JESHI la Polisi Mkoa wa Kinondoni, limefanikiwa kuwakamata watu 25
wanaotuhumiwa kwa kujihusisha na ujambazi wa kutumia silaha, pikipiki na
magari katika kufanikisha uhalifu wao.
Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, alisema watuhumiwa hao walikamatwa katika kipindi hiki cha sikukuu.
Alisema watuhumiwa hao ni wale wanaofanya uhalifu kwa kuvunja madirisha na kisha kuloa simu na mali nyingine zinazobebeka kwa kutumia ndoano iliyofungwa kipande cha wavu kwa kutumia kitambaa cha chandarua kilichofungwa misili ya goli la kwenye mchezo wa mpira wa kikapu.
“Mbinu hiyo ya uhalifu imepewa jina la Jordan, ambalo ni la mchezaji maarufu wa mchezo wa mpira wa kikapu aitwaye Michael Jordan.
“Wahalifu hao pia hutumia mbinu ya kufanya ujambazi kwa kukata makufuli na makomeo ya milango kwa kutumia mikasi maalumu, ambayo huweza kukata kitu chochote na kufanikisha kuingia mahala ambapo wamepadhamiria kufanya uhalifu.
Alisema miongoni mwa watuhumiwa waliokamatwa ni wale waliowahi kufanya matukio mbalimbali ya uhalifu katika maeneo ya Kinondoni na Jiji la Dar es Salaam.
Matukio hayo kwa mujibu wa Kenyella, ni pamoja na wale
wanaojihusisha na wizi wa magari ambapo Machi 27 mwaka huu huko eneo la
Kinondoni Mtambani, majambazi watatu walipora gari No T 331 BPK aina ya
Toyota Rav4 na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao ambao walikiri
kupora gari hiyo.Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, alisema watuhumiwa hao walikamatwa katika kipindi hiki cha sikukuu.
Alisema watuhumiwa hao ni wale wanaofanya uhalifu kwa kuvunja madirisha na kisha kuloa simu na mali nyingine zinazobebeka kwa kutumia ndoano iliyofungwa kipande cha wavu kwa kutumia kitambaa cha chandarua kilichofungwa misili ya goli la kwenye mchezo wa mpira wa kikapu.
“Mbinu hiyo ya uhalifu imepewa jina la Jordan, ambalo ni la mchezaji maarufu wa mchezo wa mpira wa kikapu aitwaye Michael Jordan.
“Wahalifu hao pia hutumia mbinu ya kufanya ujambazi kwa kukata makufuli na makomeo ya milango kwa kutumia mikasi maalumu, ambayo huweza kukata kitu chochote na kufanikisha kuingia mahala ambapo wamepadhamiria kufanya uhalifu.
Alisema miongoni mwa watuhumiwa waliokamatwa ni wale waliowahi kufanya matukio mbalimbali ya uhalifu katika maeneo ya Kinondoni na Jiji la Dar es Salaam.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Ayoubu Mohamed (20), Mkude Said (28) na Deogratius John(23) ambao wote ni wakazi wa Dar es Salaam.
Alisema upepelezi juu ya watuhumiwa hao unaendelea ili waweze kufikishwa mahakamani.
Kwa mujibu wa Kenyella, Polisi pia inawashikilia wezi wa bajaj zilizoibiwa katika eneo la Oysterbay, watuhumiwa wengine wawili wanaojihusisha na ukwapuaji wa mikoba kwa kutumia pikipiki.
Katika msako wao huo, pia walifanikiwa kukamata silaha mbalimbali, ikiwemo Bunduki aina ya shortgun iliyokamatwa eneo la Kigogo round about na bastola aina ya Glock 19 yenye namba LZB 642 na T CAR 98189 ikiwa na risasi 12 katika magazine iliyokamatwa Mabibo.
No comments:
Post a Comment