EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, March 20, 2014

KILA SAA MAPENZI…MAPENZI…HIVI HAMNA MENGINE YA KUFANYA?

Mpenzi msomaji wangu, wiki iliyopita utakumbuka nilizungumzia suala la kuwajali wapenzi wetu. Niligusia suala ya kuwapa nafasi watuchune.
 
apo walioshituka kuona kichwa kile cha habari lakini kiukweli sikumaanisha kuchuna kule ambako wanawake micharuko hufanya hasa kwa waume za watu, nilimaanisha utayari wa kila mmoja kumsaidia mwenzake kifedha. Mkeo akitaka pesa ili aende saluni kama zipo, mpe! Akihitaji pesa akanunulie vipodozi na nguo kama pesa zipo, mpatie.

Tusibaniane pale ambapo Mungu ametujaalia uwezo wa kuwafanya wenza wetu waonekane watu mbele ya wenzao. Hili ni kwa mke na mume na hata wapenzi wa kawaida. Baada ya kugusia hayo, nigeukie sasa kwenye mada yangu ya wiki hii.

Ndugu zangu, nimekuwa nikipokea malalamiko mengi kutoka kwa baadhi ya wanawake wakielezea kukerwa kwao na tabia za waume zao kuendekeza sana tendo la ndoa. Wanaume wanaoweka mbele suala hili husimamia kwenye ile pointi kwamba, kufanya mapenzi na wake zao kila wanapojisikia ni haki yao ya ndoa.

Hali hii imewafanya baadhi ya wanawake kufikia hatua ya kuomba talaka kutoka waume zao kutokana na kushindwa kuhimili vishindo. Wanaume wengi huwa wagumu sana kuzitoa talaka na ndiyo maana wakati mwingine wanawake hulazimika kwenda mahakamani kudai talaka japo si wote wanaodai kwa kukimbia tendo la ndoa.

Wanaoendelea kuwepo kwenye ndoa na wanaume wanaohusudu mapenzi, hulazimika wakati mwingine kujifanya wanaumwa ili kuepukana na kero hii. Kimsingi ndoa haiwezi kunoga bila kuwepo suala la kukutana faragha na hili linaelezwa hata kwenye vitabu vya dini.
Tunaponyimana licha ya kuwakera wenza wetu lakini pia tunamkasirisha Mungu ambaye anatutaka tufanye hivyo ili tuzaliane. Hata hivyo, kila kitu kina kipimo chake na kikizidi inakuwa ni tatizo. Wazungu wanasema; ‘Too much is harmful’.

Hili lipo hata kwenye suala la mapenzi. Ukiwa kila wakati utataka kukutana na mpenzi au mwenza wako faragha, hata ile raha iliyotarajiwa haiwezi kupatikana, matokeo yake itakuwa ni karaha. Nalazimika kuandika makala haya kutokana na ukweli kwamba, huko mtaani kuna baadhi ya watu wameliweka sana mbele suala hili.

Yaani wao kila wakati ni mapenzi… mapenzi…mapenzi….Usiku kucha hawataki hata wenzao wapumzike. Ni mchakamchaka mwanzo mwisho. Sasa huku ni kukomoana au kitu gani? Wengine wapenzi wao hawajisikii kufanya tendo hilo kutokana na kuumwa au kutokuwa na hamu.
Hiyo ni hali ya kawaida kwa binadamu lakini utashangaa mwanaume anakuja na kulazimisha mambo. Huku ni kuumizana na raha haiwezi kupatikana kwa njia hii. Katika lile tendo furaha inapatikana pale kila mmoja anapokuwa anajisikia kuwa faragha na mwenzake.

Ni tendo takatifu linalohitaji maandalizi ya kimwili na kifikra kwa hiyo tusipelekeshane. Wakati mwingine tuzikontroo hisia zetu. Katika hili naomba nishauri yafuatayo; Kwanza tujitahidi sana kujitoa kwenye kundi la watu wenye pepo wa ngono. Tukiwa kwenye kundi hili, si kwa mwanaume tu bali hata kwa wanawake ni lazima tutakuwa ni watu wa kuwaza kufanya mapenzi kila wakati.
Tuwe watu wa kuzishughulisha akili zetu kwa kufanya kazi na kuwaza mambo ya kimaendeleo na si kila wakati kutaka kuwa na wapenzi watu faragha. Itaendelea wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate