EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, August 10, 2013

Bongo Movie wanatamba kimuziki

KATIKA kujiongezea kipato zaidi au kulinda umaarufu wao usipotee katika jamii, baadhi ya wasanii wa filamu hapa  Bongo  wamejikita katika fani nyingine ya muziki.

 
Baby Madaha msanii aliyeibukia kutoka mashindano ya BSS na kuwa moja kati ya waigizaji wanaofanya vizuri katika fani zote mbili yaani muziki na filamu, kaigiza filamu za ‘Ray Of Hope’, ‘Nani’, ‘Desperado’ na nyinginezo.

Wasanii waliofanya hivyo ni wengi, japo si wote walioweza kushika chati ya muziki kwa umahiri.


Lakini wasanii wa filamu ambao wameingia katika uimbaji wamefanikiwa tofauti na wasanii wa muziki walioingia katika filamu. Jambo hilo linatoa mwanya kwa waigizaji kuamini kuwa wanaweza kuteka soko la muziki pia.

Wasanii wa filamu wanaoimba wameanza muda kidogo, wa kwanza kuingia katika muziki alikuwa Jackson Makwaya ‘Bambo’ ambaye alivuma na wimbo ‘Kitambi’.


Bambo alifanya hivyo baada ya kuwa nyota katika uigizaji kupitia kundi la Kaole Sanaa. Baadaye swahiba wake, Rashid Mwinshehe ‘Kingwendu’ naye akafuata nyayo.


Ukifuatilia kwa undani utagundua kuwa wasanii wengine wa filamu ambao wamekuwa wakifanya muziki, wanafanya hivyo kama kwa ‘kubipu’ kwani bado wanang’ang’ania filamu zao.


Tena wanaofanya hivyo ni Wachekeshaji (makomedi) ambao ni Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’, Hamis Mshangani ‘Mtanga’, Lucas Mhuvile ‘Joti’, Asha Boko, Gilliady Kahena ‘Masai Nyota Mbofu’, Makwaya ‘Bambo’, Martin Tin White, Maulid Ali ‘Mau Maufundi,’Alex Machejo ‘Bingwa wa Rivasi’ na Mwinshehe ‘Kingwendu’.


Wengine ni Isaya Mwakilasa ‘Wakuvanga’, Mohamed Abdalah James ‘Kinyambe’ na Silvester Mjuni ‘Mpoki’ ambaye wimbo wake ‘Sangazi’ umeshinda tuzo za Kilimanjaro.

Baby Madaha msanii aliyeibukia kutoka mashindano ya BSS na kuwa moja kati ya waigizaji wanaofanya vizuri katika fani zote mbili yaani muziki na filamu, kaigiza filamu za ‘Ray Of Hope’, ‘Nani’, ‘Desperado’ na nyinginezo.


Kati yao, wasanii ambao nyimbo zao zilishika chati ni Sharo Milionea (marehemu sasa). Aling’ara na nyimbo zake kama vile ‘Changanya Changanya’ na ‘Chuki Bure’.


Pia mchekeshaji Masanja Mkandamizaji naye anatamba kwa kuimba nyimbo za Injili na kuendelea kutesa katika fani ya uimbaji.


Albamu ya Isiah Mwakilasa ‘Wakuvanga’ inaitwa Kato na ina nyimbo nane, msanii huyo ni mmoja kati ya wanaounda kundi la Orijino Komedi.

Yeye pamoja na kutoa albamu, pia ameweza kutoa ajira kwa vijana wanaotembeza kuuza albamu hiyo kwa wananchi.

Marehemu Sharo Milionea baada ya kufanya vema katika uchekeshaji na kushiriki katika filamu ya Safari za Adili,  aliibuka na kutesa katika muziki hadi mauti yalipomkuta.
Wasanii wengine wa filamu wanaoimba ni pamoja na Simon Mwakipagata ‘Rado’, Rose Ndauka, Aunty Ezekiel, Dokii na  Mzee Mgari ambaye kaibuka hivi karibuni na wimbo ‘Dar Raha’.

Masanja Mkandamizaji yeye alitoa albamu ya Hakuna Jipya akiimba Injili na kufanikiwa kuwateka wapenzi wa muziki huo.

Mwigizaji mwingine anayeimba akitokea katika kundi la Scopion Girl ni Miliam Jolwa ‘Jini Kabula’. Msanii huyu akiwa na kundi hilo, alifanikiwa kurekodi wimbo wa ‘Mapenzi Nini’.
Dokii ambaye ni mwigizaji na mtayarishaji, ameigiza filamu nyingi kama vile ‘My Nephew’, ‘Money Transfer’ na ‘Sister wa Bush’, yeye alitumia ziara ya Rais wa Marekeni, Barrack Obama, nchini Tanzania kutoa kibao.

Wimbo huo ‘Welcome Obama’ ulipata chati kubwa wakati wa ziara hiyo hivi karibuni.
Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ameshiriki filamu kama ‘Tifu la Mwaka’, ‘Zawadi’ na nyinginezo na hakuna aliyeamini kama anaweza kutamba katika muziki pia.

Lakini majibu yamepatikana baada ya kuimba nyimbo za ‘Lawama’, ‘Dume Dada’, ‘Paka La Bar’ na ule wa ‘Nakomaa na Jiji’.

Msanii Snura Anton Mushi kaigiza filamu za ‘Hitimisho’, ‘Mfalme Seuta’, ‘Zinduna’ na nyinginezo, katika muziki pia ametamba na kibao cha ‘Shoga Yake Mama’ na sasa anatamba na wimbo ‘Majanga’.

Lakini hali ni tofauti kwa wasanii wa muziki walioingia katika filamu. Ni Hemed Suleiman pekee tu ndiye angalau ameweza kufanya vizuri. Hemed ameshiriki filamu nyingi na kuwa pacha wa msanii Yusuf Mlela.
Wasanii wa muziki waliowahi kuigiza ni Chege na Mh.Temba ambao wameshiriki katika filamu za ‘Dar Moro’ na ‘Papaa’.

Akina GK, AY, Juma Mchopa ‘Jay Mo’ waliwahi kuigiza katika filamu ya Girlfriend, marehemu Albert Mangwea na Dark Master nao walishiriki filamu ya Copy.
Pia kuna akina Izzo Business, Dully Skyes, Queen Darlin, Linah nao wameshiriki katika uigizaji, lakini bado hawajateka tasnia hiyo ya filamu.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate