EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, July 31, 2013

Rasimu ya Katiba mpya haimtaji mkulima.

Kadri mjadala wa Rasimu ya Katiba unavyozidi kupamba moto, wanasiasa wanazidi kubaini ufinyu wa nafasi zao iwapo rasimu hiyo itapita bila mabadiliko, hivyo kulazimika kuibua vihoja na mambo ambayo hawataki yawemo wakidhani kuwa yanaweza kuwaathiri.

Mada kuu katika rasimu iliyotolewa na Tume ya Jaji Joseph Warioba inayoleta hofu kwa wengi ni muundo wa Muungano wa Serikali tatu. Muundo huu ndiyo unaotoa taswira ya hali ya kisiasa hapa nchini hapo baadaye, iwapo Katiba Mpya itapitishwa.

Miongoni mwa wanasiasa waliotikisika ni wanasiasa kutoka Zanzibar, hasa kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), na hata wenzao wa bara ambao wameonyesha kila dalili za woga wa kupoteza madaraka.

Chama hicho kimeamua kutoa waraka wa ‘kuichana’ Rasimu ya Katiba, kikipinga Serikali tatu na mambo mengine mengi yanayopendekezwa.
Wanasiasa wenye mwelekeo huo wamejificha katika kivuli cha ‘gharama kubwa za uendeshaji wa Serikali tatu’.

Kwa mfano, Samuel Sitta, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki anasema haijawahi kuwapo nchi yoyote duniani yenye marais watatu kama inayopendekezwa, kana kwamba ilishawahi kuwapo nchi yenye marais wawili kama iliyopo sasa, Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Zanzibar katika nchi moja.

Deus Kibamba, Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba, anawashauri wanasiasa wanaopinga Serikali tatu kwa kigezo cha gharama kutafuta hoja nyingine, kwa maelezo kuwa hicho ni kihoja.

“Mimi nadhani Serikali tatu zitapunguza gharama. Ukiangalia ukubwa wa Serikali ya sasa ya mawaziri 60 ukalinganisha na Serikali inayopendekezwa ya mawaziri wasiozidi 15; wabunge wa muungano 75, ukiongeza wale wa Zanzibar na Tanzania bara, jumla yao haitaweza kufika ya sasa ya 357 (ukiondoa watatu ambao Rais Jakaya Kikwete hajateua). Hivyo gharama zitapunguzwa,” anasema.

Kibamba ambaye alikuwa anazungumza na Muungano wa Vikundi vya Wakulima (Mviwata) ambao wamejiunga kama Baraza la Katiba, anasema kwa jumla, pamoja na upungufu kadhaa yaliyomo, Rasimu ya Katiba ina mambo mengi mazuri.

Hata hivyo, anasema Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoandaa Rasimu hiyo imevunja Katiba kwa kupendekeza kupunguza mambo ya Muungano kutoka 11 yaliyofikiwa mwaka 1964 hadi saba.

Rasimu hiyo ya Katiba imependekeza mambo ya Muungano yawe saba – Katiba na mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Uraia na Uhamiaji,  Sarafu na Benki Kuu, Mambo ya Nje, Usajili wa Vyama vya Siasa, Ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na mambo ya Muungano.

Hata hivyo, Katiba ya sasa ina mambo ya Muungano 22 baada ya kuongezwa kwa nyakati tofauti kutoka 11, hatua ambayo imekuwa ikilalamikiwa na Wazanzibari wengine.

Nafasi ya mkulima
Vilevile Kibamba anasema kama ambavyo mkulima amekuwa akipuuuzwa kwa namna mbalimbali, hata Rasimu ya Katiba inayojadiliwa haijarejesha umiliki wa nchi, mikononi mwake, baada ya kile kifungu cha
“Tanzania ni nchi ya Wakulima na Wafanyakazi” kuondolewa katika Katiba ya mwaka 1961.

 “Rasimu hii haielezi nchi hii ni ya akina nani, pamoja na kutoeleza, mimi nadhani nchi hii kwa sasa ni ya wafanyabiashara na wawekezaji,” anasema Kibamba.
Pamoja na kuikosoa rasimu hiyo, Kibamba anasema walau imeonyesha kuwa inaandaliwa kwa kuwashirikisha wananchi, wakiwamo wakulima na wafanyakazi, na maandalizi yake yanafuata utaratibu wa kisheria, hivyo Katiba itakayopatikana itakuwa halali.

“Katiba tano za mwaka 1961, 1962, 1964, 1965 na ya sasa ya 1977 zilikosa uhalali kwa sababu hazikuwasirikisha wananchi, wananchi walitakiwa wajifunze katiba baada ya kupitishwa,” anasema.
Anabainisha kuwa mawazo ya wakulima hao ni muhimu ili haki zao ziweze kuingizwa, badala ya sasa ambazo ‘zimechomekwa’ katika makundi madogo wakati wenyewe ndio kundi kubwa.

Kwa mujibu wa Kibamba, wakulima hao wapiganie ardhi, rasilimali na misitu ambayo ni mambo muhimu kwa wakulima, ili yaweze kuingizwa katika rasimu, badala ya kuishia kuyaona kama mambo ambayo si ya Muungano.

Ushauri wa Sumaye
Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye anawataka kutumia wingi wao na baraza lao la katiba kuingiza mambo yenye masilahi yao kwenye Katiba ijayo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate