EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, October 9, 2013

Magufuli asalimu amri...Mabasi yaruhusiwa kutopita mizani.

MGOMO mkubwa wa mabasi ya abiria umeitikisa nchi na kuilazimisha serikali kusitisha kwa muda amri yake ya kuwatoza asilimia tano wasafirishaji wanaozidisha uzito.

Idadi kubwa ya mabasi ya abiria yanayofanya safari ndani na nje ya nchi yaligoma jana katika miji mingi ya nchi na kusababisha taharuki kubwa kwa abiria waliokuwa wamekata tiketi kwa ajili ya safari.

Idadi kubwa ya abiria walipata wakati mgumu katika kituo kikuu cha mabasi jijini Dar es Salaam, Arusha na Moshi huku wasijue la kufanya.

Wafanyakazi wa mabasi mengi walikuwa wamesimama wakidai kuwa wamekatazwa na waajiri wao kuendelea na safari hadi watakapopewa maelekezo mengine.

Sakata hilo liliwalazimu viongozi wa Jeshi la Polisi kuwasili katika vituo hivyo na kuanza kuwasiliana na Wizara ya Ujenzi ambayo ilichukua muda mrefu kupata ufumbuzi.

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, alidai kuwa mgomo huo haukuwa halali kwa sababu wamiliki hao wa mabasi walikwisha kuingia mkataba na abiria kwa kuwauzia tiketi za kusafiria kwa siku ya jana, hivyo hawakupaswa kuwanyima haki yao ya kusafiri.

Mpinga alisema kitendo cha kutowasafirisha abiria hao ni sawa na kuvunja sheria.

Hata hivyo, baada ya Kamanda huyo kukutana na viongozi wa Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) na Chama cha Wamiliki wa Mabasi (Taboa), aliwataka wamiliki hao, hususan madereva kuwapeleka abiria hao kama tiketi zao zilivyokuwa zinaelekeza, huku akiagiza Sumatra kuwakamata wale wote watakaopinga kufanya hivyo na kuwanyang’anya leseni zao na hatua nyingine zichukuliwe dhidi yao.

Hata hivyo, amri hiyo iliongeza hasira, na kuzuka mvutano mkubwa uliozidisha taharuki miongoni mwa abiria.

Hali hiyo iliwafanya viongozi hao kuwasiliana tena na mamlaka za juu, na ndipo ilipokubaliwa kuyaruhusu mabasi yote kuondoka kwa masharti ya kutopimwa katika mizani.

Hata hivyo, mmoja wa viongozi wa Taboa, Severine Ngallo, alisema makubaliano yaliyofikiwa ya kusafirisha abiria yalikuwa ya muda, wakisubiri matokeo ya kikao ambacho kingefanyika jana kwa kuwakutanisha na viongozi wa serikali.

“Nawashauri abiria wasikate tiketi katika kipindi hiki kwani kuna uwezekano mgomo huo ukaendelea tena leo na siku nyingine endapo madai yetu ya kuondolewa tozo hiyo yatakataliwa,” alisema Ngallo.

Msemaji wa Wizara ya Ujenzi, Martin Ntemo, alisema wizara imekubali kukutana na wasafirishaji hao, lakini akakana kuwapo kwa makubaliano ya mabasi kupita katika mizani bila ya kupimwa.

Jijini Arusha, mabasi yote yaligoma kuondoka kituo kikubwa cha mabasi kwa zaidi ya saa tatu, katika mwendelezo wa mgomo huo.

Hali hiyo ilimlazimu  Kamanda wa  Polisi mkoani humo, Liberatus Sabasi, kuingilia kati na kuwataka madereva hao kutumia busara ya kuendelea kuwasafirisha abiria wao ambao walikuwa tayari wameshawakatia tiketi.

Alisema kuwa kila abiria anapopanga safari yake ana kusudi lake, hivyo kuvunja safari kwa sababu za mgomo si busara.

Madereva hao walikubali kuendelea na safari kama kawaida majira ya saa mbili asubuhi huku wakidai kuwa hawajui mahali pa kuwapeleka abiria hao kwani mgomo wao ni wa nchi nzima.

Mjini Moshi, mabasi yote yalisitisha safari zake kwa zaidi ya saa tano na kuasabisha hali ya taharuki kwa wasafiri katika kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi.
Hali ilikuwa mbaya zaidi katika kituo hicho kutokana na  idadi kubwa ya wasafiri waliokuwa wakisafiri kuelekea jijini Dar es Salaam na mikoa ya Mashariki kukwama huku wengi wao wakilazimika kusitisha safari na kurejea majumbani licha ya kuwa na tiketi kwa ajili ya safari.

Baadhi ya wasafiri walilaumu kauli ya Waziri John Magufuli, kuwaambia wasafirishaji kuegesha magari yao majumbani na si katika barabara.
Walisema kauli hiyo ilichochea hasira na si ya kistaarabu, kwa kuwa imeongeza msuguano kati ya wasafirishaji na serikali.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate