EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, April 5, 2013

Watu 45 kushtakiwa vurugu za huko Tunduma.

Mbeya na Dar es Salaam. 
Watu 45 watafikishwa mahakamani wakihusishwa na vurugu zilizozuka juzi katika Mji wa Tunduma.

Vurugu kubwa ziliibuka juzi kwenye Mji mdogo wa Tunduma ambao ndiyo Makao Makuu ya Wilaya ya Momba, mkoani Mbeya kwa baadhi ya wakazi kuwa na mvutano mkali kuhusu nani anayepaswa kuchinja mifugo baina ya waumini wa Kikristo na Waislamu.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Diwani Athumani alisema jana watu 94 ndiyo waliokamatwa kutokana na vurugu hizo.

Diwani alisema watu 49 wameachiwa kwa dhamana huku uchunguzi ukiendelea wakati waliobakia 45 ndiyo watafikishwa mahakamani. Vurugu hizo za Tunduma zilihusisha uchomaji wa matairi barabarani, kuweka mawe na magogo kwa lengo la kufunga barabara na kusababisha shughuli za kiuchumi kusimama na wananchi kujifungia ndani kwenye nyumba zao.

Diwani alidokeza, hata hivyo, hali ya utulivu imerejea kama kawaida na kwamba tayari wananchi wanaendelea na shughuli zao za kawaida ikiwa ni pamoja na eneo la mpakani.

“Kwa sasa hali imerudi kama kawaida na tumetangaziwa kuwa tuendelee na shughuli zetu na kwamba hali itakapobadilika tutoe taarifa polisi...Wametutaka kila mmoja kuwa na ulinzi hivyo watu wameshaanza kujitokeza barabarani na kufungua biashara zao,” alisema mkazi wa Tunduma aliyejitambulisha kwa jina la John Mwasyeba.

Mbatia alonga
Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) kimepanga kukutana na viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini ya Kiislamu na Kikristo nchini ili kumaliza tofauti zilizopo zinazojitokeza kati ya waumini hao.

Katika mkutano wao jana, TCD ambayo ni muungano wa vyama vya siasa vyenye wabunge bungeni vikiwemo CCM, Chadema, NCCR-Mageuzi, TLP, UDP na CUF vile ambavyo havina wabunge pia vina mwakilishi mmoja katika kituo hicho.
Kituo hicho kimesema kuwa kimechukua uamuzi huo baada ya nchi kukumbwa na migogoro ya kidini.

Mwenyekiti wa TCD, James Mbatia alisema jambo hili likiachwa litaligawa taifa na kwamba migogoro hiyo haina tija kwa taifa: “Amani ikitoweka katika taifa letu watakaoathirika ni Watanzania wote, ni lazima tukutane na viongozi hawa ili kujua tatizo ni nini, kufungua ukurasa mpya.”

Mbatia ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi alisema watakutana na viongozi hao Aprili 23 na 24 mwaka huu, tayari walishaelezwa jambo hilo na wamekubali.

Kwa nyakati tofauti, viongozi mbalimbali wa dini nchini wamekuwa wakiitaka Serikali kukaa meza moja na viongozi hao, baadhi ya viongozi waliotoa kauli hiyo ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo pamoja na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadji Mussa Salum.

Vurugu hizo za Tunduma zimejitokeza ikiwa ni siku tatu tu tangu Rais Jakaya Kikwete aonye kuwa vurugu zenye sura ya udini ni hatari na zinaweza kuvuruga amani na utulivu uliodumu kwa miaka mingi nchini.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate