EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, January 7, 2014

HAWEZI KUKUFANYIA KILA KITU, RIDHIKA!

NYAKATI za mwanzo wa uhusiano, huba na kila aina ya manjonjo kwenye mapenzi hutawala. Huwa na vitu vingi sana vya kuvutia, visivyochosha. Ni rahisi kuwasikia wenzi wakilaumiana kwa kutokuamshana asubuhi!
Yeah! Ni mambo ya mwanzo hayo. Ni ukweli ulio wazi kuwa, katika siku za mwanzo za wapenzi kukutana na kufahamiana, kila mmoja huwa makini kuhakikisha hamuudhi mwenzake.

 Kila kitu hufanyika kwa umakini huku akizingatia kuwa kuna mtu mwingine katika maisha yake. Hataki kumkwaza mtu ambaye ndiye furaha yake. Kwa maneno mengine, kuchukia kwake, kutamfanya hata yeye akose furaha pia.

Hiyo ndiyo sababu kubwa hasa zinazowafanya wengi kuwa makini na uhusiano kuwa wenye nguvu. Ilivyo ni kwamba, baadaye uhusiano ukishachangamka na kufikia angalau mwaka mmoja au zaidi, kuna mambo yatabadilika.

Tayari hawa ni marafiki wakubwa, ambao kwa namna moja au nyingine wanafahamiana kwa karibu zaidi na pengine wameshaanza kuzoeana sasa. Marafiki, huo ndiyo ukweli wenyewe ulivyo.
Mfano niliotoa hapo juu, unafanana kabisa na hata kwa upande wa wanandoa. Siku za mwanzo wa ndoa huwa kuna vitu vinakuwa na mguso na mvuto wa aina yake lakini siku zinavyozidi kwenda, ndivyo baadhi ya mambo huanza kubadilika taratibu.

Ni mfumo. Hakuna cha ajabu. Hata hivyo, yapo mambo ambayo hupaswa kuzingatiwa ili penzi liendelee kudumu. Kweli kuna kupishana baadhi ya maeneo lakini sasa yasisababishe maisha yashindwe kuendelea mbele.

Hapa kwenye Love & Life tunazingatia kwamba, maisha ni mtindo ambao huchaguliwa na mhusika mwenyewe. Kwa mfano, ukiamua kumnunia mkeo au mumeo kwa sababu amefanya jambo fulani ni sawa na kulazimisha ‘stress’ ambazo si za lazima.
Kwa nini usishughulikie tatizo likaisha mara moja? Marafiki zangu, hasa wale ambao ndiyo kwanza mmeingia kwenye ndoa hivi karibuni (namaanisha kuanzia siku moja – miaka mitatu), lazima mjitahidi kutofautisha maisha ya ndoa na yale ya urafiki na uchumba.

KWA NINI HASA?
Sababu za msingi zaidi nimezieleza hapo juu. Lakini jambo kubwa la kuongezea hapa ni kwamba, mnapokuwa kwenye ndoa, mnapaswa kufahamu kuwa mmejiunganisha kwa ajili ya maisha yenu moja kwa moja.
Wakati fulani mume anaweza kuwa bize  akihangaika na kufikiria kufanya kazi pengine zaidi ya tatu kwa wakati mmoja ili familia yake ijiendeshe sawasawa. Si rahisi muda wote kukawa na mahaba yale yaliyokuwa zamani.
Sawa, ni vyema kutenga muda wa kukaa na mwenzako na kufurahia maisha. Hapo mnaweza kuamua kutoka au pengine hata kama ni mazingira yaleyale lakini kwa staili tofauti na siku nyingine.
Kikubwa ni kuwekeza upendo wako wa dhati moyoni mwako na ujihakikishie kuwa uliridhika naye kabla ya kuingia kwenye muunganiko huo. Upendo ndiyo umebeba kila kitu.

MAHITAJI
Kuna baadhi ya wanandoa (hasa wanawake) wamekuwa na tabia ya kuwalalamikia waume zao kuwa hawawapatii mahitaji yote ya muhimu kama zamani. Utakuta mwanamke anataka nguo mpya kwa mfano, anataka kupelekwa ufukweni au kwenye bendi.
Hayo ni mambo ambayo mumewe alikuwa akiyafanya wakati wa uchumba wao lakini sasa amebadilika. Jambo la kujiuliza, ni je, kuna tofauti ya tabia kati ya wakati huo na sasa?
Je, muda ambao umekuwa ukienda naye kwenye bendi ndiyo anaoutumia huko nje sasa hivi? Hapa naomba nifafanue zaidi. Lakini nje inategemea na mahali anapokuwa. Mathalani yupo kwenye mihangaiko ya kutafuta fedha, si kosa.
Kumbuka sasa mpo kwenye ndoa, starehe si muhimu sana kama kujali familia na kutatua matatizo kwa haraka.
Siyo sawa kulalamika kwa kutotimiza baadhi ya mambo. Rafiki yangu, hataweza kufanya kila kitu, lakini pia kushindwa huko kusiondoe mapenzi ambayo yamejengeka moyoni mwako. Ridhika. Mpo kwenye mpambano wa maisha.
Wiki ijayo nitakuwa hapa kwa ajili ya kuhitimisha mada hii, USIKOSE!

CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate