EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, April 15, 2013

Simba yaibania Azam FC kusogea kileleni.

Ndoto ya Azam kuisogelea Yanga kileleni imeingia doa jana baada ya kulazimishwa sare 2-2 na Simba iliyoundwa na wachezaji chipukizi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Mabingwa watetezi Simba walikuwa wa kwanza kupata mabao yao mawili kupitia mshambuliaji wao Ramadhani Singano kabla ya Azam kuamka na kusawazisha mabao kupitia penalti ya Kipre Tchetche na bao lililofungwa na Humpfrey Mieno.

Kwa matokeo hayo Azam imefikisha pointi 47, wakati Yanga wakiwa kileleni na pointi 52, huku Simba wakibaki nafasi ya nne na pointi zao 36 na kupoteza matumaini ya kuiwakilisha nchi katika mashindano ya kimataifa mwakani.

Katika mechi ya jana, Azam walianza mpira vizuri na kufanikiwa kufika langoni mwa Simba katika dakika ya kwanza baada ya shuti la John Bocco kutoka pembeni kidogo ya goli.
Simba walianza vizuri jibu mapigo baada ya mpira wa kona iliyopigwa na Mrisho Ngassa kutua kichwani mwa Shomari Kapombe, lakini kipa wa Azam, Mwadini Ally alikuwa makini kuokoa hatari hiyo.

 Chipukizi Singano aliwainua mashabiki wa Simba kwa kufunga bao la kwanza katika dakika ya 11 akimalizia kazi nzuri ya Ngassa.
Wakati Azam wakiwa hawaamini kinachotokea Singano alifunga bao la pili katika dakika ya 18, baada ya Ngassa kumtoka beki wa Azam, David Mwantika na kupitisha pasi nzuri kwa chipukizi huyo.

Beki wa Azam, Mwantika alionekana mzito na kushindwa kwenda na kasi ya Ngassa na Singano waliomgeuza walivyotaka na kuipa Simba mabao mawili ya haraka.
Baada ya bao hilo kocha wa Azam, Stewart Hall alimtoa Luckson Kakolaki na kumwingiza Hamis Mcha katika dakika ya 20. Winga huyo alitumia dakika nane tu kabla ya kuangushwa kwenye eneo la hatari na beki Miraj Mdigo na mwamuzi Oden Mbaga kutoa penalti iliyofungwa na Kipre Tchetche.

Kiungo wa kimataifa wa Kenya, Humpfrey Mieno aliisawazishia Azam bao katika dakika ya 71 akiunganisha vizuri mpira wa adhabu uliopigwa na Mcha baada ya Tchetche kufanyiwa madhambi na Said Nasoro Cholo.
Katika mechi hiyo, mwamuzi Mbaga alimtoa katika benchi, Kocha Hall na kumtaka aende kukaa jukwaani baada ya kumbwatukia akipinga uamuzi wake

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate