EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, February 1, 2014

MADENTI, PICHA ZA UTUPU ZA NINI?


Niwape hi kwa furaha sana wapendwa wasomaji wa safu hii, ingawa zaidi ningependa ziwafikie wanafunzi popote pale gazeti hili linaposomwa. Hawa jamaa ni wadau wangu wakubwa sana, hasa katika kubadilishana mawazo inapobidi.

Juzi nilikuwa naperuziperuzi kwenye mtandao, mara nikakutana na picha za aibu zilizopigwa na msichana ambaye ametambulishwa kama ni mwanafunzi, haikuelezwa kama ni denti wa sekondari au vyuo, lakini kwa uzoefu, inaonekana kabinti ni ka sekondari!

Nilipoziona, zikanikumbusha miaka kadhaa nyuma, kama minne au mitano hivi, wakati picha za msichana mmoja, aliyekuwa amevalia fulana zinazotumiwa na shule moja ya sekondari iliyopo Mbezi, jijini Dar es Salaam, zilipovuja na kufika gazetini. Binti huyo, alipigwa picha akiwa katika mikao mbalimbali akiwa mtupu!
 
Simulizi zilivuja kwamba kabla ya picha hizo kufika magazetini, ambako zilichapishwa, msichana huyo alishajaribu mara nyingi kuzuia zisisambae lakini bila mafanikio. Unajua ilikuwaje?

Mtu wa kwanza kuzidaka, alimfuata na kumuonyesha picha zake na kumtisha kuwa angezipeleka magazetini au kwa wazazi wake kama asingempa uroda. Kwa hofu, denti akalazimika kutii matakwa yale. Basi ikawa mchezo, picha zikaendelea kuhama kutoka kwa huyu hadi huyu na binti akajikuta akigeuka mtumwa wa ngono ili kulinda heshima yake, hadi alipokuja kugundua kuwa angetumika hadi mwisho wa dunia, akaamua kukataa, akisema liwalo na liwe, ndipo zilipofika gazetini na kutoka!

Kuna jambo moja la dhahiri kupitia kwa yule dada, kwamba alijuta na alifahamu kwamba alifanya makosa kupiga picha zile, ambazo kwa vyovyote alifanya hivyo akiwa na akili timamu kwani zote alionekana akiichekea kamera. Kama asingejuta, asingekubali kuwaziba watu midomo kwa njia ya kuutoa mwili wake kwa watu asiowafahamu.

Nimeanza na mchapo huo kama kuwaweka sawa ili muweze kunielewa ninachotaka kuwaambia na ambacho nyinyi wanafunzi, hasa wa kike, mtambue na kuchukua hatua ikibidi.
 
Utandawazi katika dunia ya sasa imeufanya ulimwengu kuwa mdogo unaofanana na kiganja. Simu za mikononi ni kila kitu, unazungumza na mwenzako aliye popote, unaingia mtandao wowote wa internet, unatuma au kupokea picha, sauti na kila unachokijua. Kwa maana hiyo, mtu mmoja anaweza kupiga picha akiwa Mbinga, kisha dakika moja baadaye akaonekana katika mtandao wa Facebook, Twitter, Instragram au popote na kujikuta picha hiyo ikionekana dunia nzima.

Wimbi la wadada kujipiga picha za utupu limeibuka upya na baadhi ya wanafunzi wamejikuta wakiingia mkenge. Ni hivi, wale akina dada, wakiwemo wasanii nyota wasiojitambua, wanapiga picha na kuziweka mitandaoni kwa ajili ya kujiuza. Yes, wanajiuza, tunajua!
Lakini napata taabu kidogo na wewe mwanafunzi kwa kufanya vitendo hivi. Unapiga picha hizo ili iweje anko? Unajiuza, kwa nini?

Kati ya watu ambao nafsi zitawashtaki baada ya kuwa zimewasuta sana, ni wanafunzi wanaojaribu kuingia katika ujinga huu. Ni punguani tu anaweza kukubali utupu wake uonekane dunia nzima. Madenti ni lazima wawe tofauti, waonyeshe kwa nini wao wanachukuliwa kuwa ni wasomi.
Kujipiga picha hizo na kuzitupia kwenye mitandao, ni kuonyesha kuwa kiwango cha kufikiri ni sawa na cha wale machangudoa wa Uwanja wa Fisi, Manzese Dar                 , ambao hawana mbadala wa kufanya zaidi ya kuuza miili yao.

Madenti wengi wanapigana picha za utupu na wengine hadi video. Huenda hufanya hivyo kwa kujifurahisha, lakini unapovua nguo na kumruhusu mtu akufotoe, ni zaidi ya kujifurahisha. Ninaogopa kama picha zako zitavuja na kumfikia mtu mwenye VVU, ambaye atakuahidi kutozipeleka magazetini kama utampa uroda. Huoni kama unajiua mwenyewe?
Tafakari, chukua hatua!
Je, una maoni yoyote, mkasa uliowahi kukukuta ukiwa shuleni ambao ungependa ujulikane kwa wasomaji? karibu ushiriki nasi kwa kutuandikia kupitia barua pepe ojukuus@yahoo.com

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate