EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, March 4, 2014

ABIRIA AJICHINJA NDANI YA BASI


AMA kweli duniani kuna mambo kwani dereva na abiria wa basi la Manchester ambalo namba yake haikujulikana mara moja, lililokua likitoka Lindi kwenda jijini Dar es Salaam walijikuta wakiangua vilio baada ya kumuona mwenzao akijichinja hadi kufa kwa kisu ndani ya gari hilo.
Ujumbe kabla ya kifo: Kijana aliyejichinja ndani ya basi akiandika ujumbe kabla ya kukata roho.
Kwa mujibu wa chanzo, tukio hilo la kusikitisha lilitokea saa tisa alasiri, Jumatano wiki iliyopita mara basi hilo lilipofika katika hoteli moja ya Nangulukulu kwa ajili ya kupatia chakula.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na waandishi wa habari hii jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, baadhi ya abiria walioshuhudia tukio hilo walisema kuwa  mara walipofika katika hoteli hiyo, kila mmoja alitawanyika kwa lengo la kujipatia chakula na baadhi yao walienda maliwatoni akiwemo marehemu huyo.
Msaada:...Kijana huyo akitolewa kwenye basi baada ya kujichinja kwa sime.
Walisema kwamba  marehemu huyo ambaye jina lake halikupatikana mara moja, wakati wa kushuka hakuonekana na kisu aina ya sime lakini baadaye abiria wachache waliotangulia kwenye gari, walimshuhudia akiwa ameshika sime hiyo mkono pasipokujua aliipata wapi.

“Hata sisi tulishangaa kumuona akiwa karibu  na usukani wa dereva huku akizamisha sime tumboni kisha kuichomoa  na kujichinja shingoni  hadi pale alipokuwa akivuta koromeo na kuning’inia.
Damu kila mahali: ...Akiingizwa katika gari lingine huku damu zikiwa zimetapakaa.
“Tulichanaganyikiwa kwani ni kitu ambacho hatukukitarajia na wala hatujawahi kushuhudia tukio kama hilo la mtu kujichinja hadharani, tulibakia kutokwa machozi huku akina mama wakipiga yowe, hakuna mtu aliyethubutu kumsogelea kumuokoa kwani kila mmoja alimuogopa.
“Tulishindwa kupanda basi hilo kwani ni tukio la ajabu pia ndani kwa mbele kulikuwa kumetapakaa damu, ghafla alidondoka chini ndani ya gari, aliomba kalamu na karatasi ili kuandika ujumbe.
 
Silaha: Polisi akiwa na sime aliyotumia kujichinja kijana huyo.
“Dereva alichukua kalamu na kipande cha karatasi na kumpa, alianza kuandika  huku damu ikimbubujika tumboni na shingoni, hatukujua alichokiandika, aliishiwa nguvu taratibu akadondoka.
“Abiria walimsogelea na kumuinua na walimueleza kuwa atubu kwa Mungu kosa alilolifanya kabla hajafa, alipiga magoti na kuomba,  ghafla alidondoka tena.
 
Imani: Kijana akisali kabla ya kukata roho.
“Kaka yake ambaye alikuwa akisafiri naye kuelekea Dar es Salaam alichanganyikiwa kwani hakutegemea kuwa mdogo wake angejiua, kwani alisema hana historia ya kuugua ugonjwa wa akili. Polisi walipigiwa simu na walifika kumchukua lakini baada ya muda mfupi akawa amefariki dunia.
“Sisi abiria wengine tuliendelea na safari kuelekea Dar es Salaam  ambapo marehemu na kaka yake walibakia huko  mkoani Lindi.
Kifo:...Kijana huyo baada ya kukata roho.
“Mara tulipofika Dar es Salaam dereva alitusihi tukae kimya kwa dakika moja na kuomba kutokana na tukio lililotupata, tulifanya hivyo baadaye kila mmoja alitawanyika na kuelekea kwake,” kilisema chanzo kwa sharti la kutoandikwa jina gazetini.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, ACP Renatha Mzinga alipoulizwa mwishoni mwa wiki iliyopita kuhusiana na tukio hilo alikiri kutokea.
“Ni kweli tukio hilo lilitokea lakini kwa sasa sina data kwani nipo njiani nikitokea Nairobi, Kenya kikazi kuelekea Lindi, mara nitakapofika huko ofisini ndipo nitapata tukio zima lilivyokuwa,” alisema Kamanda Mzinga.
CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate