EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, April 10, 2013

YANGA WAKATAA RASMI MECHI ZAO KUONYESHWA BURE NA SUPER SPORT

Siku moja baada ya shirikisho la soka nchini TFF kubadilisha ratiba ya baadhi ya mechi za ligi kuu ya Tanzania bara ili kuweza kufanikisha mpango wa kuonyesha mechi hizo kupitia kituo cha Supersport, klabu ya Yanga kupitia makamu wake mwenyekiti Clement Sanga imesema haikubaliani na mpango huo kwasababu haujafuata utaratibu na pia utaziingizia hasara kubwa klabu zinazohusika na mpango huo.
Akizungumza na mtandao huu Sanga alisema kwamba mpango huo wa kuonyesha mechi za ligi kuu bure kwenye Supersport haupo katika kuzinufaisha vilabu bali wahusika wengine wa mpango huo.

"Kwanza jambo muhimu kuhusu suala hili kumekuwepo na mfumo m'bovu wa mawasiliano baina ya TFF, Supersport na vilabu vyenyewe kama Yanga. Sisi kwa upande wetu tunaona kabisa huu mpango unatuingizia hasara sana, kwa mfano baada ya kubadilisha ratiba ya mechi zetu tutacheza mechi 3 ndani ya siku 8 wakati ilitakiwa ndani ya wiki tucheze mechi mbili na bado ukumbuke bado tunapaswa kusafiri kwenda Tanga hivyo kuna mambo ya gaharama na vitu vingine vingi tu. Lakini pia mechi ambazo wanataka kuzionyesha bure ni zile ambazo sie vilabu tunazitegemea sana kwenye suala zima la mapato na wao ndio wanataka kuzionyesha bure - na watanzania wengi wanaposikia hivyo mahudhurio uwanjani yanakuwa hafifu hivyo tunakosa mapato. Bora waonyeshaji wa mechi hizo wangekuwa wanatoa fidia kiasi fulani kutokana na matangazo ya kibiashara wanayopata ili kuweza kuzinufaisha klabu zetu, lakini si hivyo wanavyotaka wao. Nadhani kwenye hili TFF wangeliangalia vizuri liweze kutunufaisha sote na sio watu wachache kama ilivyo sasa," Aliongeza Sanga.

Alipoulizwa kama wameshawasilisha msimamo wao kwa uongozi wa TFF na kamati ya ligi Clement Sanga alisema, "Kwanza walipotuletea taarifa kuhusu jambo hilo kwa njia ya barua pepe tuliwajibu na baadae ikaja barua ambayo katibu wetu alijibu kutoa msimamo wetu juu ya suala hili, kinachojitokeza hapa TFF wanatumia mabavu yao kutupeleka peleka, sie tumeshika makali wao mpini. Sie tusipokubali kucheza jumatano kama wanavyotaka wao basi watachukua maamuzi ya kuigawia timu pinzani ushindi, la msingi sie tutakalolifanya hatutokubali mechi zetu zionyeshwe kwenye TV bila kupata fidia ya fedha. Sisi kama Yanga hatupo tayari kuona tunafanyishwa kazi bure. Supersport imeshafanya majaribio sana, sasa haya ya sasa nini? Viongozi wa soka tubadilike tuweke mbele maslahi ya soka letu kabla ya kujiridhisha nafasi zetu, haiwezekani watu wawili watatu waamue tu kwamba mechi kesho hakuna bila kujali hasara zitakazowagharimu wengine. Sie tulishajipanga kwamba Jumatano tunacheza na Oljoro, then tunasafiri kwenda Tanga kucheza na Mgambo then turudi Dar kwa ajili ya mchezo mwingine. Matayarisho ya mechi hizi tulishafanya wiki mbili kabla, tukalipia hotel na gharama nyingine, sasa haiwezekani ghafla kikundi cha watu fulani wenye nguvu za kimaamuzi kutubadilishia ratiba - je zile fedha tulizolipa mahoteli watatulipa akina nani, kwa sababu ni dhahiri unapolipia hotel unapewa na muda wa kuivitumia vyumba vile hivyo muda ule unapoisha fedha yako inakuwa imeenda. Nadhani hili suala linahitaji kuangaliwa vizuri, na viongozi wa vilabu tuwe na umoja kuweza kulipigania hili suala dhidi yetu. Tusiwe viongozi wa kuburuzwa ovyo ovyo."

Akizungumzia mahitaji wanayotaka ili wakubali mechi zao ziweze kuonyeshwa kwenye TV, Sanga alisema kwamba hicho kituo cha TV kinachotaka kurusha matangazo ya moja kwa moja ya mechi zao inabidi walete ofa ya kueleweka ambayo itaweza kufidia hasara ya kwenye mapato na gharama nyingine ambazo timu wataziingia ili kuweza kwenda sawa na ratiba zao. Pia akataka uwepo uwazi wa makubaliano yote ya kimsingi ili kuepusha migogoro ya namna hii.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate