EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, January 7, 2014

FRANCIS BENARD; MIAKA 29 KITANDANI MUHIMBILI, HANA NDUGU!

ALIPOPANDA basi kutoka Tanga kuelekea Dar es Salaam mwezi fulani mwaka 1984, hakujua kama ilikuwa ni siku yake ya mwisho kuwa mzima, mwenye mwili mkakamavu uliokamilika viungo vyote.
Akiwaacha nyuma mkewe, Veneranda Makamba na watoto wake wawili, Bashangi (aliyekuwa na umri wa miaka 12) na James (10), Francis Benard aliyekuwa na umri wa miaka 46 wakati huo, uzima wake ulikomea maeneo ya Mto Wami, ambako alipata ajali iliyomlaza kitandani akiwa mahututi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa miaka sita.

Hadi wakati akipata ajali hiyo, Francis alikuwa mjasiriamali, hivyo tukio hilo liliharibu kabisa mfumo mzima wa maisha yake kiuchumi.
Na bahati mbaya nyingine, akiwa hospitalini hapo, mkewe Veneranda alifariki dunia na hivyo kusababisha watoto wake kulelewa na watu asiowafahamu hadi leo akiwa na umri wa miaka 75.
Mzee Francis amepooza sehemu kubwa ya mwili wake, hali inayomfanya awe mtu wa kulala tu na akibadilisha sana ‘style’ basi ni kukaa. Hawezi kusimama, hawezi kutembea na hana hata ndugu. Kwa miaka 29 sasa anaishi na watu asiowafahamu.
Baada ya kukaa kwa miaka mingi hospitalini hapo akiwa katika hali hiyo, ambayo mwenyewe aliielezea kama kupata nafuu, alihamishwa na kupelekwa katika kituo cha kuhudumia watu wasiojiweza kinachojulikana kama Kwa Mama Theresa, kilichopo Mburahati jijini Dar es Salaam.
“Nikiwa nimelazwa pale Muhimbili, nilijifunza kufuma maua na vitambaa kiasi kwamba baadhi ya wagonjwa wenzangu wakanitambua. Wakawa wanakuja kwangu wananunua. Hadi napelekwa Mburahati nilishakuwa maarufu na nikawa na wateja wengi.
“Sasa nilipohamishiwa kule, wateja wangu wakawa wanaendelea kunifuata, kitendo kile kikawaudhi baadhi ya wenzangu wa pale, wakaanza kuninunia, wakawa wananinyima baadhi ya vitu,” anasema mzee Francis.
Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya kwa upande wake, alisema aliamua kukodi teksi kwa fedha kidogo alizozihifadhi na kuelekea Muhimbili ambako alipewa tena kitanda hadi sasa.
 
Anawashukuru sana wauguzi na uongozi wa hospitali hiyo ya taifa, kwani wanamtunza vizuri, licha ya taabu kubwa ya kimwili anayoipata.
Mzee Francis yupo wodi namba 14 katika Jengo la Kibasila na kidogo kidogo bado anaendelea kujikimu kwa namna hiyo ya kufuma na kutengeneza maua, ambayo pia yamemfanya kupata marafiki.

MSAADA
Kutokana na uwezo wake wa kujua kufuma vitambaa na kutengeneza mapambo mengine ya urembo, mzee huyo anaomba kuwezeshwa zaidi ili aweze kujiongezea kipato.
Na kwa vile ajali hiyo ilimfanya ashindwe kusimama wala kutembea, anamuomba Mtanzania yeyote kumsaidia baiskeli ya walemavu ili aweze kutembelea ambayo alisema amesikia kuwa zinauzwa shilingi laki nane za Kitanzania.
Kwa aliyeguswa na tatizo la mzee huyu anaweza kwenda Hospitali ya Muhimbili wodi 14 Kibasila au kuwasiliana naye moja kwa moja kupitia simu yake namba 0653313804.
CREDIT:GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate