EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, June 11, 2013

Mbunge ataka rais ashitakiwe asipotimiza ahadi.

MBUNGE wa Viti Maalumu, Suzan Lyimo (CHADEMA), amesema marais wanaoshindwa kutekeleza ahadi zao mpaka wanapomaliza vipindi vyao vya uongozi washitakiwe.

Lyimo alitoa kauli hiyo bungeni jana wakati akiuliza swali la nyongeza ambapo alisema wabunge wengi hususan wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanalalamika kwa kutotekelezwa kwa ahadi za marais na kutaka wapelekwe mahakamani walishindwa kufanya hivyo.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, alisema katika ahadi za rais hakuna mtu wa kushitakiwa na kwamba ahadi zinazotolewa na hutekelezwa na serikali.

“Ahadi inayotolewa na rais utekelezaji ni jukumu la serikali na fedha inatoka serikalini haitoki mfukoni mwa rais sasa hapa hakuna wa kushitakiwa, kwani rais aliyepo madarakani akiondoka atakuja mwingine ambaye ataendelea na utekelezaji wa ahadi zilizobakia,” alisema Lukuvi.
Alisema serikali kwa kadiri ya uwezo wake imejitahidi kutekeleza ahadi mbalimbali zinazotolewa na viongozi wa juu serikalini.

Awali katika swali la msingi Mbunge wa Mkinga, Dustan Kitandula (CCM) alitaka kujua hatua zilizochukuliwa hadi sasa katika utekelezaji wa ahadi ya rais ya kujenga Hospitali ya Wilaya ya Mkinga pia alitaka kujua ni lini utekelezaji wa ahadi za rais utakamilika.

“Wakati wa ziara yake wilayani Mkinga, rais aliahidi kujengwa haraka Hospitali ya Wilaya ya Mkinga kutokana na kukipandisha hadhi Kituo cha Afya Maramba ili kitoe huduma za hospitali ikiwamo upasuaji, utekelezaji wa ahadi hizo umefikia wapi?” alihoji.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Afya, Dk. Seif Rashid, alikiri kwamba katika mwaka 2010 rais alipotembelea wakazi wa Mkinga aliahidi kupandisha hadhi Kituo cha Afya cha Maramba ili kiweze kutoa huduma za dharura lakini pia aliahidi kuharakisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mkinga.
“Hata hivyo katika kutekeleza ahadi hizo serikali imetumia jumla ya sh milioni 132.1 kuboresha miundombinu ya Kituo cha Afya Maramba ili kiweze kupandishwa hadhi na kutoa huduma bora zinazoendana na hospitali,” alisisitiza naibu waziri huyo.

“Kazi zilizofanyika ni upanuzi wa eneo la kituo hicho kwa kuhamisha makazi ya watu wanne na kuwalipa fidia, kufanya ukarabati wa chumba cha upasuaji, kuweka upya mfumo wa umeme na maji taka, kununua kontena kwa ajili ya kutengeneza chumba cha mapokezi na kununua mashine ya dawa ya usingizi na mashine ya kufua nguo,” alisema Dk. Rashid.
Kuhusu ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mkinga, alisema imeshatoa sh milioni 221.4, ambapo sh milioni 21 zimetumika.

Aidha, alisema kwa sasa Kituo cha Afya cha Maramba kinatoa huduma zote muhimu isipokuwa upasuaji kwa wajawazito na chumba cha upasuaji kipo katika hatua ya mwisho ya ujenzi na kinatarajiwa kukamilika kabla ya Julai mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate