EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, November 16, 2013

WAHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA, NDUGU WAANGUA VILIO!

Stori: Mbeya Yetu
NDUGU wa watuhumiwa wawili kati ya wanne waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana hatia la kumuua aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, John Mwankenja waliangua vilio baada ya hukumu hiyo.
 
Marehemu  John Mwankenja, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe enzi za uhai wake.
Jumatano iliyopita, Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya aliyekuwa ikiendesha vikao vya kesi katika Mahakama ya Wilaya ya Rungwe, Samuel Karua alipotoa hukumu hiyo, baadhi ya ndugu wa waliohukumiwa walilipuka kwa vilio kutokana na uchungu wa adhabu hiyo.
      Kushoto hakimu Mwakalinga ambaye ni mshtakiwa wa kwanza kuhukumiwa kunyongwa.
Hukumu ya kesi hiyo iliahirishwa kutolewa zaidi ya mara tatu na kuzua hali ya sintofahamu kwa ndugu wa washtakiwa na wafuatiliaji wa kesi hiyo, wengi wakihoji kulikoni!

Kabla ya kusoma kwa hukumu hiyo, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Archiles Mulisa aliwataja watuhumiwa wote wanne kuwa ni Hakimu Mwakalinga, Daudi Mwasipasa, Obote Mwanyingili na Kelvin Myovela wanaokabiliwa na tuhuma za kumuua kwa makusudi John Mwankenja.
Baadhi ya wananchi wakiwa nje ya mahakama.
Alisema watuhumiwa hao wenye kesi namba 131/2012 walitenda kosa hilo Mei 19, 2011 katika Kijiji cha Mpandapanda, Kata ya Kiwira, Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.
Akisoma hukumu hiyo, Jaji Karua ambaye alianza majira ya saa 8:37 mchana na kumaliza saa 9:37 alasiri alisema katika kesi hiyo upande wa mashtaka na utetezi haubishani kuhusu kifo cha marehemu.
Aliongeza kuwa pande hizo pia hazibishani kuhusu ripoti za kitaalam na dhamira za mauaji hayo bali kinachobishaniwa ni uhusika wa watuhumiwa hao dhidi ya mauaji hayo.
Alisema katika kutetea hoja zao upande wa mashtaka ulipeleka mahakamani mashahidi 11  wakiongozwa na shahidi namba moja aliyewatuhumu washtakiwa kuhusika na tukio hilo.
Shahidi huyo namba moja Weston Jacob (17) mkazi wa Kiwira na mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari Kipoke ambaye pia ni mjomba wa marehemu ambaye aliiambia mahakama kuwa siku ya tukio akiwa nyumbani saa 2: 30 usiku marehemu alifika na kupiga honi ya gari akitaka afunguliwe mlango.
Kutokana na ushahidi huo, Jaji Karua alisema  mshtakiwa namba moja na namba mbili ambao ni Hakimu Mwakalinga na Daudi Mwasipasa wanatiwa hatiani kuhusika moja kwa moja na mauaji kutokana na kukiri kwao kwa mlinzi wa amani, mchukua maelezo na  vipimo vya vinasaba.
Alisema mshtakiwa namba tatu, Obote Mwanyingili yeye anatiwa hatiani kutokana na kosa la kumhifadhi mtuhumiwa namba moja baada ya kutoka kufanya mauaji hivyo yeye hausiki na kosa hilo.
Jaji Karua alisema mshtakiwa namba nne, Kelvin Myovela anatiwa hatiani kutokana na kuhifadhi silaha iliyotumika katika mauaji hayo ingawa hakuhusika na kitendo hicho.
Kutokana na ushahidi huo, Jaji Karua alisema washtakiwa namba moja na namba mbili wanahukumiwa kunyongwa hadi kufa.
Aliongeza kuwa, mshtakiwa namba tatu aliyemhifadhi mtuhumiwa wa kwanza ataenda jela miaka saba, mshtakiwa namba nne,  Kelvin Myovela aliyehifadhi silaha iliyotumika kwenye mauaji hayo atatumikia kifungo cha  miaka saba.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate