EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, October 8, 2013

TBL Yazindua mashindano ya mitindo na ubunifu nchini.

Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha Redd’s Original imezindua tamasha la mitindo na ubunifu kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu hapa nchini, litakalojulikana kama ‘Redd’s Uni-Fashion Bash’.

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika Dar es Salaam jana, Meneja Masoko wa TBL, Fimbo Butallah alisema,  tamasha hilo lenye lengo la kuinua vipaji vya wanafunzi katika tasnia ya mitindo, linatarajiwa kuanza mwezi huu na kumalizika mwezi ujao.

Meneja masoko wa TBL Fimbo Butallah akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam kwenye uzinduzi wa mashindano ya ubunifu na mitindo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu nchini ( Redd's Uni-Fashion Bash 2013) yatakayofanyika katika mikoa ya Dar Es Salaam,Mwanza,Iringa na Kilimanjaro.Kushoto ni Meneja mawasiliano na habari wa Tbl Edith Mushi.
*******
Butallah alisema, tamasha hilo kwa sasa litashirikisha vyuo vyote vya elimu ya juu vilivyopo katika Mikoa ya Dar es Salaam, Iringa, Kilimanjaro na Mwanza.

“Tunataka kuinua vipaji vya wanafunzi wa vyuo katika tasnia ya mitindo, kupitia maonyesho yakatakayofanywa na wanafunzi wa vyuo hivyo, hapa tunataka wale wenye ubunifu kuonyesha ubunifu wao wa mitindo, hivyo hii ni fursa kwao kujitangaza na kudhihirisha uwezo wao,” alisema Butallah.
Kuhusu ushiriki, Butallah alisema, kutakuwa na fomu maalumu zitakazosambazwa katika vyuo husika, ambapo wanafunzi wanamitindo na wabunifu watazijaza na majaji watazipitia na kupata wabunifu 10 na wanamitindo wa idadi hiyo kutoka kila mkoa, ambao watapata fursa ya kuonesha mavazi yao siku ya tamasha.

Kuhusu zawadi, Meneja Habari na Mawasiliano wa TBL, Edith Mushi alisema, kutakuwa na zawadi mbalimbali kutoka Redd’s Original, ambapo washindi watano wa ubunifu na idadi kama hiyo ya wanamitindo kutoka kila mkoa watajiondokea na fedha taslimu.

Edith alisema, kwa upande wa wabunifu mshindi wa kwanza ataondoka na Sh 700,000 wa pili Sh 500,000 watatu Sh 300,000 huku wa nne na watano kila mmoja akiondoka na Sh 100,000.

Kwa upande wa wanamitindo mshindi wa kwanza atajiondokea na Sh 500,000 wa pili Sh 400,000 wa tatu Sh 300,000 wakati wanne na watano wakipata Sh 100,000 kila mmoja.

“Tuna imani kubwa zawadi hizi zitaongeza chachu kwa wabunifu na wanamitindo kuendeleza fani hii ya mitindo. Lakini matamasha haya pia yatahusisha burudani za aina mbalimbali za kuvutia.

“Hii itakuwa sehemu muhimu ya kuwakutanisha wanafunzi wa vyuo na kada mbalimbali katika kufurahia na kubadilishana mawazo juu ya masuala ya ubunifu na mitindo, kwani kinywaji cha Redd’s Original kimekuwa mstari wa mbele katika kuendeleza tasnia ya urembo, ubunifu na mitindo hapa nchini,” alisema Edith.

Kinywaji cha Redd’s Original pia ndicho kinachodhamini shindano la Redd’s Miss Tanzania na kinazalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate