EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, January 9, 2014

“TUTAKUZA USHIRIKIANO NA ALGERIA”, WAZIRI MKUU


 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda akiwa katika kikao na Ujumbe kutoka  nchi ya Algeria wakiongozwa na Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria Mhe. Youcef Youfsi (wa kwanza kulia) walipomtembelea jana Ofisini kwake. Wa kwanza Kushoto ni Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Profesa Sospeter Muhongo. Wengine katika picha ni Watendaji wa Mashirika ya nishati na gasi ya Tanzania.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda  (katikati) katika picha ya Pamoja na Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria Mhe. Youcef Yousfi na  ujumbe wake ( wa pili kushoto mstari wa mbele), Wa pili kulia ni Waziri wa Nishati na Madini Mhe.profesa Sospeter Muhongo .

Na Asteria Muhozya
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda amesema Tanzania itakuza uhusiano na ushirikiano na nchi ya Algeria kutokana na nchi hiyo kuwa mfano mzuri kwenye uwekezaji wa rasilimali asilia.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana wakati Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria Mhe. Youcef  Yousfi alipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Aliongeza kuwa, Algeria ni moja ya nchi zilizopiga hatua kubwa katika maendeleo ya sekta ya nishati za gesi na umeme  kutokana  na kwamba sekta hiyo inachangia takribani asilimia 60 ya uchumi wa nchi hiyo hali ambayo inatoa fursa kwa Tanzania kujifunza na kuendeleza sekta hiyo kutoka kwao.

 “Ni fursa nzuri kwetu kujua namna wenzetu walivyoweza kufanikiwa na kuendelea kwa kutumia rasilimali hizo. Hali ambayo imefanya nchi hii kuwa mwalimu wa Mataifa mengine yanayochipukia katika kuwekeza katika rasilimali hizo”. Alisema.

Aidha Waziri Mkuu aliongoza kuwa, Algeria ni nchi ya mfano kwa Tanzania ikizingatiwa kuwa, imezisaidia nchi kadhaa za Falme za kiarabu zilizofanikiwa  katika sekta hiyo ikiwemo pia nchi ya Qatar.
Akiongelea kuhusu Serikali kumiliki uchumi kupitia sekta hizo kama ilivyo kwa Algeria, Waziri Mkuu alisema Serikali inataka kuona nchi hii inafanikiwa katika hilo.

“Serikali ya Algeria inasimamia asilimia 51 ya hisa katika sekta hizo kupitia kampuni za umma, na sisi tuna makampuni kama  Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania ( TPDC), na  Shirika la Madini Tanzania (STAMICO) hivyo tunataka kujifunza kwa wenzetu kuona namna gani vyombo vyetu vya umma vinavyoweza kufanya kazi kwa kuangalia mifano ya wenzetu na kukidhi matarajio ya wananchi.” Alisema.

Kuhusu kuendeleza rasilimali watu katika sekta hiyo, Waziri Mkuu kwanza ameishukuru Serikali ya Algeria kwa kuendelea kutoa msaada wa ufadhili kwa wanafunzi kusoma nchini humo, lakini zaidi hasa katika masomo ambayo ni maalumu katika sekta hiyo.
Aliongeza kuwa, ni funzo kwa Tanzania kuona namna gani Serikali itavitumia vyuo vilivyoko nchini kuzalisha wataalamu wa sekta za gesi,mafuta,umeme na madini.

Vilevile alisema kuwa anaamini wizara ya Nishati na Madini imejipanga vizuri kutekeleza mipango na hivyo ameitaka Wizara kuhakikisha wananchi wanapata matokeo ya haraka katika muda mfupi.

Kwa upande wake Waziri wa Nishati na Migodi Algeria Mhe. Youcef Yousfi ameishauri Serikali kutekeleza makubaliano yaliyofikiwa kwa kuwa yanatarajia kuleta tija kwa Tanzania huku watanzania wenyewe wakiwa na utaalamu mkubwa katika sekta hiyo. “Tunataka kuisaidia Tanzania kujua namna bora ya kusambaza umeme na gesi, ndio maana tuko hapa alisema”, Waziri Yousfi. 

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate