EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, October 30, 2013

VIJANA WAPINGA KODI YA SIMU

Katibu Mkuu wa UVCCM, Sixtus Mapunda.
BARAZA Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) limeitaka Serikali kurejesha bungeni kwa hati ya dharura Muswada wa Marekebisho ya Tozo ya Sh 1,000 kwa laini za simu kwa mwezi.

UVCCM imesema ikiwa tozo hiyo itatekelezwa, itanyima Watanzania zaidi ya milioni nane haki ya msingi ya mawasiliano na huduma za kupokea na kutuma fedha kwa mtandao, jambo ambalo pamoja na kwamba lililenga kuongeza mapato, ni dhahiri litayashusha.
Sambamba na hilo, Baraza limempa Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza siku 21 kutoa kwa umma hatua anazochukua ili kuokoa wakulima wa korosho nchini dhidi ya unyonyaji, unaofanywa na walanguzi wa zao hilo.

Katibu Mkuu wa UVCCM, Sixtus Mapunda aliwaambia waandishi wa habari jana katika ofisi za Makao Makuu ya CCM mjini hapa kuwa maazimio hayo yalifikiwa na Baraza Kuu la Umoja huo katika kikao chake cha siku moja jana, chini ya Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Sadifa Juma Hamis.
Kwa mujibu wa Mapunda, katika kikao hicho walijadili migogoro ya wafugaji na hifadhi, taarifa ya utekelezaji wa tozo ya Sh 1,000 kwa laini za simu na masuala ya wakulima wa korosho.

Kuhusu tozo ya Sh 1,000, Mapunda alisema: “Baraza limejadili kwa kina na kubaini athari zinazoweza kutokea kutokana na tozo hiyo kwamba ni pamoja na ugumu wa ukusanyaji Sh bilioni 178 kwa mwezi katika bajeti ya mwaka 2013/14 ambao utaratibu wake unazorotesha na kurudisha nyuma juhudi za kisekta kuwezesha mawasiliano kwa wote.

“Lakini idadi kubwa ya wateja milioni nane ambao ni wa kipato cha chini watakosa huduma. Kushindwa kufikia watu wengi kwa huduma zaidi ya milioni nane kati ya idadi ya watumiaji milioni 26, ni dhahiri wakiondolewa kwenye mfumo wa mawasiliano, mapato yatashuka kwa watoa huduma na Serikali,” alisema Mapunda.

Kutokana hilo, alisema Baraza Kuu la UVCCM linaitaka Serikali kuzingatia mazungumzo ya Julai 23 ya Rais Jakaya Kikwete na watoa huduma za mawasiliano ya simu nchini baada ya Rais kukubali kuwapo ugumu wa utekelezaji wa hilo hasa namna ya ukusanyaji wa fedha na ukosefu wa mawasiliano kwa watu wenye kipato cha chini.

Kuhusu wakulima wa korosho, Mapunda alisema Baraza lilijadili changamoto za wakulima wa korosho nchini ikirejea uamuzi wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Mei mjini hapa kuhusu matatizo ikiwamo kuyumba kwa bei ya korosho, malipo kuchelewa, tozo nyingi na udhaifu wa baadhi ya vyama vya ushirika.

“Baraza Kuu limeamua kwa pamoja kuwa hali hiyo haivumiliki na wananchi wana haki ya kulalamikia matatizo hayo, pia limesikitishwa na kasi ndogo ya utekelezaji wa agizo la Kamati Kuu ya CCM la Mei lililoitaka Serikali iwaite wadau wote na kuchukua hatua mapema,” alisema Mapunda.

Alisema kutokana na hilo, Baraza Kuu linamtaka Waziri Chiza kufanya uamuzi wa dharura wa kushughulikia matatizo hayo katika kipindi cha siku 21 na kutoa kwa umma hatua alizochukua na atakazoendelea kuchukua kuokoa wakulima wa korosho na unyonyaji hasa wa bei kuyumba.

Mapunda alisema Baraza Kuu lilijadili migogoro ya wafugaji na hifadhi, hasa katika mikoa ya Shinyanga, Simiyu na Mara inayopakana na hifadhi ya Serengeti na mkoa wa Lindi, ambako wilaya zake za Kilwa na Liwale zinapakana na Hifadhi ya Selous kuwa kumekuwa na unyanyasaji mkubwa.

Alisema wafugaji na askari wa wanyamapori na wa kampuni ya uwekezaji ya Gurumeti, wamekuwa wakinyanyaswa na kutozwa kiwango cha Sh 50,000 hadi Sh 300,000 kwa ng’ombe mmoja bila stakabadhi na walitaka watendaji wa Serikali wasikae kimya wakati wananchi wananyanyaswa.
CHANZO NI HABARI LEO

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate