EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, February 8, 2014

VALENTINE’S DAY ISIWE CHANZO CHA MAUMIVU YA MOYO!

BADO siku tisa tu kuifikia Sikukuu ya Wapendanao ambayo hujulikana zaidi kama Valentine’s Day. Kila mwaka huadhimishwa Februari 14, duniani kote.
Umejiandaaje kwa ajili ya siku hiyo? Je, kwako  itakuwa siku ya furaha au chanzo cha mateso kwako na kwa mwenzi wako? Unadhani unatakiwa kufanya nini ili kuifanya siku hiyo kuwa nzuri kwako?
Yapo mengi ya kufanya, lakini kabla ya kuingia huko tuone kwanza maana yake, japo kwa kifupi sana. Marafiki, kuna watu mpaka leo hawafahamu chimbuko na maana halisi ya siku hiyo muhimu. Hapa kwenye All About Love ni mahali sahihi zaidi pa kupata elimu hiyo.
Nini maana yake?
Asili hasa ya siku hiyo ni Roma.
Inaelezwa siku hiyo huadhimishwa kama kumbukumbu ya Padre Valentino ambaye aliuawa na Utawala wa Kirumi uliokuwa chini ya Mfalme Claudia kwa kosa la kutetea waumini wake wafunge ndoa.

Ilivyo ni kwamba, Mtakatifu Valentino alikerwa na Utawala wa Kirumi ambao uliwakataza vijana kufunga ndoa na badala yake kwenda vitani. Kwa msingi huo vijana wakawa na vimada nje hivyo kwenda kinyume na utaribu na maagizo ya imani aliyoisimamia.

Kwa sababu hakupenda hilo liendelee, akaamua kuendesha zoezi la kuwafungisha ndoa vijana kwenye makatakabo (mahandaki chini ya kanisa) kwa siri kubwa.
Hata hivyo, aligunduliwa na kufungwa na baadaye kuhukumiwa kifo. Kwa msingi huo, kwa sababu Mtakatifu Valentino aliuawa siku na tarehe kama hiyo, ikatangazwa rasmi kuandhishwa kwa ajili ya kumkumbuka kama Baba wa Upendo – mtetezi wa wanandoa.

Ikumbukwe kuwa, Padre mwenyewe alikuwa akiitwa Mtakatifu Valentino (unaweza kumuita Valentine), kwa maana hiyo, ilikuwa siku yake – ya kukumbuka alivyopenda watu wapendane.
Awali ilianza kuadhimishwa Roma, lakini baadaye ikaenea katika nchi za Magharibi na dunia nzima kwa jumla. Wakati mapokeo ya kuadhimisha siku hii yalipoanza, ilionekana kama ni ya kidini zaidi, lakini baadaye ilipochunguzwa mantiki ya uadhimishwaji wenyewe, ikaonekana kuwa na maana kwa watu wa madhehebu yote.

Aliyetangaza rasmi kuadhimishwa siku hiyo ni Papa Gelasius, ambapo alisema ikumbukwe kama ishara ya kumuenzi mtetezi wa ndoa, Mtakatifu Valentino.
Iadhimishwe kwa maana yake halisi
Baadhi ya watu wameibadilisha maana ya siku hii muhimu kwa wapendanao. Wenyewe wanahisi kuwa ni siku ya kufanya mambo yasiyofaa. Kwao, wapendanao ni ngono. Kuna ambao huanzisha uhusiano siku hiyo kwa lengo la kupata mtu wa kustarehe naye, hili ni kosa.

Kuna baadhi wamekuwa wakifanya vurugu na kila aina ya uchafu. Si maana yake. Kama nilivyotangulia kusema, ni siku ya kuonyeshana namna mnavyopendana na kuthaminiana. Msingi hasa hapa ni pendo la kweli.

Wewe unaiadhimishaje?
Wewe unaadhimishaje? Huwa una kawaida ya kufanya nini kwa ajili ya siku hiyo muhimu kwa ajili ya penzi lako?
Tunatofautiana kufikiria, kupanga na kufanya mambo. Inawezekana umezoea kumchukua mpenzi wako na kwenda naye katika hoteli ya kitalii kisha mnakula raha zenu huko halafu sikukuu inakuwa imeisha!

Si vibaya! Labda una mpango wa kushinda na mwenzako ndani siku nzima. Mwingine inawezekana anapanga kwenda katika ukumbi wa burudani na kusikiliza nyimbo nzuri za wapendanao. Si mawazo mabaya.

Hata hivyo, rafiki zangu lazima ufikirie kufanya jambo kubwa, maalum ambalo si tu halitasahaulika bali litatengeneza kitu kikubwa katika historia ya mapenzi yenu.
Inawezekana umeumiza kichwa sana ukijaribu kufikiria kitu cha kufanya kwa ajili ya kunogesha penzi lako, kuifanya ndoa yako kuwa imara, lakini uwezo wako wa kufikiri umefika mwisho na hujapata cha kufanya.

Ngoja nikuambie, umewahi kuwaza kuhusu kufanya hafla ya wapendanao? Hafla ya wapendanao ni nzuri, maana huwakutanisha wenzi na kupanga pamoja namna ya kuishi kwa amani na upendo.
Muda bado unaruhusu, wiki ijayo nitakuwa hapa kukuelekeza namna ya kufanya, USIKOSE!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate