EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, June 12, 2013

Watanzania hatarini kupata mabusha, matende

IMEELEZWA kwamba Watanzania wote wapo kwenye hatari ya kupata maambukizi ya mabusha na matende.

Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam jana na Dk. Edward Kirumbi wakati wa semina kwa wahariri na waandishi wa habari kuhusu uelewa wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.

Katika semina hiyo pia wataalamu wa magonjwa hayo walisema wakazi wa majiji ya Mwanza na Dar es Salaam watapewa dawa za magonjwa hayo kwa siku tano mfululizo kuanzia Juni 22, mwaka huu.

Aliyataja baadhi ya magonjwa sugu yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kuwa ni mabusha na matende, minyoo, kichocho, usubi, trakoma na kichaa cha mbwa ambayo husababisha ulemavu wa kudumu.

Dk. Kirumbi alisema maradhi hayo huenezwa na mbu aina ya Anopheles na Curex ambao hubeba vimelea vya minyoo hivyo kuwaweka Watanzania wote kwenye hatari hiyo bila kujali umri.

“Mbu anayekuambukiza malaria anaweza kukuambukiza mabusha au matende kwa sababu yanaambukizwa kwa minyoo midogo midogo iliyopo kwenye mfumo wa majimaji na damu,” alisema na kuongeza watu zaidi ya bilioni moja wapo kwenye hatari ya kuambukizwa magonjwa hayo.

Awali, Dk. Upendo Mwingira, alisema Watanzania milioni 2.5 wapo kwenye hatari ya kupata maambukizi ya trakoma huku akisisitiza kwamba magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele yapo zaidi kwenye jamii maskini.

“Kwa vile yapo kwenye jamii maskini zaidi kwenye ukanda wa tropiki, mgonjwa hana sauti, yanaathiri ukuaji wa mtoto kiakili, yanazorotesha shughuli za maendeleo na kuzidisha umaskini,” alisema.

Kwa mujibu wa Dk. Upendo ambaye pia ni Mratibu wa Mpango wa Taifa wa kutokomeza magonjwa hayo (NTDCP) wamezifikia halmashauri 97 ambazo huzipatia dawa kila mwaka.
“Tunao mpango wa kwenda kwenye halmashauri nyingine kwa kuongeza majiji ya Dar es Salaam na Mwanza kwenye mpango wetu wa kugawa dawa mara moja kila mwaka hivyo tunaamini tutazifikia halmashauri zaidi ya 105,” alisisitiza.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate