EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, October 7, 2013

Tundu Lissu amjibu Rais Jakaya Kikwete.

MNADHIMU wa kambi rasmi ya upinzani bungeni, Tundu Lissu, amesema kuwa watapima kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuhusu muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba, watakapokutana leo katika Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Lissu alisema kuwa Rais Kikwete katika hotuba yake kwa taifa juzi alisema kuwa suala hilo linazungumzika.

“Mimi ninataka kuona leo kwenye Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala liwepo suala hilo katika ratiba kati ya mambo yatakayojadiliwa tayari kwa ajili ya kurejesha muswada bungeni.

“Kama suala hilo halitakuwepo, basi hotuba ya rais itakuwa ni porojo za Magogoni (Ikulu). Rais asiposaini muswada huo ataonyesha nia nzuri aliyokuwa nayo, na hayo tuyaone katika ratiba ya kamati,” alisema.

Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA) na msemaji mkuu wa kambi hiyo kwa Wizara ya Katiba na Sheria, alieleza mshangao wake kwa Rais Kikwete kuhutubia taifa kwa habari za kuambiwa, kuelezwa na kufahamishwa bila yeye kujiridhisha.

Alisema kuwa rais alimtuhumu kwa kumuita “mzushi na muongo mtupu mwenye kauli za kinafiki, fitina na uzandiki wa hali ya juu”, lakini akahoji ni kwanini anawataka wapinzani wakae mezani wazungumze naye wakati ni waongo.

“Hoja zangu zilihusu Zanzibar kutokushirikishwa katika mchakato wa kuboresha muswada wa mabadiliko ya sheria, nilisema hakuna mdau hata mmoja au mtu binafsi aliyeonana na wajumbe wa kamati.

“Kwa upande wa bara kulikuwa na wadau 22, ukijumlisha na vyama vya siasa 22, hivyo bara peke yake tulisikiliza wadau 44. Je, fitina, uzandiki na uongo anauosema Kikwete upo wapi?” alihoji.

Lissu alitaja baadhi ya taasisi za bara walizokutana nazo kuwa ni Ongeza Elimu ya Juu, vyama vya siasa na watu binafsi mfano Jaji Mkuu mstaafu, Barnabas Samatta na Prof. Issah Shivji.

Alisema kuwa kwa Zanzibar walipewa ratiba ya kutembelea miradi ya Tasaf, ofisi ndogo ya Bunge na ofisi ya Makamu wa Rais, na kwamba walilalamika kubadilishiwa ratiba hiyo wakiwa Zanzibar.

“Tuliambiwa na Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah tungepewa fedha za kukaa Zanzibar hata kwa wiki nzima, na tulilipwa fedha nyingi tofauti na tunavyolipwa kwa utaratibu wa kawaida,” alisema.

Lissu alisema kuwa Kikwete aliwahakikishia Watanzania kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilishirikishwa, lakini Waziri wa Sheria wa Zanzibar alisema kuwa walipelekewa muswada na Mwanasheria Mkuu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Wiliam Lukuvi na kuwataka watoe maoni siku hiyo hiyo.

Kwamba Wazanzibari waliona mambo manne waliyopelekewa katika muswada wa mabadiliko ya sheria hayakuwa na shida wakasema sawa, lakini muswada uliopelekwa bungeni ulikuwa na mambo zaidi ya 11.

“Je, hapa kuna uzandiki? Unafiki uko wapi? Je, na waziri huyo wa Zanzibar naye ni mwongo?” alihoji.

Aliongeza kuwa Rais Kikwete katika hotuba yake alisema ‘ameambiwa’, ‘ameelezwa’ na ‘amefahamishwa’, maneno ambayo ameyatamka mara tisa, na hivyo kuhoji inakuwaje rais anahutubia taifa kwa maneno ya kuambiwa ambayo kisheria hayana nguvu?

“Rais ana uwezo wa kukataa muswada na ana mamlaka ya kukataa mambo ya kijinga yanayopitishwa na wabunge. Tunaomba asisaini muswada huo.

“Rais wetu afanye kama Obama aliyenukuliwa siku za hivi karibuni akisema wabunge wakipitisha mambo ambayo hayana tija kwa taifa hatasaini,” alisema.
Akizungumzia athari za haraka kama rais atasaini muswada huo, Lissu alisema nchi itapata katiba mbovu ya hovyo na matukio ya vurugu kama ya Zimbabwe na Kenya yatajitokeza Tanzania.

Alisema kuwa nchi hizo zilifikia hapo baada ya serikali kujidai inahodhi muswada wa katiba, ikijipendelea yenyewe badala ya kusikiliza wananchi waseme.
Kuhusu wadau ambao waliwasilisha majina halafu rais akateua kadiri alivyoona bila kuteua majina hayo, Lissu alisema hayo hayakuwa mawazo yake, bali waulizwe mwakilishi wa 

Baraza la Maaskofu Katoliki, Dk. Charles Kitima na Mchungaji Rohho wa CCT.
Kwa wawakilishi wa Shirikisho la Vyama Vya Wenye Ulemavu (Shivyawata), Lissu alidai kuwa walisema kuwa Alshaymar Kweygir, rais ndiye anajua alivyomteua kwani hawakumpendekeza.
CHANZO CHA HABARI NA TANZANIA DAIMA.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate