EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, July 21, 2013

Mkutano Simba balaa..

Dar es Salaam. 
Mwenyekiti wa Simba, Aden Rage jana alitoka nje ya Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oyesterbay chini ya ulinzi mkali baada ya kumalizika kwa mkutano wa klabu hiyo, ambao wanachama walishindwa kujadili kwa kina ajenda kutokana na vurugu na zomeazoea.
 

Rage na Mzee Kinesi

Ibrahim Masoud Maestro na mwenyekiti wa kamati ya usajili Zakaria Hans Pope
Kabla hata ya kufanyika mkutano huo, tayari kulikuwa na makundi ya wanachama wakiupinga na ndiyo hao ambao walitumia fursa ya kushiriki kwao kwenye mkutano kumzomea Mwenyekiti Aden Rage.
Mwenyekiti Rage alijikuta kwenye wakati mgumu kutokana na baadhi ya wanachama kumzomea wakati akiwasomea maelezo ya mikakati na maendeleo ya klabu hiyo, ingawa mwishoni alifanikiwa kuwatuliza baadhi ya waliompinga.

Kasheshe ya kuzomea-zomea iliendelea hata baada ya kuitwa mbele Mkuu wa Chuo Kikuu Huria, Tolly Mbwete kuzindua mpango mkakati wa maendeleo ya klabu hiyo.

Wakati Mbwete (Profesa) akisoma maelezo ya mkakati huo, baadhi ya mashabiki walisikika wakisema; “Hatutaki...hatutaki...toka, hatutaki kusikia habari ya Chuo Kikuu, tunataka matokeo mazuri uwanjani huo mkakati wenu hautusaidii.”

Pamoja na kuzomewa, Rage alimtaka Mbwete kuendelea kusoma maelezo ya mkakati huo huku kelele zikiongezeka kutoka kwa wanachama wengi, hali iliyowafanya wengine kushindwa kusikiliza kilichokuwa kikiongelewa.
     Mwenyekiti aliyepita wa Simba Hassan Dalali alikuwa mmoja wa wahudhuriaji

Kama mwendelezo wa kupinga kilichokuwa kikiongelewa, baadhi ya wanachama waliondoka kwenye mkutano huo uliokuwa chini ya ulinzi wa askari zaidi ya 70.
Baada ya mambo kwenda vibaya, Rage aliwataka polisi kuwakamata wanachama waliokuwa wakifanya fujo ikiwa ni pamoja na kuwatishia kuwafuta uwanachama, jambo lililoibua zogo zaidi.

“Hatoki mtu hapa...tupo tayari kufa lakini hapa hatoki mtu...unatuburuza, hatukutaki...tumekuchoka ondoka,” wanachama walipaza sauti.

Mkutano huo, uliofunguliwa saa 3 asubuhi na kuhudhuriwa na wanachama 712 kati ya 1516 ambao ni hai, na wanachama hao walishindwa kuchangia kikamilifu ajenda hali iliyopelekea mambo mengi kupitishwa kienyeji.

Kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, Simba ilipata kipigo cha mabao 2-1 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya timu ya URA kutoka Uganda.
Simba walikuwa wa kwanza kufunga bao katika dakika ya saba likifungwa na Betram Mombeki. URA walisawazisha kupitia kwa Lutimba Yayo dakika 60, na kisha akafunga bao la ushindi dakika ya 76.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate