EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, January 9, 2014

BENKI YA COVENANT YAZINDUA HUDUMA YA BENKI MTAANI KWAKO


   Mwenyekiti wa Bodi wa benki ya Covenant Balozi.Salome Sijaona(katikati)akibonyeza kitufe cha kopyuta kuashiaria uzinduzi rasmi wa huduma ya” benki mtaani kwako” ambayo inawawezesha wananchi na wateja wa benki hiyo kutumia simu zao za kiganjani kupata huduma za kibenki ikiwemo kuweka na kutoa fedha katika akaunti zao.Anaeshuhudia kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Bi.Sabetha Mwambenja pamoja na wajumbe  wa bodi wa benki hiyo.
  Mwenyekiti wa Bodi wa benki ya Covenant Balozi.Salome Sijaona(kulia)akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa uzinduzi rasmi wa huduma ya” Benki Mtaani Kwako” ambayo inawawezesha wananchi na wateja wa benki hiyo kutumia simu zao za kiganjani kupata huduma za kibenki ikiwemo kuweka na kutoa fedha katika akaunti zao.kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Bi.Sabetha Mwambenja.
  Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Covenant Bi.Sabetha Mwambenja(katikati)akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi rasmi wa huduma ya” Benki Mtaani Kwako” ambayo inawawezesha wananchi na wateja wa benki hiyo kutumia simu zao za kiganjani kupata huduma za kibenki ikiwemo kuweka na kutoa fedha katika akaunti zao,pamoja nae katika picha ni  Mwenyekiti wa Bodi wa benki hiyo Balozi.Salome Sijaona(watatu kutoka kushoto) pamoja na wajumbe  wa bodi wa benki hiyo.
=========  ========  ========
BENKI YA COVENANT YAZINDUA HUDUMA YA BENKI MTAANI KWAKO
Dar es Salaam 9, Januari 2014. Katika kuhakikisha inaendelea kupanua wigo na kusogeza huduma zake za kibenki karibu na wateja  wake benki ya Covernant imezindua huduma za kibenki kwa njia ya simu inayojulikana kama”Benki Mtaani kwako” huduma hii ambayo itawawezesha wateja wa benki hiyo kuweka na kutoa fedha katika akaunti zao kupitia simu za Mkononi.
Akizungumza  wakati wa kuzindua huduma hiyo Mwenyekiti wa Bodi wa benki hiyo Balozi.Salome Sijaona,amesema kuwa benki yake inawalenga watu wa kawaida kabisa ambao wengi wao wanaishi maeneo ya nje ya mji wengi wao wakiwa wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo hivyo kuanzisha huduma hii ni faraja kubwa kwa wateja wetu ambao hawatapata tabu tena ya kutoka sehemu waliko kuja katika tawi la benki hiyo kupata huduma.
“Uzinduzi huu umekuja wakati muafaka ikiwa ni sehemu muhimu ya kuendelea kuboresha na kusogeza huduma zetu kwa wateja wetu, tuna wateja maeneo mengi ya mjini na vijijini, tumeona ni jambo jema kuwaanzishia huduma hii ambayo haita walazimu wao kuja katika tawi letu kupata huduma, aliongeza  Balozi Sijaona.
“Tunawajali na kuwathamini wateja wetu na sasa tumewaletea huduma hii ya  kuweka na kutoa pesa kwenye akaunti zao kupitia simu za kiganjani wakiwa mahala popote pale, wote tunatambua kuwa dunia ya sasa teknolojia ndio kila kitu, mtu anapoweza kupata kila kitu kupitia simu yake ya mkononi ni jambo jema kwetu, natoa wito kwa wateja wetu kutumia huduma hii ambayo naamini ni suluhisho kwao watakapo kuwa na uhitaji wa kuweka au kutoa fedha katika benki yetu.”
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Bi. Sabetha Mwambenja amesema amefurahi kwa benki yake kuendelea kuboresha huduma kwa wateja wake na kuhakikisha wanafikia malengo ya huduma bora kwa wateja wake,Pia alizitaja sifa muhimu za huduma hiyo kuwa ni kulipia Ankara mbalimbali,kuhamisha fedha kwenda akaunti yoyote uliyokuwa nayo na covenant benki,kuhamisha fedha kupitia mtandao wowote wa simu za viganjani nchini,kutuma na kuchukua fedha ATM bila kadi ya benki hata kama aliyekutumia hana akaunti na Covenant benki,kupata miamala uliyofanyika kwenye akaunti yako na kusajili huduma hii mwenyewe kupitia simu yako na usajili unakamilika papo hapo.
“Tunamipango mingi ya kuendelea kupanua na kuboresha huduma zetu, hadi kufikia sasa tunashukuru namna ambavyo wateja wetu wameendelea kutuunga mkono siku hadi siku, tunawaahidi kuendelea kuwaunga mkono na kuhakikisha tunatimiza ndoto zao za kuwa na maisha bora.”
Tunaendelea kuwahamasisha Watanzania kuendelea kujiunga na huduma zetu ambazo zinafaida nyingi kwani wateja wanaweza kutumia akaunti zao wakati wowote,kuondoa adha ya kusafiri/kutembealea tawi la benki,kuhamisha fedha kwa uwapendao kwa urahisi zaidi,wanaweza kuwalipa washiriki wa biashara na wagavi bila wasiwasi,Pia hadi sasa tunazo akaunti za aina mbalimbali ambazo ni akaunti za akiba inayojumuisha akaunti ya Ahadi, Jerusalem, Tausi Women Entrepreneurs Account, Winner Junior account, Vikundi, Akaunti ya Akiba ya Bajaj, Akaunti ya Muda Maalum na nyinginezo na akaunti za biashara ni pamoja na akaunti binafsi na nyinginezo.

Ili kujiunga na huduma hiyo Mteja wa benki hiyo atatakiwa kupiga namba *150*27#

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate