EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, March 4, 2014

FREEMASON WATUA KANISA LA GWAJIMA

WATU wanaodaiwa kuwa ni wa imani ya Freemason wametua ndani ya ibada katika Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima, Uwazi lina ‘ei tu zedi’ ya tukio hilo.
Baadhi ya vitu vilivyokutwa kanisani kwa Gwajima.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, Freemason hao wawili waliingia kwenye ibada hiyo iliyofanyika Februari 23, mwaka huu ndani ya kanisa hilo lenye makao makuu yake katika Viwanja vya Tanganyika Peckers, Kawe jijini Dar wakiwa na mfuko wa rambo wenye vitu mbalimbali vikiwa na alama zao.
GWAJIMA MADHABAHUNI
Habari zilidai kwamba wakati neno likiendelea kunenwa na Mchungaji Gwajima, watu hao walifunua mfuko huo ambapo baadhi ya waumini waliokuwa karibu yao walihoji kulikoni kuwa kwenye ibada na vitu vyenye viashiria ya Freemason.
Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima.
“Wengine tulishangaa sana kwani baadhi ya vitu vilionekana kuwa na thamani kubwa, tukadhani labda wameleta zawadi kwa mtumishi wa Mungu (Gwajima),” kilisema chanzo hicho ambacho kinaabudu katika kanisa hilo.

MFUKO WANASWA NA WALINZI
Mtiririko wa tukio hilo unazidi kuwekwa wazi kwamba, haraka sana walinzi wa kanisa hilo walifika eneo lenye mfuko huo na kuunasa huku watu walioingia nao wakipotea au kujichanganya miongoni mwa waumini wengine.
WASIWASI WATANDA
Kufuatia tukio hilo, baadhi ya waumini wa kanisa hilo walipozungumza na Uwazi baada ya ibada kumalizika walisema wanaamini watu hao walifika kanisani hapo kwa nia mbili, kujisalimisha au kuzijaribu nguvu za Gwajima ambaye ni maarufu kwa kuibua misukule.
Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima akiongoza ibada.
MFUKO WENYE VITU
Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa, ndani ya mfuko wa watu hao kulikutwa saa ya rangi ya fedha, pete ya dhahabu, cheni 2 za fedha, bangili, fulana nyeupe na shati jeusi, vyote vikiwa na picha zenye alama mbalimbali za Freemason kama mafuvu, nyoka na bikari.
“Lakini mimi naamini wale watu nia yao hasa ilikuwa kumjaribu mtumishi wa Mungu ambaye ni kinara wa kuwarudisha watu waliokufa katika mazingira ya mazingara (misukule),” kilisema chanzo kimoja na kujitambulisha kwa jina moja la Isaya.
IMANI KWA GWAJIMA YAKAZIWA
“Mimi ninavyomjua Gwajima sidhani kama wangefanikiwa, ni vigumu sana. Kuna majambazi waliwahi kujaribu kumuua lakini waliambulia patupu, wakapigwa na upepo wa kisurisuri, sembuse Freemason? Ninachokijua mimi watamjaribu lakini hawataweza,” kilisema chanzo kingine.
UWAZI MZIGONI, WALINZI WAWA MBOGO
Wakati sakata hilo likiendelea, mmoja wa waandishi wa Uwazi alipata taarifa ambapo aliwahi tukio hilo na kujaribu kupiga picha lakini mlinzi mmoja (jina tunalo) alimkataza licha ya kufanya jitihada kubwa.
Mlinzi huyo alimnyang’anya kamera mwandishi wetu na kuishikilia kwa muda huku akitishia kufuta picha zote hata kama hazikuwa za tukio hilo.
GWAJIMA KIMYA
Baada ya kuinyaka ishu hiyo nzima, Uwazi lilitumia siku tano kumsaka Mchungaji Gwajima ili kupata mtazamo wake juu ya tukio hilo ambalo huenda ni la kwanza kwenye kanisa hilo la kiroho jijini Dar es Salaam lakini bila mafanikio kutokana na kukwamishwa na wasaidizi wake.
Awali, ilikuwa Februari 25, mwaka huu ambapo hakupatikana kanisani kwake na hata kwa njia ya simu.
Baada ya kumkosa mtumishi huyo kwa kutopokea simu, Uwazi lilimtumia ujumbe wa simu (SMS) na kumuuliza kuhusu tukio hilo na ikiwezekana kukutana ambapo alijibu kwamba alikuwa kwenye kikao cha viongozi wa Kikristo, Kurasini jijini Dar, hivyo asingeweza kuonana na wanahabari.
Ijumaa ya Februari 28, mwaka huu, waandishi wa gazeti hili walitumia saa tano kumsubiri Gwajima kanisani kwake bila mafanikio.
MSIKILIZE MSEMAJI WAKE
Baadaye msemaji wa kanisa hilo, Mchungaji Yeconia Bihagaze alipoulizwa juu ya sakata hilo aliliambia gazeti hili kuwa, matukio kama hayo hutokea mara kwa mara licha ya kuchukua muda mrefu ikilinganishwa na hili la juzikati.
“Mambo ya Freemason kujisalimisha hapa mbona ni ya muda sana! Mimi naona kama yamepitwa na wakati, tukio hilo unalolisema mimi sijalisikia. Kanisa letu ni kubwa, mambo mengine ni madogomadogo hivyo siyo lazima yafike kwenye uongozi wa juu.
“Kwa nini msiandike misukule tunaowafufua hapa kila siku? Kwa nini msichukue matukio makubwa kwenye mtandao wa kanisa letu? Ninyi wanahabari wakati mwingine huwa mnatuvunjia heshima ndiyo maana huwa tunaamua kuwapotezea,” alisema Mchungaji Bihagaze. 
CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate