EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, June 6, 2013

Rasimu yavuruga mipango ya urais 2015

Dar es Salaam/Dodoma: 
Mapendekezo yaliyotolewa katika Rasimu ya Katiba Mpya na Tume ya Marekebisho ya Katiba yamewavuruga wanasiasa ambao tayari walikuwa wamejipanga kwa ajili ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, Mwananchi limebaini.


Tangu juzi Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba alipotangaza rasimu hiyo, kumekuwa na wasiwasi mkubwa sasa kwamba mipango ya urais wa 2015 itavurugika ikiwa mapendekezo hayo yatapitishwa.



Tishio kubwa katika rasimu hiyo ni pendekezo la kuwapo kwa Serikali ya tatu hali ambayo inatafsiriwa na baadhi ya wanasiasa kwamba inaondoa nguvu ya Rais yeyote; awe wa Jamhuri ya Muungano, Zanzibar au Tanzania Bara.


Habari za kuaminika zilizopatikana kutoka ndani ya kambi za vyama vya CCM na Chadema zinaeleza kuwa wale waliokuwa wakifikiria kuwania nafasi hiyo wameingiwa na wasiwasi.

Kadhalika, suala la umri wa kuwania urais kubakia miaka 40 pia linaonekana kuwagusa waliowahi kutangaza kutaka nafasi hiyo ya juu ya uongozi wa nchi kabla ya mapendekezo ya tume.


Katika suala la urais, wanasiasa wenye nia hiyo wanauona uongozi wa Jamhuri ya Muungano kuwa ni kama hauna nguvu tena kutokana na kushughulikia mambo machache, lakini wakati huohuo wanauona urais wa Tanzania Bara kwamba hauna mamlaka kamili ya kuwawezesha watambuliwe nje ya nchi.

Tume ya Marekebisho ya Katiba imependekeza mambo saba tu yawemo chini ya Serikali ya Muungano kati ya 22 ya sasa. Yanayopendekezwa ni Ulinzi na Usalama, Katiba na mamlaka ya Jamhuri ya Muungano, mambo ya nje, sarafu na Benki Kuu, uraia na uhamiaji, usajili wa vyama vya siasa, ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na Muungano.

Ndani ya CCM


Makundi mbalimbali yanayowania urais ndani ya CCM inaaminika hayajafurahishwa na mapendekezo ya rasimu ya kutaka Serikali tatu.


Kwa maneno mengine, wanaona kama Rais wa Muungano ameng’olewa baadhi ya meno na masuala mengi yatakuwa yanashughulikiwa na Serikali ya Tanzania Bara na ile ya Zanzibar.

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amesema Tume ya Mabadiliko ya Katiba imeliacha hewani suala la Tanganyika hasa baada ya kutoa mapendekezo ya Serikali tatu kwenye Rasimu ya Katiba.


Sitta ambaye ni Mbunge wa Urambo Mashariki (CCM), alisema hakuna mantiki ya kuunda Serikali tatu ikiwa Tume haikutoa mwongozo wa hali itakavyokuwa kwa Tanzania Bara, Serikali ya Muungano na ile ya Zanzibar.

“Ukiangalia kwa haraka, hivi Serikali ya Tanganyika itakuwaje? Bunge la Tanganyika litakuwa la namna gani na utaratibu gani utatumika kupata wabunge?” alisema Sitta kwenye Viwanja vya Bunge, Dodoma jana.
Pia, Sitta aliyewahi kujipambanua kuwa atawania urais 2015 na hata kutaja kundi la muungano wa marafiki zake, alisema Tume pia haikuweka wazi utawala utakavyokuwa ndani ya Serikali tatu.

“Hivi viongozi wa Tanzania Bara na Zanzibar na wao wataitwa marais! Wapi duniani imeshatokea nchi moja ikawa na marais watatu? Hii haijawahi kutokea, na Tume inatakiwa kuweka sawa katika uongozi hasa ngazi ya Rais wa kuongoza hapa,” alisema Sitta.
Alipinga mpango uliopendekezwa wa wabunge kuchaguliwa wawiliwawili akionya kuwa utasababisha matatizo kwa kuwa Tume haijaweka wazi njia za kuwapata.

MwanaCCM mwingine ambaye ni miongoni mwa watu wanaotajwatajwa kuwania urais 2015 alikaririwa akisema: “Hivi kweli Mzee Warioba kweli anataka kututengenezea Mikhail Gorbachev (Rais wa zamani wa Urusi) hapa Tanzania? Hatutakubali!” Alikuwa akimfananisha Rais ajaye, ambaye atatokana na rasimu hiyo na Rais wa zamani wa Urusi, Gorbachev, ambaye mwaka 1991 alipoteza mamlaka yake baada ya kutoa madaraka ya ndani kwa nchi 14 zilizokuwa zinaundwa Muungano na baadaye zikajitangazia uhuru jambo ambalo kiongozi huyo alishindwa kulizua.
Pia watu wa karibu na mgombea huyo wanaamini kuwa kukubaliana na pendekezo la Serikali tatu ni sawa na kuvunja Muungano.

“Tunatakiwa kwenda Serikali moja na siyo kurudi Serikali tatu ukizingatia sasa ni miaka 50 tangu Tanganyika na Zanzibar ziungane. Hatuungi mkono suala hili kwani haliutakii mema Muungano.”

Katika siku za karibuni, joto la kuwania urais wa Tanzania lilianza kupamba moto baada ya kuibuka habari kuwa suala la kuwania urais lilijadiliwa wakati Rais Kikwete alipokutana na wabunge wa CCM.

Habari za ndani kutoka katika mkutano huo zilieleza kuwa Rais Kikwete alishauri kuwa haikuwa dhambi kujipanga kuwania urais mwaka 2015 lakini alionya kufanya hivyo kusiathiri umoja wa CCM.

Mtu mwingine, ambaye yuko karibu na kati ya watu wanaotamani urais kupitia CCM, alisema: “Hii rasimu ngumu, ila tukiona mambo siyo mazuri kwenye Muungano tutajitosa kwenye uchaguzi wa Rais wa Tanzania Bara.”
Chadema
Rasimu pia imegusa harakati za kuwania urais kupitia Chadema hasa ikizingatiwa kwamba mmoja wa makada wake, Zitto Kabwe alishatangaza dhamira yake mapema.
Kama rasimu hiyo itapitishwa na kuwa Katiba, Zitto atajikuta anakwama kwani imependekezwa miaka ya kugombea urais ianzie 40.

“Ila watu wengi wanafikiri Zitto amekwama ila jamani kuna Katiba ya Tanzania Bara inaweza kuwa tofauti na umri kuwa chini zaidi,” alieleza mtu wa karibu na Zitto.
Bila shaka hali hiyo itakuwa heri kwa wale wanaomuunga mkono Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa ambaye alikuwa anatarajiwa kukabiliana na Zitto kuwania tiketi ya kugombea urais kupitia chama hicho.
Wabunge wapinga

Mbunge Peter Serukamba, Kigoma Mjini (CCM) ameonya kuwa kubadili muundo wa Serikali ni gharama kubwa na kuhoji kutakuwa na marais wangapi?
“Muundo mzima ni gharama na tutatumia hadi fedha za maendeleo ya wananchi kuendesha Serikali ya Katiba mpya. Mimi binafsi napingana na hili, nataka Serikali mbili,” alisema.
Kwa upande wake, Maua Daftari, Viti Maalumu (CCM) alisema mfumo wa Serikali tatu uliopendekezwa ukipita itakuwa hasara kubwa kwa Wazanzibari.

“Kwa mtazamo wangu, kwa Zanzibar bado sana kuweza kusimama kwa miguu yake na wakati huohuo kuchangia katika Serikali ya Muungano,” alisema Daftari, ambaye amewahi kuwa Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi kwenye Serikali ya Muungano.
Mbunge mwingine kutoka Zanzibar, Mariam Msabaha, Viti Maalumu, (Chadema), alisema chuki za watu na uroho wa madaraka kwa watu wachache unaweza kuwa ndiyo sababu ya kupendekezwa kwa mfumo huo.
                                           HABARI NA GAZETI LA MWANANCHI

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate