EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, October 28, 2013

Watu 20 wa familia moja hoi kwa kula chakula cha sumu.

Watu  20 wa familia moja akiwamo Ofisa Mtendaji wa kata katika kitongoji cha Igogo A kata ya Nyampurukano wilayani Sengerema, wamelazwa katika Hospitali Teule ya wilaya hiyo baada ya kula chakula kinachohofiwa kuwa na sumu.
Mbunge wa Sengerema (CCM), William Ngeleja.

Watu hao wanadaiwa kula chakula hicho cha usiku Oktoba 23, mwaka huu.

Imeelezwa kwamba mara baada ya kula chakula hicho, walianza kusikia maumivu makali ya tumbo na kulazimika kukimbizwa hospitalini kwa uchunguzi na matibabu.
Aidha, baba wa familia hiyo amelazwa katika chumba cha uangalizi maalum (ICU) kutokana na hali yake kuwa mbaya zaidi.

Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Mary Jose, alithibitisha kulazwa hospitalini hapo kwa watu hao tangu Alhamisi iliyopita kwa hofu ya kula chakula chenye sumu.
Hata hivyo, Dk. Jose alisema aina ya sumu iyohofiwa kuliwa na watu hao, bado haijafahamika.

''Ni kweli wagonjwa hao wapo lakini haijafahamika  chanzo halisi cha matatizo yao na uchunguzi ulikuwa bado unafanywa kubaini hasa chanzo chake," alisema Dk. Jose.

Hata hivyo, alisema baadhi ya watu hao wameanza kupata nafuu lakini wengine hali zao bado mbaya.

Ofisa Mtendaji wa kata hiyo, Sofia Manyilizu, alisema serikali kwa kushirikiana na  vyombo vya dola na madaktari, walikuwa wanajaribu kuchunguza  chanzo cha tukio hilo.

''Mimi kama mlinzi wa amani wa kata ya Nyampurukano lilipotokea tukio, nilifika na kuchukua maelezo ya awali pamoja na orodha, ambapo jumla ya watu 20 wakiwamo na watoto, wameathiriwa na tukio hilo," alisema.

Miongoni mwa waliothiriwa na chakula hicho ni wazazi, watoto, wajukuu na vitukuu ambapo baba wa familia hiyo, Stanslaus Kisinza, hali yake bado ni mbaya.

Mbunge wa Sengerema (CCM), William Ngeleja,  ambaye yuko  mkoani Shinyanga kikazi, alitoa pole kwa familia hiyo na kusisitiza  kuwa tukio hilo ni lazima lifanyiwe uchunguzi wa kina.

"Taarifa za tukio hili nimezipata leo (jana), baada ya kuwasili mkoani hapa (Shinyanga) kikazi nikitokea Dar Salaam na kwa hakika limenishtua sana," alisema.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate