi.
“Mradi huu wa Mwakyembe na chama chake haukufuata sheria ya manunuzi ya umma (PPRA). Hakukuwa na zabuni iliyotangazwa wala ushindani kwa makampuni na mashirika mengine yenye sifa,” alisisitiza.

Kigaila aliongeza kuwa nyaraka zilizopo TPA zinaonyesha kuwa tangu mwaka 2010, Bodi ya Bandari ilipokea maombi kutoka Manispaa ya Temeke ya kutaka kufanya ubia wa eneo la maegesho, ambapo walitenga eneo huko Kurasini, karibu kabisa na bandari.
Alisema kuwa wazo hilo halijafanyiwa kazi, badala yake Mwakyembe amekuja na mradi wake.

Kigaila alisema vyanzo vyao ndani ya serikali na CCM vinasema mjumbe mmoja wa Bodi ya TPA alihoji kwanini shirika linaingiza fedha hizo kwenye mradi huu katika eneo la SUKITA, lakini mkurugenzi wa bandari alijibu: “Huu ni mradi wa chama tawala, hivyo ni muhimu tukau-sapport”.

Alihoji kama Mwakyembe, serikali na CCM hawaoni umuhimu wa kutumia fedha hizo kuimarisha bandari zilizopo kwenye maeneo ya maziwa kama vile Kigoma, Mwanza, Rukwa na Musoma ikiwa ni kujiweka sawa kwenye ukanda wa biashara na ukuaji wa soko la Afrika Mashariki.

Alisema kuwa siku zote CCM na serikali yake wamekuwa wakijifanya kuwaonea huruma Watanzania na kuwataka wahame mabondeni, lakini hao hao wanatumia mabilioni ya shilingi na kuyaingiza katika bonde la Msimbazi, ambako kuna hatari kubwa ya mvua kusomba magari na makontena ya wateja wa TPA.

“Lakini ukiangalia hii ripoti, utaona kuwa kuna miradi mikubwa 35 ambayo imeombewa fedha si kwa sababu ya kuiendeleza, bali ni kukusanya fedha za kutafuta urais,” alidai.
Kigaila aliongeza kuwa Mwakyembe amekataa mapendekezo yaliyokuwa yamefanywa na uongozi wa bandari kushirikiana na Manispaa ya Temeke kupanua bandari eneo la Kurasini, badala yake ameelekeza upanuzi huo ufanyike katika eneo la SUKITA.
“Kampuni ni ya CCM, kiwanja ni cha CCM, zabuni haikutangazwa wala kufanya upembuzi yakinifu kwa kampuni hii kama imekidhi vigezo. Mwakyembe atuambie ilishindanishwa na kampuni zipi na ilishinda kwa vigezo vipi. Iweje yale aliyoyakataa kwenye Richmond ameyatenda?” alihoji.

Kigaila amelaani tabia ya viongozi wa CCM kuanzisha miradi au kampuni hewa wakati wa kuelekea uchaguzi mkuu kwani ni kwa njia hii huchota fedha kwa ajili ya kufanikisha uchaguzi kama ilivyofanyika kwa EPA.
“Mwakyembe yupo kwenye kambi ya Samuel Sitta, wanaungana na familia ya Jakaya Kikwete kumsaidia Bernard Membe katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu ujao, hivyo wameamua kuanzisha miradi hii kwa njia za kifisadi,” alisema.
Juhudi za Tanzania Daima kuzungumza na Mwakyembe au Naibu wake, CharlesTizeba na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nauye ziligonga mwamba baada ya wote kutotoa ushirikiano.

Waziri Mwakyembe simu yake iliita bila kupokelewa na hata alipoandikiwa ujumbe mfupi (sms) hakupatikana tena hewani wakati naibu wake, alisema: “Wewe gazeti lenu liliandika nilifukuzwa Mtwara, na sasa unataka kunigonganisha na propaganda za CHADEMA ili upate habari ya kuandika, sitaki gazeti lako na sikutaki wewe.”
Naye Nape alisema: “Andikeni mnavyoandika mimi nitajibu kesho kwa kuwa najua nikijibu sasa mtayaweka ndani kwa udogo.”
Alipoulizwa kwanini asitumie hiyo nafasi kujibu, alimwambia mwandishi: “Kama hutaki kusikia yangu, basi andika ya kwako, mimi nimesema nitajibu kesho.”
Via Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate