EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, June 12, 2013

Lwakatare apata dhamana, Ludovick akwama

Dar es Salaam. 
Baada ya kusota rumande kwa takriban miezi mitatu, hatimaye Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare ameachiwa kwa dhamana.

Hata hivyo, mwenzake Joseph Ludovick ambaye wanashtakiwa pamoja, alikwama kupata dhamana baada ya wadhamini wake kushindwa kuwa na vielelezo vyenye vigezo kulingana na masharti ya dhamana
hivyo alirejeshwa rumande.

Baada ya Lwakatare kuachiwa, alipokewa kwa shangwe na wafuasi wa Chadema waliokuwa na mabango yenye maandishi mbalimbali ya kuelezea furaha yao na mengine yakikiponda chama tawala CCM, huku wakimshangilia kwa kuimba: “peoples’ power... peoples’ power!” wakiwa na maana ya nguvu ya umma.

Akitoa uamuzi kuhusu dhamana hiyo, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Aloyce Katemana alisema imetolewa baada ya kuzingatia kigezo cha washtakiwa kufutiwa mashtaka ya ugaidi ambayo yalikuwa yanaangukia kwenye sheria inayozuia dhamana.

Aliwataka washtakiwa kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika na wanaotoka katika taasisi zinazotambulika kisheria.
Sharti lingine ni kila mdhamini kutia saini hati ya udhamini ya Sh10 milioni pamoja na washtakiwa wenyewe.

Hakimu huyo pia aliwataka washtakiwa kusalimisha hati zao za kusafiria mahakamani na kutokutoka nje ya Dar es Salaam bila ya kuwa na kibali cha Mahakama.
Hakimu Katemana aliiahirisha kesi hiyo hadi Juni 24, mwaka huu itakapotajwa tena kwa lengo la kujua iwapo upelelezi umekamilika ili ipangiwe tarehe ya kuanza kusikilizwa.

Awali, uamuzi huo wa dhamana ulipangwa kutolewa Mei 13, mwaka huu lakini ulikwama baada ya Katemana kuripotiwa kuwa likizo na badala yake, Hakimu Mkazi Sundi Fimbo aliitaja tu kesi hiyo na kuiahirisha.


Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare (mbele) akisindikizwa na wafuasi wa chama hicho kutoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam jana baada ya kuachiwa kwa dhamana.

Mei 27, mwaka huu ilitajwa tena hata hivyo uamuzi wa dhamana haukutolewa.
Awali, Lwakatare kupitia kwa mmoja wa mawakili wanaomtetea, Peter Kibatala aliwasilisha maombi ya dhamana mahakamani hapo Mei 13, mwaka huu wiki moja baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kumfutia mashtaka matatu ya ugaidi yaliyokuwa yakimkabili.

Pamoja na dhamana hiyo, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) tayari ameandaa maombi ya marejeo katika Mahakama ya Rufaa akipinga uamuzi wa Mahakama Kuu wa Mei 7, mwaka huu kuwafutia mashtaka ya ugaidi washtakiwa hao.

Katika maombi hayo, DPP anaiomba mahakama hiyo iitishe majalada ya kesi hiyo na kuchunguza uhalali wa uamuzi huo wa Mahakama Kuu, uliotolewa na Jaji Lawrence Kaduri.
Anadai kuwa katika hati ya maombi ya washtakiwa hao waliyowasilisha Mahakama Kuu, hapakuwepo na maombi ya kufuta mashtaka na kwamba hapakuwa na taarifa zilizowasilishwa dhidi ya washtakiwa ambazo Mahakama Kuu ingezizingatia katika kufikia uamuzi.

Hata hivyo, jopo la mawakili wa Lwakatare nalo liliwasilisha pingamizi la awali dhidi ya maombi hayo ya DPP, likiainisha hoja mbili ambazo mawakili wake watazitoa wakati wa usikilizwaji wa maombi hayo.

Lwakatare anadai kuwa maombi hayo ya marejeo yana dosari ambazo haziwezi kurekebishwa kutokana na kushindwa kuambatanisha nakala ya mwenendo wa uamuzi unaolalamikiwa ambao ndipo maombi hayo yalipojengwa na kwamba kiapo kinachounga mkono maombi hayo kimehusisha mambo mengine yasiyohusika.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate