EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, May 31, 2013

MATOKEO MAPYA: Kidato cha nne majanga tena.

MATOKEO ya kidato cha nne ambayo serikali iliagiza yapitiwe upya na kufanyiwa uhakiki kwa vigezo vya miaka ya nyuma, yametolewa jana huku kukiwa na mabadiliko kidogo.
Matokeo hayo mapya yalionyesha hali bado ni mbaya kwani ni watahiniwa 30,000 tu kati ya 240,909 waliopata daraja sifuri ndiyo walionufaika na ‘mbeleko’ ya serikali.
Mabadiliko hayo yanaonyesha waliopata daraja sifuri wamepungua kidogo na sasa wamefikia 210,846.
               Waziri wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa.
Matokeo yanaonyesha kiwango cha ufaulu kimeongezeka kwa asilimia 9 ambapo mara ya kwanza ilikuwa asilimia 34.5 wakati hivi sasa ni asilimia 43.08.
Matokeo hayo mapya yanaonyesha kuwa takriban asilimia 61 ya watahiniwa walipata daraja sifuri awali sasa yamepungua na kuwa asilimia 56.9.

Akitangaza matokeo hayo kwa waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam, Waziri wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, alisema hali bado ni mbaya.
Kawambwa alisema kuwa jumla ya watahiniwa 480,029 walisajiliwa kufanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana wakiwemo wasichana 217,587 sawa na asilimia 45 .33 na wavulana 262,442 sawa na asilimia 54.67.

Alisema watahiniwa waliofanya mtihani ni 458,139 sawa na asilimia 95.44 ambapo watahiniwa 21,890 sawa na asilimia 4.56 ya watahiniwa wote waliosajiliwa hawakufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali.

Alibainisha kuwa matokeo ya watahiniwa wa shule 159,609 kati ya watahiniwa 397,138 waliofanya mitihani walifaulu ambapo wasichana walikuwa 60,751 na wavulana walikuwa ni 98,858.

Kawambwa alisema ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa wa shule unaonyesha jumla ya watahiniwa 35,349 wamefaulu katika daraja la 1-111 ambapo kati yao wasichana ni 10,924 na wavulana ni 24,425 sawa na asilimia 43.08.

Matokeo ya awali yaliyotangazwa yalionyesha kuwa kati ya watahiniwa 367,756 waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana, waliokuwa wamefaulu kwa daraja la kwanza mpaka la tatu walikuwa 126,847 sawa na asilimia 6.4. Waliopata daraja la nne walikuwa ni 103,327 sawa na asilimia 28.1.
Idadi ya watahiniwa waliotangazwa hapo awali na waliotangazwa sasa imeonyesha pia kuwa na tofauti ambapo awali waziri alisema kuwa jumla ya watahiniwa 35,349 wamefaulu katika madaraja 1-111 ambapo kati yao wasichana ni 10,924 na wavulana ni 24,425.

Aliongeza kuwa katika matokeo hayo watahiniwa wa kujitegemea waliosajiliwa walikuwa 68,804 wakiwemo wasichana 34,605 sawa na asilimia 50.30 na wavulana 34,199 sawa na asilimia 49.70 ambapo alisema watahiniwa 61,001 wakiwemo wasichana 30,918 na wavulana 30,083 wamefanya mitihani wakati watahinmiwa 7,803 sawa na asilimia 11.34 hawakufanya mitihani.

Alzitaja shule za sekondari zilizoshika nafasi ya kumi katika kundi la shule zenye watahiniwa 40 na zaidi ni shule ya wasichana St. Fransic iliyoko Mbeya, Marian Pwani (Wavulana) na Feza Boys Dar es Salaam.

Shule nyingine ni Canosa, Feza Girls, Rosmini Girls, Anwarite Girls, St. Marys Mazinde Juu na Jude Moshono.
Pia alisema matokeo ya kupangiwa shule watakazotakiwa waende yatafanyika mwezi Juni na wanafunzi wataanza kidato cha sita mwezi Julai.
“Tumefanya hivyo, hatukuchakachua na matokeo haya ni halali kabisa hivyo ndiyo yatakayokuwa rasmi kutumika sehemu yoyote na si yale ya awali kama ilivyokuwa mwanzo,” alisema Waziri Kawambwa.

Shule watakazopangiwa
Kawamba alisema watahiniwa hao watapangiwa shule watakazotakiwa waende kuanzia kesho na wanafunzi wataanza kidato cha sita mwezi ujao.
“Tumefanya hivyo hatukuchakachua na matokeo haya ni halali kabisa hivyo ndiyo yatakayokuwa rasmi kutumika sehemu yoyote na si yale ya awali,” alisema Kawambwa.
Alisema pia baada ya kufanya kwa marekebisho hayo ufaulu umeongezeka kutoka asilimia 34.5 awali na sasa 43.08 huku akieleza kuwa mwaka 2001 matokeo yalikuwa juu kwa asilimia 53.
Hata hivyo alisema kuanzia sasa utatumika mfumo mpya ambapo alama zote zitakuwa sawasawa na hakutakuwa na tofauti za alama katika masomo.
Kwa maelezo zaidi soma tangazo ukurasa wa 20

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate