EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, June 8, 2013

Kitimtim cha Kili Music Awards 2013 Usiku wa leo.


Hatimaye siku imetimia, ile siku ambayo kila mja na muungwana katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya alikuwa akiingoja, usiku wa tunzo za Kilimanjaro Tanzania, zitaunguruma kuanzia saa moja hadi kuendelea, Watanzania takriban 32 wanaofanya kazi katika tasnia ya muziki wanatarajiwa kuondoka na tunzo mikononi mwao leo.

Zaidi ya wasanii 100 wametajwa kuwania tunzo hizi, na wote wana imani ya ushindi na watakuwa ukumbini leo pamoja na baadhi ya mashabiki wao, kushuhudia matokeo ya kazi ngumu waliyoifanya katika msimu uliopita wa muziki wa Tanzania.

Kampuni ya Bia Tanzania kwa kupitia kinywaji chake cha Kilimanjaro, kilichodhamiria kupeleka muziki wa Tanzania katika kilele cha mafanikio, leo ndiyo mwenyeji wa shughuli husika na wameahidi usiku wa kihistoria, huku wakiadhimisha mwaka wa 13, wa tunzo hizi ambazo kila kukicha zinazidi kujizolea umaarufu.

George Kavishe, ni Meneja wa bia ya Kilimanjaro na amefanya mahojiano na gazeti hili kuhusiana na usiku wa leo na mambo muhimu makubwa matatu yametajwa katika kuunogesha usiku mwingine wa tunzo, uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu.

Kwanza, usiku hautakuwa Dar es Salaam peke yake utakuwa katika mikoa ya Mwanza, Kilimanjaro na Dar ambapo katika viwanja mbalimbali vya Taifa Dar es Salaam, Mabatini Mwanza, na CCM Mkoa kwa Kilimanjaro kutakuwa na TV kubwa zitakazokuwa zikionyesha moja kwa moja tukio la utoaji tunzo litakalokuwa likiendelea katika Ukumbi wa Mlimani City usiku wa leo.

Watazamaji wa mikoani, watashuhudia tunzo hizo kwa kiingilio cha bia moja tu milangoni, na wakiingia katika viwanja hivyo watakuta maandalizi mazuri kutoka kampuni ya bia Tanzania, na watakuwa wakishuhudia onesho lote, pamoja na burudani mbalimbali zitakazokuwa zinatolewa na waandaaji.

Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es salaam watakaopata bahati ya kuhudhuria onesho hilo ambapo kiingilio kitakuwa Sh 75,000 kwa watu maalumu na kawaida itakuwa Sh20,000.

“Sababu mbili za msingi za kuweka onesho hili uwanjani, kwanza, ni kutokana ma mfumo wa digitali, ambapo Watanzania wengi wameshindwa kukabiliana nao kutokana na hali ya kiuchumi, hivyo tumewapa fursa nyingine ya kushuhudia tunzo, lakini pia tungependa mashabiki wakae pamoja na kushuhudia tukio hili la kihistoria,” alisisitiza George Kavishe.
Red Carpert
 
Hili ni zoezi litakalohusisha mastaa hasa upande wa mitindo, ambapo picha zitakuwa zikichukuliwa, katika kuperuzi nani kaja vipi na kavaa nini na alikuwa amesindikizwa na nani.

Hii itakuwa na mtangazaji wake na itakuwa ni kama sehemu ya kipindi cha TV na kwa habari tulizonazo, ni kwamba mtangazaji wa Channel O na mdau mkubwa wa burudani, Jokate Mwegelo ndiye atakuwa mwendeshaji.
Kwa mujibu wa waandaaji, zoezi litachukua kama saa limoja hivi, maana shughuli yenyewe itaanza saa mbili usiku.
Burudani
 
Itakuwa katika makundi manane, lakini si burudani ambayo umewahi kuiona mahala popote pale, ni burudani itakayozingatia kauli mbiu ya tunzo hizo kwa mwaka huu, kikwetukwetu.
Kwa mujibu wa Kavishe ni kwamba kamwe, hutaona mwanamuziki akiimba wimbo wake uliouzoea, au unaouona akiuimba kila siku, pale atakuwa katika mwonekano mwingine na ni burudani ambayo mwisho ni itakusisimua uhisi kwamba umesogea hatua moja tangu uanze kuburudishwa na sanaa ya muziki wa jukwaani.

Kavishe amethibitisha kwamba hakuna mwanamuziki wa nje aliyehusishwa na burudani za muziki wa Kili mwaka huu, burudani nzima itakuwa ikiendeshwa na wanamuziki wa nyumbani.
Wanaotajwatajwa...
Wanamuziki Ben Pol, Vanessa Mdee na Ommy Dimpoz wametajwa sana na mashabiki kwamba huenda ukawa ni mwaka wao kwa mujibu wa tunzo hizo na hii ikaja baada ya kuonekana kutajwa mara nyingi sana katika kuwania tunzo hizo.

Mmoja kati ya mashabiki wakubwa wa muziki na mdau, Poti Poti kutoka maeneo ya Kawe, jijini Dar es Salaam ameliambia Mwananchi kwamba mwaka huu wanamuziki hao huenda wakaigeuza kabisa historia ya muziki wa kizazi kipya kutokana na kazi yao nzuri waliyoifanya mwaka jana.
Ben Pol, mpaka sasa anashikilia tunzo ya mwanamuziki bora wa R&B ambapo Vanessa Mdee ni mwanamuziki mpya kabisa kwenye tasnia ya muziki na ni mmoja kati ya wanamuziki wanaowania tunzo ya mwanamuziki chipukizi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate