EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, October 7, 2013

YANGA JANA WALIENDELEZA WIMBI LA USHINDI BAADA YA KUICHAPA MTIBWA SUGAR MABAO 2 - 0.

MABINGWA wa soka Tanzania Bara, Yanga jana waliendeleza wimbi la ushindi baada ya kuichapa Mtibwa Sugar ya Manungu, Turiani, Morogoro kwa mabao 2-0.
 ...dakika sita tu kuanza kucheza na nyavu kwa bao la Mrisho Ngasa
Kwa matokeo hayo, Yanga wamefikisha pointi 12 baada ya kushuka dimbani mara saba na kuchupa hadi nafasi ya pili nyuma ya watani zao Simba wenye pointi 15.

Katika mechi hiyo ya Ligi Kuu ya Vodacom iliyopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, 
 Yanga iliwachukua dakika sita tu kuanza kucheza na nyavu kwa bao la Mrisho Ngasa akimalizia pasi safi ya Mrundi Didier Kavumbagu.
Kama haitoshi, dakika ya 20, Kavumbagu naye alimsalimia kipa wa Mtibwa Sugar, Hussein Sharrif kwa kupachika bao la pili akiitumia pasi ya Ngasa.

Mtibwa walijibu mapigo, lakini Vicent Barnabas alishindwa kuitendea haki pasi ya Ally Shomari dakika ya 23, wakati alipopiga nje mpira kwa kichwa, kabla ya dakika ya 33, Ngasa kubaki na Kipa Sharrif lakini shuti lake jepesi likadakwa.

Hadi mwamuzi Isihaka Shirikisho anapuliza filimbi kuashiria mapumziko matokeo yalikuwa 2-0.
Kipindi cha pili, Mtibwa ilizinduka hasa baada ya kufanya mabadiliko kadhaa, lakini bahati haikuwa yao.

Awali kabla ya kuanza kwa mchezo, Yanga walizuia Azam TV kurusha mechi yao hiyo ya nyumbani kwa madai kuwa mazungumzo bado yanaendelea.

Azam TV walirejesha kamera zao dakika ya 40 na kuendelea na kazi, baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuingilia.

Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura, alisema walilazimika kuingilia kati, kwani suala hilo ni la kimkataba, hivyo mechi kuonyeshwa ni mali ya shirikisho hilo na Azam TV, wala sio klabu.
Yanga: Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite/Juma Abdul, David Luhende, Nadir Haroub ‘Canavaro’, Kelvin Yondani, Athumani Idd ‘Chuji’, Simon Msuva/Nizar Khalfan, Frank Domayo, Didier Kavumbagu, Mrisho Ngasa, Hamis Kiiza/Said Bahanuzi.
Mtibwa: Hussein Sharrif, Hassan Ramadhani, Paulo Ngalema, Salvatory Ntebe/Dickson Daudi, Salim Abdallah, Shabani Nditi, Ally Shomari, Awadh Juma, Mussa Hassan ‘Mgosi’, Shabani Kisiga, Vicent Barnabas/Masoud Mohamed.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate