
KOCHA Manuel Pellegrini amefanikiwa kutwaa taji la kwanza akiwa bosi wa Manchester City baada ya jana kuifunga Sunderland katika fainali ya Kombe la Capital kwa mabao 3-1kwenye Uwanja wa Wembley jijini London.

Licha ya Sunderland kuanza kufungua ukurasa wa mabao katika dakika ya 10 kupitia kwa Fabio Borini, ilijikuta ikizidiwa nguvu na kupata kipigo hicho kipindi cha pili.
Yaya Touré ndiye aliyefunga bao kali kwa shuti katika dakika ya 55, wapinzani wao hao walijikuta wakipagawa na kufungwa la pili dakika moja baadaye na Samir Nasri.
No comments:
Post a Comment