EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, April 5, 2013

Msuguano mkali Kamati za Bunge

Dar es Salaam. 
Wabunge wameendelea kusuguana na Serikali katika vikao vya Kamati za Bunge vinavyojadili mapendekezo ya bajeti za wizara mbalimbali, hali inayoashiria kwamba huenda kukawa na msuguano zaidi katika Bunge la Bajeti ya 2013/14 linalotarajiwa kuanza tarehe 9 mwezi huu.

Misuguano ambayo ilijitokeza jana ni baina ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) ambayo ilimgomea Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa kupunguza Bajeti ya Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).


Kwa upande wake, Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ilikataa kupitisha mapendekezo ya Bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) ya Sh42.7 bilioni kwa maelezo kwamba fedha hizo ni kidogo sana.

Wakati hayo yakitokea, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa aliiwekea ngumu Kamati ya Miundombinu, ambayo ilikuwa ikitaka kuongezwa muda wa matumizi mfumo wa analojia hadi 2015, badala ya mwaka huu.


Wiki iliyopita Kamati ya Maendeleo ya Jamii ikikataa mapendekezo ya Bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, mwanzoni mwa wiki hii PAC iliziibua tuhuma za kuwapo wizi wa mabilioni ya fedha unaofanywa kutokana na kampuni za simu kukwepa kodi.


Jana PAC inayoongozwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ilipinga uamuzi wa Serikali kupunguza bajeti ya CAG kutoka Sh78 bilioni hadi Sh66 bilioni. Zitto alisema wamezigomea hoja za Dk Mgimwa na kumweleza kuwa kamati ikishapitisha bajeti ya ofisi ya CAG wizara haiwezi kuipunguza.


“CAG aliomba Sh78 bilioni, lakini wizara ikasema ina uwezo wa kutoa Sh66 bilioni tumemwita waziri aje kujieleza hata hivyo maelezo yake tumeyakataa,”alisema Zitto.


Alisema kuwa kwa mujibu wa Sheria ya Ukaguzi wa Umma Na 11 ya mwaka 2008 kamati ikishapitisha bajeti ya Ofisi ya CAG, wizara haiwezi kuipunguza na kwamba wameielekeza wizara kuacha bajeti kama ilivyopitishwa na kamati hiyo. Ofisi ya CAG imeomba kuidhinishiwa Sh78.8 bilioni, kati ya hizo Sh50.7 bilioni ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida, Sh6.6 bilioni kwa ajili ya mishahara na Sh21.3 bilioni kwa ajili ya maendeleo.


Makamu wa Rais
Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Lembeli alisema msimamo wa kamati yake unatokana na hesabu za bajeti kuonyesha kwamba kati ya Sh42.7 bilioni zilizotengwa, Sh30.6 bilioni zinakwenda Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa ajili ya mazingira.


Lembeli alisema Sh12.1 bilioni zinabaki Tanzania Bara na kati ya hizo, Sh3.7 bilioni ni za maendeleo na nyingine Sh3.2 bilioni zitatumika kwenye ujenzi.
“Tumeshindwa kupitisha bajeti kwa sababu fedha walizopewa hazifanani na mazingira ya kazi, jambo ambalo linaweza kuwafanya washindwe kuwajibika ipasavyo,”alisema Lembeli. Alitoa mfano wa Idara ya Mazingira ambayo imetengewa Sh1.3 bilioni ikiwa ni pamoja na mishahara ambayo ni kiasi cha Sh621 milioni, wakati Baraza la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wametengewa Sh3.1 bilioni.


Kwa mujibu wa Lembeli, fedha za ndani ni Sh3.7 bilioni, wakati fedha za wahisani ni Sh9.2 ambazo hazina uhakika wa kutolewa kwa wakati.
Alisema kwa jinsi hali ilivyo ni dhahiri kwamba ujenzi wa Ofisi za Makamu wa Rais Bara na Zanzibar hautatekelezwa kama inavyokusudiwa.


“Huwezi kuwa na ofisi kubwa kama hiyo ambayo iko chini ya Makamu wa Rais ambaye ni namba mbili kwa uongozi wa Taifa, lakini haipewi bajeti ya kutosha kwa ajili ya kutimiza majukumu yake,”alisisitiza Lembeli.

 Mbarawa agoma
Profesa Mbarawa aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba Serikali itaendelea na ratiba yake ya kuzima mitambo ya analojia kama ilivyokuwa imepangwa.


Juzi kamati hiyo kupitia mwenyekiti wake, Peter Serukamba walipendekeza wizara iongeze muda hadi 2015 ili kupunguza malalamiko yaliyopo kwa wananchi kutokana na kuzimwa kwa mitambo ya analojia.
“Changamoto tunazijadili na kuzifanyia kazi kwa sasa, lakini tutaendelea kuzima mitambo ya analojia na kuhamia dijitali kwa awamu ya pili,”alisema Profesa Mbarawa. Profesa Mbarawa alisema hata hivyo, miji mingi hapa nchini imekuwa ikitumia dijitali kwa muda mrefu hivyo ni miji michache tu ambayo ndiyo badi inatumia analojia. “Tutaendelea kuzima kwani huo wa kamati ni ushauri tu.”

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate