EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, June 7, 2013

MAELFU WAFURIKA KUMZIKA COWBOY YATIKISA MOROGORO JANA.

MAZISHI ya msanii maarufu wa muziki wa kizazi kipya, Albert Mangwair, yaliyofanyika makaburi ya Kihonda-Kanisani, jana yaliutikisa mji wa Morogoro mbele ya Mkuu wa Mkoa huo, Joel Bendera.
Shughuli hiyo ilitanguliwa na kuaga mwili na ilifanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri kutokana na wingi wa maelfu ya watu.
 Hapa jeneza la Ngwair linaingizwa karubini, ikiwa ni picha inayoonyesha kuwa hatutaweza tena kukutana na msanii huyu hapa chini ya jua. R.I.P Ngwair

Wingi wa watu ndio uliifanya Kamati ya Mazishi chini ya Adam Juma, ihamishie hafla hiyo Uwanja wa Jamhuri badala ya nyumbani kwa usalama zaidi.
Mji wa Morogoro ulianza kuzizima tangu asubuhi, baada ya kushuhudia vikundi vya watu wengi vikielekea Jamhuri wakiwa kwa miguu, pikipiki, baiskeli na wengine kwenye magari vikienda na kurudi.

Wasanii na viongozi mbalimbali, akiwamo Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, nao walikuwapo kwenye tukio la kuaga mwili wa Ngwair na baadaye kwenye mazishi yake ambayo yalizua mkanyagano wa aina yake.

Idadi kubwa ya watu ilijitokeza katika shughuli ya kumuaga marehemu, ambapo pia ilikimbilia makaburini kwa ajili ya kushuhudia mwili wake ukiingia kaburini.
Awali, Mkuu wa Mkoa Morogoro, Joel Bendera, alifika nyumbani kwa mama wa marehemu saa nne za asubuhi na kupata fursa ya kuwapa pole wafiwa.
Akizungumza na wanafamilia na baadaye Uwanja wa Jamhuri, Bendera alisema Tanzania imepoteza msanii nyota na mwenye bahati ya kupendwa na watu wengi.

“Hii ni hatari kubwa maana Ngwair ameonyesha ni kiasi gani alikuwa nyota katika tasnia ya muziki wa Hip Hop kwa umahiri wake, sambamba na kuishi na watu vizuri.
“Hii leo ni historia katika mkoa wa Morogoro, hususan kwa kushuhudia watu wengi wakiwa na huzuni katika kumuaga msanii wao mpendwa kwa namna moja au nyingine, hivyo serikali itaendelea kufanyia kazi changamoto zinazowakabili vijana hawa,” alisema Bendera.

Naye Mbunge wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, alisema wasanii wamechoka kuishi kimaskini wakati watu wengi wanaheshimu kazi zao.
“Inaumiza kuona tunazikwa kwa mtindo huu wakati maisha yetu ni magumu mno, hivyo hatuwezi kuona hali hii inaendelea kuota mizizi, hivyo wasanii tuendelee kuwa makini katika hili.

“Matatizo yaliyompata Ngwair katika maisha yake ni sehemu ya changamoto zilizopo katika tasnia hii ya muziki wa kizazi kipya, ingawa tukifa mazishi yetu yanakuwa ya heshima mno,” alisema.
Pamoja na kukusanya watu wengi, watu wengi walionekana kwenda uwanjani kuwaona wasanii wengine, hivyo kusababisha mkanyagano kila anapoingia au kutoka msanii nyota.
Baadhi ya wasanii wenye majina makubwa walikuwa Wema Sepetu aliyelazimika kujificha kila wakati kutokana na mayowe ya watu.

Hata hivyo, matatizo yalianza kujitokeza wakati wa kuaga mwili kutokana na askari kushindwa kukabiliana na wingi wa watu katika kuwadhibiti.
Wakati wa shughuli ya kuaga, ghafla, rafiki wa Ngwair, aliyopata matatizo naye Afrika Kusini, Mgaza Pembe, M 2 The P, aliletwa uwanjani hapo kumuaga Ngwair.

Baada ya kuona muda unazidi kwenda na watu hawaishi, shughuli ya kuaga ilikatishwa na kuanza msafara kuelekea makaburini, Kihonda Kanisani.
Barabara zilizopitiwa na msafara wa mwili wa Ngwair, zilikuwa zimejaa watu wakiwa na nia ya kumungalia nyota wao akielekea nyumba yake ya milele baada ya kufariki Afrika Kusini, Jumanne ya wiki iliyopita.

Kufika makaburini, umati mkubwa wa watu ulikuwapo, hivyo ndugu wa marehemu kukosa muda wa kutia mchanga katika kaburi, hasa pale watu waliposhindwa kusogea.
Kaka wa marehemu, Kenneth Mangwea, aliwashukuru Watanzania kwa moyo wao wa upendo kiasi cha kushirikiana na wao kuhakikisha kuwa mwili wa Ngwair unazikwa Tanzania.
“Nashukuru sana, natumia muda huu kuwatakia upendo zaidi na zaidi Watanzania wenzetu, sambamba na kumtakia mapumziko mema huko mbinguni Ngwair,” alisema Kenneth.
Hatari kubwa ilijitokeza makaburi ya Kihonda Kanisani, kutokana na barabara kufurika watu na hata eneo la makaburi.

Mwili wa Mangwair ulizikwa majira ya saa tisa za mchana, ikiwa ni siku moja tangu aagwe kwenye Viwanja vya Leaders, jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate