EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, August 15, 2013

Sheikh Ponda Issa Ponda (54), amesomewa shtaka akiwa kitandani.

KATIBU wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda (54), amesomewa shtaka akiwa kitandani katika Kitengo cha Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu (MOI).

Katika shtaka hilo, Ponda anadaiwa kuwahamasisha wafuasi wake kufanya kosa.
Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Hellen Riwa, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Tumaini Kweka, alidai kuwa uhamasishaji huo ulifanyika sehemu mbalimbali nchini kuanzia Juni 2 hadi Agosti 11 mwaka huu.

Kweka alidai kuwa kosa hilo ni kinyume cha sheria ya makosa ya jinai kifungu 390 na 35 ya kanuni za adhabu.

Kutokana na shtaka hilo, Hakimu Riwa aliahirisha kesi hadi Agosti 28 na kutoa agizo 
Sheikh Ponda aendelee kuwa chini ya uangalizi wa vyombo vya dola wakati akiendelea na matibabu.

Baada ya Hakimu Riwa kuahirisha kesi, wakili wa mshtakiwa Nasoro Jumaa, alilaumu utaratibu uliotumika na kusema kuwa mahakama imefanya kazi nje ya muda wa kawaida wa saa za kazi za kiserikali.

Alisema mawasiliano ya awali ilikuwa askari na Tume ya Haki Jinai ya Jeshi la Polisi kufika hospitalini hapo kwa ajili ya kufanya mahojiano na Sheikh Ponda.

Aliongeza kuwa baada ya maofisa hao kufika hali ya Sheikh Ponda haikuruhusu mahojiano kufanyika na ilipofika saa kumi jioni kila mmoja alitawanyika.
Jumaa alisema kuwa wakiwa wanakaribia geti la kutokea Muhimbili, walipigiwa simu kuwa Sheikh Ponda anasomewa mashtaka, hatua aliyodai kuwa iliwashangaza.

“Kama walikuwa na dhamira ya kumsomea mashtaka wangetuambia, kwa kuwa ni haki ya msingi kwa mtuhumiwa kuwa na mwanasheria wake kwa ajili ya kujua taratibu zilizotumika,” alisema.

Alisisitiza kuwa baada ya kupata hati ya mashtaka wanajiandaa kupinga kosa hilo kwa kile alichoeleza kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina uwezo wa kusikiliza kosa la aina hiyo.

Aliongeza kuwa kabla ya kufikiwa kwa hatua ya kumsomea shtaka Sheikh Ponda, walishaandika barua ya kutokuwa na imani na Tume ya Haki Jinai ya Jeshi la Polisi katika uchunguzi wao kwa kile alichoeleza kuwa ni watuhumiwa wa kwanza katika tukio la kujeruhiwa kwa mteja wake.

Awali kabla ya kesi hiyo kusomwa maeneo mbalimbali ya Hospitali ya Muhimbili hususan jirani na jengo alilolazwa Sheikh Ponda, yalikuwa yamezingirwa na makachero wa polisi wakiwa na magari matano ya Kikosi cha Kutuliza Ghasia.

Magari mawili yenye namba PT 2072 na PT 2061 yalikuwa jirani na mlango wa kuingilia katika kitengo cha mifupa huku askari wakiwazuia wananchi wasiende kumuona Ponda kwa kile walichoeleza kuwa kuna shughuli za kiserikali zinaendelea.
Miongoni mwa watu waliozuiwa ni wakili maarufu nchini, Profesa Abdallah Safari.
Credit: Tanzania Daima.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate