Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova akionesha mapanga yanayodaiwa kutumiwa kumjeruhi Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi nyumbani kwake hivi karibuni. Katikati ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima Dar es Salaam jana. (Picha na Mroki Mroki).
WATU tisa wanashikiliwa na Polisi Dar es Salaam kwa tuhuma za kuvamia nyumbani na kumjeruhi Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba na mwanasheria mkongwe, Dk Sengondo Mvungi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emannuel Nchimbi alisema jana Dar es Salaam kuwa baadhi ya watuhumiwa hao walikutwa na simu iliyoporwa nyumbani kwa Dk Mvungi pamoja na mapanga yanayodaiwa kutumika katika shambulizi hilo.
Dk Mvungi alivamiwa na kushambuliwa wiki iliyopita nyumbani kwake Kibamba na kupoteza fahamu kukimbizwa katika Hospitali ya Tumbi, Kibaha kabla ya kuhamishiwa Muhimbili ambako alilazwa katika Taasisi ya Mifupa (MOI) na kishsa kupelekwa Milpark, Afrika Kusini ambako anatibiwa.
Waziri Nchimbi alisema baada ya mahojiano ya kina washukiwa hao walikiri kushiriki tukio hilo na walitoa ushirikiano wa kutosha hadi kupatikana kwa mapanga hayo na kigoda.
“Uchunguzi wa Polisi katika tukio hili umekamilika kwa asilimia 80, tumebakiza watu wachache walioshiriki na tunawahakikishia wananchi kuwa tutawakamata hivi karibuni,” alisema Nchimbi ambaye alifuatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima na Mkuu wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova.
Kova alitaja waliokamatwa kuwa ni Msigwa Mpopera ambaye ni mlinzi nyumbani kwa Dk Mvungi ambaye kwa mujibu wa Kova ndiye alikuwa kiongozi wa tukio hilo na kwamba aliongoza wenzake kufanya shambulio hilo.
Mwingine ni Chibango Magozi ambaye alikamatwa akiwa na simu iliyoibwa nyumbani kwa Dk Mvungi. Kamanda Kova alisema baada ya watuhumiwa hao kubanwa walitaja wenzao na kukubali kwenda kuonesha mapanga waliyotumia kutenda uhalifu huo.
Wengine wanaoshikiliwa ni Ahmed Ali, Zakaria Msesa, Manda Saluwa, Paul Jailos na Juma Khamis ambao wote ni wakazi wa Vingunguti; Longishu Semariki mwuza tumbaku (ugoro) katika eneo la Msimbazi na Msunga Makenza dereva wa bodaboda Kitunda.
“Upelelezi wa tukio hili umefanywa kwa kiwango cha juu na tunashukuru ushirikiano uliooneshwa na familia na vyombo vya habari,” alisema Kamanda Kova.
Alisema kazi iliyobaki sasa ni kukamilisha upelelezi na kupeleka jalada kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) ili atoe kibali cha kesi hiyo kwenda mahakamani.
Akijibu maswali ya waandishi wa habari, Kova alisema uhalifu aliofanyiwa Dk Mvungi hauhusiani na siasa kwani ushahidi unaonesha kuwa watuhumiwa walikuwa wanatafuta kipato.
Ulimboka, Kibanda
Alipoulizwa sababu ya upelelezi wa tukio la Dk Mvungi kuharakishwa, wakati kuna matukio kama ya Mhariri Mtendaji wa New Habari, Absalom Kibanda na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Steven Ulimboka hadi leo Polisi iko kimya, Kova alisema watuhumiwa wa Dk Mvungi walipatikana haraka kutokana na ushirikiano wa vyombo vya habari na familia.
“Unajua katika tukio hili hazikuwapo habari za Polisi kuhusika au mhusika ni nani, haya mambo ya upelelezi ukishamtuhumu polisi wakati ndiye anafanya upelelezi wakati mwingine inakatisha tamaa,” alisema Kova.
Dk Nchimbi alifafanua kuwa matukio ya Dk Ulimboka na Kibanda yanaendelea kufanyiwa uchunguzi.
“Katika nchi zinazoendelea, upelelezi wa matukio mengine unafanyika hata miaka mitatu au minne na baadaye watuhumiwa wanakamatwa kirahisi.”
Wakati huo huo, Dk Nchimbi alisema katika kupambana na uhalifu nchini, Polisi itasambaza maofisa wake wapatao 200 kila tarafa ambao watashirikiana na Polisi Jamii kupambana na uhalifu.
CHANZO NI HABARI LEO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
HABARI MBALIMBALI
‘Dk. Cheni’
‘Sharo Milionea
‘Thea’
African Women
AGNESS MASOGANGE
AK CLASSIC COSMETICS
ALI KIBA
Amanda Poshy
Ant
ANT LULU
Ashley Toto
Aunt Ezekiel
Aunty Ezekiel
AUNTY LULU
Azam Fc
Baby Madaha
BAHATI BUKUKU
Barnaba
BATULI
BBA
Beauty of the day
Belle 9
BI KIDUDE
BIBI BOMBA
Big Brother
Big Brother Africa
Bill Gates
BINTI KIZIWI
BOB JUNIOR
Bodi ya Filamu
Bongo Movie
Bongo Movies
CCM
CHADEMA
Chombezo
Christina Shusho
Chuchu hans.
Clouds Media Group
Club Bilicanas
DAR LIVE
DAVINA
Dayna Nyange
Diamond
Dida
Diva Loveness Love
Dj Ommy Crazy wa Maisha Club
DOGO JANJA
DOKI
DR.CHENI
DSTV
Dude
Dully Sykes
EBSS 2013
Elizabeth Michael
Epiq Bongo Star Search (EBSS)
ESHA BUHETI
Ester Bulaya
Feza Kessy
FIESTA 2014
Flaviana Matata
FLORA MBASHA
FLORA MVUNGI
Francis Cheka
GARDNER
GLOAL PUBLISHERS
GLOBAL TV ONLINE
H. BABA
Halima Mdee
HAMISA
Happy birthday
Hemedi
Hemedy Suleiman
HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE
Hoyce Temu
Huddah Monroe
HUSINA
IRENE PAUL
Irene Uyoya
ISABELLA
J film 4 life
Jack Chuz
JACK PATRICK
Jacob Steven ‘JB’
Jacqueline Dustan
JACQUELINE WOLPER
Jaji Khamis 'Kashi'
Jay Dee
JENNIFER KYAKA (ODAMA)
JIDE
JINI KABULA
JK
JO
Johari
Jokate Mwigelo ‘Kidot’.
JOTI
Joyce Kiria
Joyce Kiwia
JUX
K-LYNN
KADINDA
kaja
Kajala Masanja
Kapotive Star Singers
KATUNI
Kemmy
Kero Zetu
KHADIJA OMAR KOPA
KIKWETUKWETU
KILI MUSIC AWARDS
KOLETA
Lady Jay Dee
Lady Jaydee
Lake Oil
LAVEDA
Linah Sanga
Linex
Lisa Jensen
Loveness Diva
Lucy Francis Komba
Lulu
M2 The P
MABILIONEA
Madam Rita
MADELA
Magazeti
Mahusiano
Maimartha Jesse
MAINDA
MAISHA
Makala
Malkia Elizabeth
MAMTEI
MANDELA
MARIAM ISMAIL
Masanja Mkandamizaji
Mashindano ya Miss Tanzania
Matangazo
Matonya
MaxMalipo
MAYA
MELLIS EDWARD
MENINAH
MGOSI MKOLONI
Mh Halima Mdee
mic
Michezo
MILLEN HAPPINESS MAGESE
MISS CHANG'OMBE
MISS DAR CITY CENTER
Miss East Africa
MISS REDD'S IRINGA 2013
MISS TANGA 2013.
MISS TANZANIA 2014
Miss Tanzania mwaka 2011
MISS TEMEKE 2014
MISS USTAWI
MISS UTALII TANZANIA 2012/13
Miss vyuo vikuu 2013
MKALA
MREMBO HUDDAH
Mrisho Mpoto
Mrisho Ngassa
MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES.
MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013
Mtitu
muziki
Mwana FA
MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Mzee Majuto
Nancy Sumari
Nani Mtani Jembe?
NAPE
Nassoro ‘Nora’
Natasha
Nay wa Mitego
Necta
Nelly Kamwelu
NEY WA MITEGO
Nisha
NSSF;Zantel
Nyamwela
NYimbo
Nyota yako
OBAMA TANZANIA
OMMY DIMPOZ
P FUNK
PAM D
Peniel Mgilwa ‘Penny’
PETIT MAN
Profesa Jay
Q - CHILA
Q Boy
Q Chilla
QUEEN DARLEEN
RACHEL NDAUKA
RAIS KIKWETE
Rais Kikwete.
Rasimu Ya Katiba TZ
Ray
Ray C
Redd’s Miss IFM
REDD'S MISS KAGERA 2013
REDD'S MISS TZ
REDDS MISS TANZANIA 2014
Redds Miss wa Mikoa
REHEMA FABIAN
RICHIE RICHIE
Rihanna
ROSE MUHANDO
Rose Ndauka
Ruge Mutahaba.
SABASABA 2013
Saida Karoli
Saikolojia
Sajeti
SAJUKI
Sandra
SHAA
Shamsa Ford
Sheikh Ponda
Shilole
Sintah
Siwema
Skin Tricks
Snura Mushi
Spika Makinda
staa
Staa Wetu
Stella Mwangi
STYLE ZA NYWELE
Taifa Stars
Tamasha la matumaini
TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013
Tangazo
TANZANIA
TEGO
TENGENEZA WEBSITE NA BLOG
TID
Tundaman
Tupo wangapi?
TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Twanga Pepeta
USA PAGEANT 2014
VAI
Wastara
WEMA
WEMA SEPETU
Yanga
Yanga Bingwa 2013
YOUNG D
Yvonne Cherry ‘Monalisa’
Z Anton.
Zari
Zito kabwe
No comments:
Post a Comment