EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, June 12, 2013

Polisi wadaiwa kuuza silaha kwa Al-Shabab.

 Habari na Tanzania Daima.
SIKU mbili baada ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara, kuwapandisha kizimbani askari wake wawili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mara kwa tuhuma za wizi wa risasi, siri nzito imefichuliwa.

Juzi askari, Michael Leus (55), Sajenti wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) katika kituo cha Polisi cha Musoma na Ally Majembe Koplo wa kituo cha polisi wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani walifikishwa kizimbani kujibu mashtaka yanayowakabili.

Mwendesha mashkata, Jonathan Kaijage mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Ngikwama alidai kuwa askari hao walikutwa na risasi 1556 za SMG na Shortgun.
Kosa jingine walilokutwa nalo ni wizi wakiwa kazini ambapo walikana mashtaka hayo yote mahakamani hapo.

Hata hivyo kwa mujibu wa chanzo chetu, inadaiwa kuwa mtandao huo wa askari ni mkubwa na kwamba silaha hizo na risasi zinazoibiwa zinasafirishwa hadi mpakani mwa Kenya na Tanzania na kuuzwa kwa wapiganaji wa kundi la waasi la Al-Shabab la nchini Somalia.

Kundi la Al-Shabab limekuwa tishio nchini Somalia kwa matukio ya mashambulizi ya kuuwa watu na kufikia hatua ya kuvuka mpaka hadi Kenya, hatua iliyoilazimu nchi hiyo kupeleka jeshi lake Somalia kupambana na kundi hilo.

Wakizungumza kwa simu na Tanzania Daima Jumatano kwa sharti la kutotajwa majina yao gazetini ili kulinda ajira zao, watoa siri hao walisema kuwa biashara hiyo haramu waliyoifananisha na uasi ndani ya jeshi hilo iliripotiwa mapema lakini hakuna hatua zilizochukuliwa.

“Hii biashara inawahusisha watu wazito maana tangu imeripotiwa hakuna hatua zilizochukuliwa na wahusika wamekuwa wakiendelea kuvusha silaha hizo hadi walipokuja kunaswa baadhi yao.

“Hali sasa ni tete kwa wale waliotoa siri hiyo kwani mtandao huo umeanza kuwapa vitisho vya kuwaua ili wasije kufichua mpango mzima wa ushahidi dhidi yao,” walisema.
Hata hivyo, watoa taarifa hao walitilia shaka kuwa huenda wakubwa wao wanafahamu mpango mzima na hivyo kumuomba Mkuu wa Jeshi hilo, Inspekta Jenerali (IGP), Saidi Mwema, kuunda tume ya kuchunguza kashfa hiyo na kuliepusha taifa lisivamiwe na maadui.

Alipotafutwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Absalom Mwakyoma, kulitolea ufafanuzi suala hilo, alikataa kata kata akisema liko mahakamani na hivyo haruhusiwi kulizungumzia.
Alipoulizwa kama ana taarifa za vitisho vya baadhi ya askari wake waliofichua siri hiyo, Kamanda Mwakyoma alisema waripoti malalamiko hayo polisi ili yafanyiwe uchunguzi.

Katika kesi inayowakabiri askari wawili kwa tuhuma za kuiba risasi na silaha, mwendesha mashtaka aliielezea mahakama hiyo kuwa walikutwa na risasi hizo katika upekuzi wa ndani ya basi la Mohamed Trans usiku wa Juni mosi mwaka huu. Kesi hiyo iliahirishwa hadi Juni 24.
                      CHANZO CHA HABARI NA TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate