EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, May 12, 2013

KUTOA ASANTE YA MWILI NI KUJIDHALILISHA.

NINA imani wote m’wazima wa afya njema kwa uwezo wake Manani.  Leo nataka nizungumzie tofauti ya upendo na msaada.  Sote tunajua katika penzi la kweli kuna kujaliana katika shida na raha na kuonyesha upendo wa mtu kwa mwenzake.
Tunajua wote katika mapenzi  kuna kupendana ili kukamilisha pea ya upendo ikimaanisha kila mmoja ampende mwenzake kwa dhati.
 

Penzi la upande mmoja tumeona si kamili kwa vile mpendaji huwa mmoja na mwingine huwa yupo na mwenzake kwa sababu fulani, akishakidhi haja zake huondoka bila kwa heri na kusababisha mateso kwa mmoja.
 

Kuna tatizo limejitokeza kwa kina dada kuamini mtu anayempa msaada basi anamhitaji kimapenzi. Kweli anayekusaidia lazima atakuwa mtu anayejua utu wa mtu bila kuangalia anakujua au la.
Sehemu hii imekuwa ikiwachanganya wengi na kuingia kichwakichwa mwisho kuachwa njia panda na kuona umegeukwa, yaani mtu uliyemuamini amekugeuka.


Kwa nini?
Upendo na msaada ni vitu viwili tofauti, msaada umo ndani ya upendo kwa maana anayekupenda atakusaidia katika shida na raha, lakini si kila msaada una upendo.



Kwa sababu gani?
Tumeona kwenye usafiri wanawake wamekuwa viumbe dhaifu pale wanapopewa msaada na mwanaume na huamini msaada ule ni dalili za kupendwa, kumbe aliyetoa msaada hakutoa kama sehemu ya kuonyesha anakuhitaji kimapenzi bali kukusaidia kama mwanadamu mwenzake.
 

Wanawake wengi wamekuwa wakipoteza dira ya maisha kwa kuanzisha uhusiano na mtu anayekutana naye safarini na kumpa msaada kama chakula au kumsaidia mtoto. Baada ya msaada huo mioyo yao huwa dhaifu na kuamini yule ndiye mwanaume sahihi kwa vile kamsaidia bila kumjua pengine msaada huo haupati kwa mwenza wake.
Mara moja huanzisha uhusiano na kupeana namba za simu ili watafutane baadaye. Wanawake wengi hufikia hatua ya kuzikana ndoa zao kwa vile tayari mioyo yao imeishakurupuka bila kufikiri.
 

Wengi wao wamekuwa wakifunga hata safari kuwafuata watu hao hata kama ni mbali bila kuijua historia ya mtu waliyekutana naye kwenye gari.
Baada ya kukutana ndipo wanapokutana na tabia tofauti na waliyoifikiria, hapo ndipo yanakuja majuto. Wapo wanaodiriki kuvunja hata uhusiano wao kwa penzi la mwanaume wa safarini na kuamini aliyekuwa naye si lolote si chochote kwa mwanaume aliyekutana naye.
 

Hata kama hakumfuata, hicho huwa chanzo cha nyumba kuvunjika au kuingia kwenye migogoro kwa vile  akili yao wameihamishia kwa mwanaume wasiyemjua.
Baada ya kuachwa anaangukia pua kwa vile yule mtu aliyetoa msaada haukuwa kwa lengo ya kumvuta kimapenzi.
 

Hivyo, inatakiwa tuwe makini sana na uamuzi wetu wa kukurupuka, si kila msaada unaopewa asante yake ni kumvulia nguo mwanaume. Utawavulia nguo wangapi watakaokusaidia?  Kumbuka kusaidiwa ni haki yako kama mwanadamu na si kwa ajili ya kudhalilishwa.
 

Uheshimu utu na mwili wako, kwa sababu heshima ya mtu huijenga mwenyewe hujengewi na mtu. Usikubali kuutoa mwili wako kama asante kwa msaada utakaopewa, asante ya domo inatosha.
 

Kama mtatongozana hiyo ni hiyari yenu kukubali au kukataa,  uwe muwazi ili kujiweka eneo salama kwa kuheshimiwa na si kuukana uhusiano wao kwa vile tu umenunuliwa chipsi na kuku pengine soda na kitafunwa.
Akitoa ni kwa upendo wake una haki ya kukubali au kukataa si kila upewacho lazima ukubali kuchukua na asante yako ni kuutoa asusa mwili wako!

Tukutane wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate