EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, October 9, 2013

Magomeni Kota waionya Manispaa Kinondoni.

WAKAZI wa zamani wa Magomeni Kota wameionya Manispaa ya Kinondoni, kuhakikisha inawalipa fedha zao za pango kama mkataba ulivyo, vinginevyo watazua vurugu kubwa.

Onyo hilo linafuatia kuwapo kwa sintofahau kuhusu malipo hayo, huku mmoja wa watendaji wa manispaa hiyo (jina limehifadhiwa) akikiri kuwa hakuna uwezekano wa kufanyika malipo hayo.

Ofisa huyo alisema viongozi wa manispaa waliosaini mkataba wa malipo hayo, wakazi hao waliwadanganya, kwa kuwa jambo hilo haliwezi kutekelezwa kwa kuwa ni kuvunja sheria.

Alisema kuwa viongozi wa juu wa manispaa hiyo wana hofu kufanya malipo hayo ya sh 695,520,000 ikiwa ni pango la kodi kwa wakazi hao linaloanzia Januari hadi Desemba mwaka huu kutokana na uwezekano wa kuingia katika kashfa, kwa kuwa sheria haikuzingatiwa tangu awali.

“Hapa ninapokuambia viongozi wote wana hofu ya kutoa fedha hizo, ingawa mkataba unaonesha kusainiwa na baadhi ya viongozi wa manispaa lakini wanajua wazi ukaguzi wa 

Mdhibiti na Makaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ukifanywa kuna utata utajitokeza iwapo fedha hizo zitatumika,” alisema.

Alisema kuwa hofu hiyo ndiyo iliyosababisha baraza la madiwani na baadhi ya viongozi wa juu kuzuia malipo hayo kufanyika ingawa wanashindwa kuwaeleza ukweli wakazi hao.

Alisema kuwa ni kitendo cha ajabu wanasiasa wa manispaa hiyo walivyowadanganya wananchi hao kwa kuwa hakuna fedha ya walipa kodi inayotolewa pasipo kufanyiwa kazi.

Akizungumzia juu ya malipo hayo, kiongozi wa kamati ya wakazi hao, Abbas Mkweta, alisema kuwa hadi sasa hawajapata taarifa rasmi za lini manispaa hiyo italipa malipo hayo.

Mkweta alisema kuwa wanategemea kati ya siku hizi mbili wapewe fedha hizo kwa kuwa uhakiki umefanyika kwa kiasi kikubwa na zilizobaki ni nyumba 15 tu.

“Sisi tunaamini tutalipwa fedha hizo lakini hadi sasa manispaa haijatueleza watatulipa lini ila tunawaomba wakazi wa Magomeni wawe na subira, najua kati ya siku hizi mbili ni lazima watupe taarifa za uhakika,” alisema.

Aidha, mmoja wa wakazi hao ambaye hakutaka kutajwa jina lake alisema kuwa wanaona kama mchezo wa kuigiza unaoendelea maana baadhi yao wametoka mbali kufuatilia malipo hayo huku wakiwa wamekopa nauli.

Mkazi huyo alisema kuwa manispaa ni lazima ithamini mkataba huo la sivyo wakazi hao watalazimika kutafuta mahema na kuja kufunga katika viwanja hivyo kutokana na wamiliki wa nyumba walizopanga kuwadai kodi ya mwaka mzima.

“Hivi ninavyokwambia wamiliki tulikopanga tumewadanganya hadi tumechoka na sasa imefika mahali wanataka hela zao, sasa kama manispaa inataka vurugu wajaribu kutufanyia jambo hilo la kugoma kutulipa hizo fedha,” alisema.

Halmashauri hiyo iliingia mkataba na wakazi hao Septemba mwaka 2011 katika Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi ambapo ilikubali kuwalipia pango la chumba wakazi hao kuanzia mwaka huu hadi pale nyumba za eneo hilo zitakapokamilika.

Nyumba za Magomeni Kota zilijengwa na Jiji la Dar es Salaam miaka ya 1950 na baadaye kumilikishwa kwa halmashauri ya manispaa hiyo.

Nyumba hizo zilipangishwa kwa mkataba kwa wakazi hadi mwaka 2006. Wakazi hao 644 waliendelea kukaa hapo hadi mwaka 2009 ambapo walitakiwa kuondolewa na wakakimbilia mahakamani.CHANZO CHA HABARI NI TANZANIA DAIMA.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate