EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, February 6, 2014

Kampeni za udiwani balaa

  • Ofisa Mtendaji akatwa mapanga
  • Mbunge CHADEMA, makada 16 wapanda kizimbani
Afisa mtendaji kata ya Ubangwe Alphonce Kimaro
KAMPENI za uchaguzi mdogo wa madiwani zimeingia katika hatua mbaya baada ya Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ubagwe, Alphonce
 
Kimaro, kukatwa mapanga, huku Mbunge wa Maswa Mashariki, Sylvester Kasulumbayi, akipandishwa kizimbani.

Wengine waliopandishwa kizimbani kwa tuhuma za kuwajeruhi wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni pamoja na Diwani wa Kata ya Buselesele, wilayani Chato, mkoani Geita, Christian Kagoma na makada wengine 15 wanaodaiwa kuwa wa CHADEMA.

Washitakiwa hao walikamatwa juzi na kufikishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Gadiel Mariki jana na kila mmoja kusomewa mashitaka sita.

Mwendesha Mashtaka wa Mahakama, Shukrani Madulu, alidai kuwa washtakiwa wote kwa pamoja walitenda kosa hilo juzi katika Kata ya Ubagwe.

Alidai kuwa washtakiwa hao wakiongozwa na Mbunge Kasulumbayi waliwashambulia kwa mapanga wafuasi wa CCM wakati wa kampeni za udiwani wa Kata ya Ubagwe iliyopo Halmashauri ya Ushetu.
Alidai kuwa katika vurugu hizo washtakiwa, pia walilishambulia gari la CCM la wilaya na kuliharibu.

Washtakiwa wote walikana mashtaka, lakini wamenyimwa dhamana kwa madai kuwa watu waliowajeruhi wako katika hali mbaya, kwani baadhi yao wamehamishiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando kutoka Hospitali ya Wilaya ya Kahama. Kesi hiyo imeahirishwa hadi leo.

Kabla ya kufikishwa mahakamani, walioshuhudia vurugu hizo walieleza kuwa majeruhi hao walikumbwa na mkasa huo wakati wakiwa kwenye gari la CCM wilaya ambalo pia lilikuwa na watuhumiwa watatu wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa CHADEMA, waliokuwa wakipelekwa kituo kidogo cha Polisi Bulungwa.

Watuhumiwa hao walidaiwa kufanya fujo kwenye mkutano wa kampeni wa Chama cha TADEA ambacho pia kimeweka mgombea wa udiwani katika Kata ya Ubagwe.

Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Kahama watu 16 akiwemo Mbunge wa Maswa
Mashariki, Kasulunabayi, walikamatwa na Polisi wakidaiwa kuhusika na vurugu hizo.

Baadhi ya majeruhi waliolazwa kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Mji
wa Kahama akiwemo dereva wa gari la CCM Wilaya ya Kahama, Charles Peter, walisema walipofika  kwenye kizuizi hicho walisimama ndipo wafuasi wa
CHADEMA waliposhuka kwenye gari la mbunge huyo na kuanza kuwapiga.

Ilielezwa kuwa Ofisa Mtendaji wa Kata hiyo, Alphonce Kimaro, alikumbwa na sekeseke hilo kwani alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa ndani ya gari la CCM akiwasindikiza watuhumiwa hao Polisi.
“Mtendaji huyo ni mmoja wa majeruhi waliojeruhiwa vibaya kwa kukatwa mapanga  ovyo mwilini na watu wengine watano wamejeruhiwa katika tukio hilo na hali zao ni mbaya,” alisema Peter.

Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Halmashauri ya mji wa Kahama, Richard Mabagala, aliwataja majeruhi wengine kuwa ni pamoja na Katibu Mwenezi wa CCM, Masuod Melimeli (34), Sebastian Masunga (34) na Ramadhani Salumu (24).

Wengine ni Subira Nyangusu, pamoja na Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ubagwe, Kimaro na dereva wa gari la CCM, Peter.
Kwa mujibu wa Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Andrew
Emmanuel, Masunga Kamaro na Peter walisafirishwa kwenda Hospitali ya Bugando
jijini Mwanza kwa matibabu zaidi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate